-
Khatibu wa Swala ya Ijumaa Tehran: Adui anataka kuleta mifarakano; kila mmoja alinde umoja
Aug 28, 2026 12:20Khatibu wa muda wa Swala ya Ijumaa iliyoswaliwa leo hapa mjini Tehran amesisitiza umuhimu wa kuhifadhi umoja katika jamii na kubainisha kwamba, hakuna udhuru wowote unaokubalika wa kuchochea hitilafu na mifarakano.
-
Araghchi: Hali ya Lango Bahari la Hormuz haiwezi kurejea kama ilivyokuwa kabla ya Februari 28
Aug 28, 2026 10:00Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema kuwa hali ya sasa ya eneo la Mashariki ya Kati na Mlango-Bahari wa Hormuz ni matokeo ya mashambulizi ya kijeshi ya Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Pezeshkian amwambia Waziri Mkuu wa Qatar : Iran haitasalimu amri mbele ya mashinikizo na vitisho
Aug 28, 2026 03:31Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa haki zote za kisheria za wananchi wa Iran lazima zitambuliwe ndani ya mfumo wa sheria za kimataifa, akisisitiza kuwa Tehran haitafuti chochote zaidi ya haki zake halali na haitasalimu amri mkabala wa mashinikizo au vitisho.
-
Spika wa Bunge la Iran: Adui atashindwa katika vita kamili vya kiuchumi alivyoanzisha
Aug 28, 2026 03:28Spika wa Bunge la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema: Nchi iko katika vita kamili ya kiuchumi na tutaona jinsi adui atakavyoshindwa katika vita hivi.
-
Mkutano wa Kimataifa wa Umoja wa Kiislamu waanza mjini Tehran
Aug 27, 2026 12:02Mkutano wa 40 wa Kimataifa wa Umoja wa Kiislamu umeanza mjini Tehran, ukijikita zaidi kwenye maono ya Kiongozi marehemu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Shahidi Sayyid Ali Khamenei kuhusu kuimarisha umoja katika Ulimwengu wa Kiislamu.
-
Iran yapendekeza 'mkataba wa usalama wa pande zote' miongoni mwa mataifa ya Kiislamu
Aug 27, 2026 11:59Rais Masoud Pezeshkian wa Iran amependekeza "mkataba wa usalama wa pande zote na kutokuchokozana" miongoni mwa nchi za Kiislamu ili kulinda usalama wa kikanda, hasa katika kipindi hiki ambapo Marekani na Israel zinaendeleza uchokozi wao katika eneo la Asia Magharibi.
-
Kwa nini vita vya kiuchumi vya Trump dhidi ya Iran vinaiathiri Marekani yenyewe?
Aug 27, 2026 06:06Mohammad Bagher Ghalibaf, Spika wa Bunge la Iran, amefananisha mpango mpya wa Marekani wa kutoa mashinikizo ya kiuchumi dhidi ya Iran na 'boomerang,' ambacho ni kifaa cha kurushwa ambacho humrudia aliyekirusha, kwa maana kuwa utawadhuru tu waasisi wake wenyewe.
-
Pezeshkian: Marekani haitapata chochote kupitia mashinikizo ya kiuchumi dhidi ya Iran
Aug 27, 2026 04:32Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa Marekani haitaweza kufanikisha lolote kupitia mashinikizo ya kiuchumi, akisisitiza kuwa Iran itaendelea kusimama imara.
-
Iran yataka UN na nchi wanachama zikatae “ugaidi wa kiuchumi” wa Marekani
Aug 27, 2026 04:28Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Sayyid Abbas Araghchi, amelitaka Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa na nchi wanachama wa umoja huo kukataa kampeni mpya ya Marekani ya ugaidi wa kiuchumi dhidi ya Iran, akisema Washington inalenga kuzilazimisha nchi nyingine kuacha mahusiano halali ya kiuchumi na Tehran kwa kutumia vitisho vya vikwazo.
-
Kamanda wa Kikosi cha Ulinzi wa Anga cha Jeshi la Iran: Iran kupanua kwa mafanikio mifumo ya ulinzi
Aug 27, 2026 04:24Kamanda wa Kikosi cha Ulinzi wa Anga cha Jeshi la Iran amesema kuwa Iran inapiga hatua mbele kwa kutegemea kikamilifu uwezo wake wa ndani, ikipanua mifumo yake ya ulinzi wa anga na kuzalisha nakala za mifumo ile iliyofanya vyema wakati wa vita vya siku 40.