-
Iran yaonya kuhusu wapenda vita wanaotaka “vita vya maafa”
Feb 21, 2026 07:39Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema kuwa Marekani haijawahi kudai kusitishwa kabisa kwa urutubishaji wa urani katika mazungumzo yasiyo ya moja kwa moja yanayoendelea, huku akionya kuwa baadhi ya wenye misimamo mikali wanajaribu kuisukuma sera ya Marekani kuelekea katika “vita visivyo vya lazima na vya maafa.”
-
Russia yasisitizia uungaji mkono wake kwa haki za kisheria za Iran katika mazungumzo ya nyuklia
Feb 21, 2026 02:20Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia imetangaza kuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa nchi hiyo Sergey Lavrov amesema Moscow inaunga mkono kufikiwa suluhisho la kisiasa na kidiplomasia litakaloheshimu haki za kisheria za Iran katika mazungumzo ya nyuklia na Marekani.
-
"Vyombo vya diplomasia vya Iran vijadiliane kwa kuzingatia hekima, izza, na maslahi ya taifa"
Feb 20, 2026 11:33Khatibu wa Swala ya Ijumaa iliyoswaliwa leo hapa mjini Tehran amesema kuwa, "Vyombo vya kidiplomasia (vya Iran) lazima vichore ramani yake ya mazungumzo kwa njia sahihi, ya uwazi na ufasaha, kwa kuzingatia kanuni za heshima, uwazi na hekima, na kuchukua hatua za ujasiri na imara katika njia hii."
-
Iran yaonya: Hatutaanzisha vita, lakini tutajibu vikali uvamizi wowote
Feb 20, 2026 09:48Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa amesisitiza kwamba, Jamhuri ya Kiislamu haitaanzisha vita, lakini itatoa jibu zito kwa kitendo chochote cha uchokozi dhidi ya nchi hii.
-
Majeshi ya majini ya Iran, Afrika Kusini na Sri Lanka kushirikiana usalama baharini
Feb 20, 2026 07:15Kamanda wa Jeshi la Wanamaji wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza udharura wa ushirikiano kati ya vikosi vya majini vya Iran na vile vya Afrika Kusini na Sri Lanka ili kukabiliana na vitisho vya pamoja na kuhakikisha usalama endelevu katika maji ya kimataifa.
-
Mauzo ya nje ya kilimo ya Iran yaongezeka, asilimia 85 ya chakula ni uzalishaji wa ndani
Feb 20, 2026 07:14Waziri wa Jihadi ya Kilimo wa Iran ametangaza ongezeko kubwa la mauzo ya nje ya kilimo hapa nchini hadi dola bilioni nane na kutangaza kwamba asilimia 85 ya usalama wa chakula wa Iran inadhaminiwa na uzalishaji wa ndani.
-
Kiongozi Muadhamu ahudhuria hafla ya Qur'ani siku ya kwanza ya Ramadhani
Feb 20, 2026 03:28Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Seyyed Ali Khamenei amehudhuria kikao cha kiroho cha Qur'ani katika siku ya kwanza ya mwezi mtukufu wa Ramadhani, akijumuika na maqarii na wasomaji mashuhuri wa Iran na kimataifa wa Qur'ani Tukufu.
-
Mawaziri wa Iran na Saudi Arabia wajadili uhusiano wa pande mbili, mazungumzo ya nyuklia kati ya Iran na Marekani
Feb 19, 2026 12:13Mawaziri wa Mashauri ya Kigeni wa Iran na Saudi Arabia wamefanya mazungumzo na kujadili uhusiano wa pande mbili na mchakato wa mazungumzo ya nyuklia kati ya Iran na Marekani
-
Russia yaonya shambulizi dhidi ya Iran linaweza kuwasha moto wa kikanda
Feb 19, 2026 07:46Balozi wa Russia mjini Tehran amezikosoa vikali Marekani na Israel kwa kufuata “sera za uharibifu,” akionya kuwa uchokozi wowote dhidi ya Iran unaweza kusababisha “athari zisizotabirika na zenye maangamizi makubwa” katika eneo la Asia Magharibi na kwingineko duniani.
-
Njama za Israel zimeisukuma Iran kujitegemea katika sekta ya nyuklia
Feb 19, 2026 07:41Mkuu wa Shirika la Nishati ya Atomiki la Iran amesema kuwa njama na vitendo vya uharibifu vilivyotekelezwa na utawala wa Israel dhidi ya mpango wa nishati ya nyuklia wa Jamhuri ya Kiislamu viliilazimisha Iran kuelekea kujitegemea kikamilifu katika sekta ya nyuklia. Alieleza kuwa mchakato huo ulikuwa ni jibu la moja kwa moja kwa shinikizo la muda mrefu na juhudi za makusudi za kuvuruga maendeleo ya nchi.