-
Araghchi: Mashauriano ya Beijing yamefanikiwa; Iran yathamini “ushirikiano wa kimkakati” na China
Sep 17, 2026 12:09Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, ameelezea mashauriano yake mjini Beijing kama “yaliyofanikiwa,” akizungumzia maudhui ya safari yake katika mji mkuu huo wa China, ambapo alikutana na mwenzake, Wang Yi.
-
Kamanda wa IRGC: Iran itajibu vikali kosa lolote la kimahesabu la adui
Sep 17, 2026 10:59Kamanda wa Kikosi cha Nchi Kavu cha Jeshi la Iran la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) ameonya kuwa kitendo chochote cha uchokozi kutoka kwa adui kitakabiliwa na jibu kali na thabiti kutoka kwa vikosi vya ulinzi vya Iran.
-
Waziri wa Sayansi wa Iran atahadharisha kuhusu hatari ya Akili Mnemba kuwa "udikteta usioonekana"
Sep 17, 2026 02:49Waziri wa Sayansi, Utafiti na Teknolojia wa Iran, akitoa tahadhari kuhusu madhara ya ufuatiliaji mpana unaotumia Akili Mnemba amesema, hali hiyo inaweza kuweka mazingira ya kubadilisha udhibiti wa data kuwa udhibiti wa watu na hatimaye kusababisha kuibuka “udikteta usioonekana.”
-
Meja Jenerali Amir Hatami: Nguvu halisi ya Iran ni umoja na azma ya wananchi
Sep 16, 2026 12:13Meja Jenerali Amir Hatami Kamanda Mkuu wa Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema katika ujumbe wake wa kupongeza siku 200 za uwepo wa kishujaa wa wananchi wa Iran na kusisitiza kwamba uwepo huo ni dhihirisho la kudumu la imani, mshikamano na azma ya kitaifa, pamoja na kuwa kielelezo cha nguvu na uimara wa ndani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
China: Tuko tayari kutetea kwa nguvu haki za Iran
Sep 16, 2026 12:10Waziri wa Mambo ya Nje wa China amesema kuwa uhusiano na ushirikiano wa nchi yake na Iran ni wa kimkakati na kwamba Beijing inatangaza rasmi kwamba iko tayari kuimarisha mazungumzo na ushirikiano na Iran, na kutetea kwa dhati haki na maslahi halali ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Pakistan: Makubaliano yetu na Saudia hayatoathiri uhusiano wetu na Iran
Sep 16, 2026 12:00Msemaji wa Jeshi la Pakistan amesema kuwa makubaliano ya kijeshi ya nchi yake na Saudi Arabia pamoja na Uturuki maarufu kwa jina la Makubaliano ya Makka, hayatoathiri uhusiano wa Tehran na Islamabad.
-
Iran yashika nafasi ya tatu duniani katika kutibu ugumba, yakamilisha mpango wa chanjo
Sep 16, 2026 02:56Mkuu wa Shirika la Madaktari la Iran amesema kuwa, Jamhuri ya Kiislamu imeshika nafasi ya kwanza duniani katika utoaji wa chanjo na nafasi ya tatu duniani katika kutibuu tatizo la ugumba.
-
Jeshi, IRGC: Iran inawakabili maadui ambao hakuna taifa jengine linalothubutu 'kuwafyatulia hata risasi moja'
Sep 15, 2026 11:38Wasemaji wakuu wa Jeshi la Iran na Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) wameashiria umoja usioweza kuvunjika kati ya matawi hayo mawili ya kijeshi na kutangaza kwamba Iran inavishambulia kwa mafanikio vikosi vya Marekani na Israel, vilivyojizatiti kwa silaha nzito, ambazo hakuna nchi nyingine yoyote duniani inayothubutu kukabiliana nazo.
-
Iran yasema hakuna mazungumzo na Marekani hadi masharti yake yatimizwe
Sep 15, 2026 04:18Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran (SNSC), Meja Jenerali Mohsen Rezaei, amesisitiza kuwa kauli za mkanganyiko na ujumbe unaotatanisha kutoka kwa Rais wa Marekani haupaswi kumpotosha yeyote kutoka kwenye uhalisia mpya uliopo sasa kuhusu mafuta na milango-bahari, akiongeza kuwa hakutakuwa na mazungumzo yoyote hadi masharti yaliyowekwa na Iran yatimizwe kikamilifu.
-
Meli kubwa ya mafuta yalipuka baada ya kukanyaga mabomu ya majini kwenye njia haramu kusini mwa Hormuz
Sep 15, 2026 04:15Kikosi cha Wanamaji cha Jeshi la Iran la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) kimetangaza kuwa meli kubwa ya kubeba mafuta ghafi (supertanker) iliyojaribu kupita bila idhini katika eneo lililopigwa marufuku kusini mwa Lango Bahari la Hormuz imelipuka baada ya kukanyaga mabomu ya kutega majini, huku chombo hicho chote kikiwa kimeteketea na kufunikwa na miali mikubwa ya moto.