-
Ayatullah Khamenei: Mashambulizi ya Marekani na Israel yalishindwa kwa hima na ushujaa wa vijana wa Iran
Dec 27, 2025 09:48Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, amesema mashambulio makubwa ya jeshi la Marekani na mwanaharamu wake katika eneo la Magharibi mwa Asia yalishindwa kutokana na ubunifu, ushujaa na kujitolea kwa vijana wa Iran ya Kiislamu.
-
Ujumbe Kiongozi Muadhamu kwa Umoja wa Jumuiya za Wanafunzi wa Kiislamu barani Ulaya; kubebwa na Iran bendera ya kukabiliana na utaratibu usio wa kiadilifu
Dec 27, 2025 11:11Katika ujumbe wake kwa mkutano wa kila mwaka wa Umoja wa Jumuiya za Wanafunzi wa Kiislamu barani Ulaya, Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu amesisitiza kuwa: "Taifa la Iran kwa kutumia uwezo wake linaweza kusimama na kutoa wito wa thamani za Kiislamu kwa walimwengu kwa sauti kubwa kuliko wakati mwingine wowote."
-
Iran yalaani vikali shambulio baya la kigaidi nchini Syria
Dec 27, 2025 02:47Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imelaani vikali shambulio la kigaidi dhidi ya Waislamu katika Msikiti wa Imam Ali ibn Abi Talib (AS) katika Mkoa wa Homs nchini Syria ambalo limeua shahidi na kujeruhi watu wengi wakati wa Sala ya Ijumaa ya jana Msikitini humo.
-
Mji wa Shiraz; moja ya vituo vikuu vya utalii wa kimatibabu Asia Magharibi
Dec 27, 2025 02:26Chuo Kikuu cha Sayansi ya Tiba cha Shiraz katika Mkoa wa Fars, Iran, kimechukua hatua kubwa za kubadilisha jiji hili kuwa kitovu cha utalii wa matibabu katika Asia Magharibi kwa kufikia makubaliano ya ushirikiano na Uzbekistan na kupanga kupanua mazungumzo na nchi zingine jirani.
-
Ayatullah Khatami: Adui atakumbwa na usiku wa giza iwapo atasababisha madhara kwa Iran
Dec 26, 2025 12:07Khatibu wa Sala ya Ijumaa iliyosaliwa leo hapa mjini Tehran amesisitiza kuwa, uwezo wa makombora wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran utaendelea kuwepo na kwamba: "Maadui watakumbana na usiku wa giza kama wanataka kuidhuru Jamhuri ya Kiislamu.
-
Gharibabadi: Mashambulizi ya adui dhidi ya raia wakati wa vita yamethibitisha suala la nyuklia lilikuwa kisingizio tu
Dec 26, 2025 11:55Kazem Gharibabadi Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Anayehusika na Masuala ya Kisheria na Kimataifa ameissitiza kuwa mashambulizi ya adui dhidi ya raia na makazi ya watu wakati wa vita haramu vilivyoanzisha na Israel kwa kushrikiana na Marekani dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran mwezi Juni mwaka huu yamethibitisha kuwa kadhia ya nyuklia ilikuwa kisingiizo tu cha kuishambulia nchi hii.
-
Araghchi: Vita vya siku 12 vilimalizika kwa heshima, hadhi na ushindi kwa Iran
Dec 26, 2025 03:25Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema kwamba Jamhuri ya Kiislamu ilijihami kwa njia halali mbele ya uvamizi haramu wa adui, na hatimaye adui akalazimika kuomba kusitisha mapigano bila ya masharti na hivyo, Vita vya Siku 12 vilimalizika kwa heshima na ushindi kwa taifa la Iran.
-
Rais Pezeshkian ampongeza Papa kwa mnasaba wa Krismasi na Mwaka Mpya
Dec 25, 2025 11:54Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ametuma salamu kwa Papa Leo wa XIV, kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani, akimpongeza kwa mnasaba wa kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Nabii Isa (amani iwe juu yake) na kuwadia Mwaka Mpya wa 2026.
-
IRGC yanasa meli iliyobeba lita milioni 4 za mafuta ya magendo
Dec 25, 2025 07:18Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu la Iran (IRGC) limekamata meli iliyokuwa imebeba shehena kubwa ya mafuta ya magendo katika maji ya Ghuba ya Uajemi.
-
Iran yasuta 'diplomasia ya mabomu' ya Marekani
Dec 25, 2025 06:40Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi amekejeli na kukosoa vikali tafsiri ya Marekani ya 'diplomasia' katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, akisisitiza kuwa, uwazi na utayarifu kwa mazungumzo hauna mfungamano wowote na kuuripua kwa mabomu upande wa pili wakati wa majadiliano.