-
Pezeshkian akumbuka mashambulizi ya mabomu ya atomiki huko Hiroshima na Nagasaki, asema mtazamo uleule bado unatawala Washington
Aug 08, 2026 12:59Rais Masoud Pezeshkian wa Iran amelaani mashambulizi ya mabomu ya nyuklia yaliyofanywa na Marekani dhidi ya miji ya Hiroshima na Nagasaki huko Japan na kueleza kuwa mtazamo fikra zilizopelekea kufanyika mashambulizi hayo bado zipo Washington hii leo.
-
Maafisa wa ngazi ya juu wa Iran wapongeza nafasi ya waandishi wa habari katika kuhami ukweli na umoja wa kitaifa
Aug 08, 2026 12:57Maafisa wa Iran wamewasifu na kuwapongeza waandishi wa habari kutokana na mchango wao wa kukabiliana na taarifa potofu za uhasama na vita vya kisaikolojia, na kusisitiza umuhimu wa vyombo vya habari katika kulinda uelewa wa umma na umoja wa kitaifa.
-
Tabia za Marekani Kudumisha Mvutano katika uhusiano wake na Iran
Aug 08, 2026 06:28Mwenendo wa Rais Donald Trump wa Marekani kuhusiana na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran unachochea kuendelea kwa mvutano na uhasama katika uhusiano wa Washington na Tehran.
-
Iran yayaasa mataifa ya Kiislamu: Ni wakati sasa wa sisi kujitegemea, kuwa na udugu wa kweli
Aug 08, 2026 03:24Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imetoa wito wa kuwepo muunganiko na ushirikiano mkubwa wa kikanda, ikitilia mkazo udharura wa mataifa ya eneo kutegemea uwezo wao wa kikanda ili kuondoa uingiliaji wa kigeni.
-
Spika Qalibaf: Mkakati wa Marekani wa vitisho na kuvunja ahadi umefeli
Aug 07, 2026 03:38Spika wa Bunge la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Mohammad Bagher Qalibaf, amekosoa miamala ya hivi karibuni ya Washington kama “diplomasia ya maigizo” isiyo na mashiko, akitangaza kuwa mkakati wa Marekani wa vitisho, kuvunja ahadi, na kusuka simulizi za uongo umefeli. Aidha amesisitiza kwamba Iran haitashiriki katika michezo hiyo ya kuigiza tena.
-
Waziri wa Ulinzi: Vikosi vya Iran vimesheheni silaha za kujibu mapigo kwa tishio lolote lile
Aug 07, 2026 03:36Kaimu Waziri wa Ulinzi wa Iran amesisitiza kuwa, kwa kutegemea utaalamu wa kiulinzi wa ndani ya nchi, Vikosi vya Ulinzi vya Jamhuri ya Kiislamu vimesheheni kila vinachohitaji ili kutoa jibu kwa tishio lolote lile.
-
Pezeshkian: Iran inajulikana kama nchi yenye nguvu na inayoheshimika; maadui wanalenga nembo za nguvu zake
Aug 06, 2026 11:08Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa licha ya changamoto zinazoikabili nchi, Iran inatambulika kimataifa kama taifa lenye nguvu na linaloheshimika sana, huku akitahadharisha kuwa maadui wa taifa hili wanajaribu kudhoofisha alama za nguvu zake.
-
IRGC: Watu 8 wenye silaha wenye mfungamano na makundi ya kigaidi watiwa nguvuni kusini-mashariki mwa Iran
Aug 06, 2026 11:06Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) kimetangaza kuwa kimewatia nguvuni watu wanane wenye silaha wenye mfungamano na makundi ya kigaidi katika mkoa wa Sistan na Baluchestan kusini-mashariki mwa Iran kufuatia oparesheni maalum mtawalia.
-
Mgawanyiko kati ya Nchi za Kiarabu za Ghuba ya Uajemi Kuhusu Vita vya Marekani dhidi ya Iran
Aug 06, 2026 05:45Kwa mujibu wa gazeti la The Wall Street Journal, nchi za Kiarabu katika eneo la Ghuba ya Uajemi bado zimegawanyika pakubwa kuhusu namna ya kushughulikia vita vya kichokozi na kulazimishwa dhidi ya Iran.
-
Pezeshkian: Iran itaunga mkono maamuzi yatakayochukuliwa na viongozi wa Palestina
Aug 06, 2026 03:53Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Masoud Pezeshkian, amesisitiza kuwa Jamhuri ya Kiislamu itaunga mkono mpango au uamuzi wowote utakaopitishwa na viongozi wa Palestina katika mchakato wa mazungumzo yanayoendelea, akithibitisha tena uungaji mkono thabiti wa Tehran kwa mapambano ya Palestina.