-
Araghchi: Vita vya siku 12 vilimalizika kwa heshima, hadhi na ushindi kwa Iran
Dec 26, 2025 03:25Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema kwamba Jamhuri ya Kiislamu ilijihami kwa njia halali mbele ya uvamizi haramu wa adui, na hatimaye adui akalazimika kuomba kusitisha mapigano bila ya masharti na hivyo, Vita vya Siku 12 vilimalizika kwa heshima na ushindi kwa taifa la Iran.
-
Rais Pezeshkian ampongeza Papa kwa mnasaba wa Krismasi na Mwaka Mpya
Dec 25, 2025 11:54Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ametuma salamu kwa Papa Leo wa XIV, kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani, akimpongeza kwa mnasaba wa kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Nabii Isa (amani iwe juu yake) na kuwadia Mwaka Mpya wa 2026.
-
IRGC yanasa meli iliyobeba lita milioni 4 za mafuta ya magendo
Dec 25, 2025 07:18Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu la Iran (IRGC) limekamata meli iliyokuwa imebeba shehena kubwa ya mafuta ya magendo katika maji ya Ghuba ya Uajemi.
-
Iran yasuta 'diplomasia ya mabomu' ya Marekani
Dec 25, 2025 06:40Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi amekejeli na kukosoa vikali tafsiri ya Marekani ya 'diplomasia' katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, akisisitiza kuwa, uwazi na utayarifu kwa mazungumzo hauna mfungamano wowote na kuuripua kwa mabomu upande wa pili wakati wa majadiliano.
-
UWW: Muirani Amouzad ndiye mwanamieleka 'Aliyetamalaki Zaidi' duniani 2025
Dec 25, 2025 05:42Muungano wa Mieleka Duniani (UWW) umemtaja Rahman Amouzad kutoka Iran kuwa mwanamieleka wa mtindo wa freestyle (kujiachia) "Aliyeng'ara Zaidi" kwa mwaka huu 2025.
-
Iran yasema haikubali ukaguzi wa vituo vya nyuklia vilivyoshambuliwa
Dec 25, 2025 03:32Mkuu wa Shirika la Nguvu za Atomiki la Iran (AEOI) amesema kuwa shinikizo la kisiasa na kisaikolojia kuhusu ukaguzi wa vituo vya nyuklia vilivyoharibiwa katika mashambulizi ya Israel na Marekani halitakuwa na athari yoyote, akisisitiza haja ya kuwepo taratibu zilizo wazi kwa hali kama hizo.
-
Wabunge 150 wa Iran walaani chokochoko za Marekani nchini Venezuela
Dec 24, 2025 11:31Kundi la wabunge 150 wa Iran limeilaani vikali Marekani kwa chokochoko zake huko Venezuala na kuzuia meli za mafuta katika Bahari ya Karibi, likisema kuwa vitendo hivyo vya Washington ni uharamia wa baharini na ni tishio kwa utulivu na usalama wa ukanda huo.
-
Iran, Russia na China Zaungana katika Kupinga Snapback
Dec 24, 2025 10:32Wawakilishi wa Iran, Russia na China katika Umoja wa Mataifa wamesisitiza, katika mkutano wa Baraza la Usalama la umoja huo, kwamba madai ya Marekani pamoja na Uingereza na Ufaransa, hayakuwa halali kuhusu kurejeshwa mara moja na bila masharti vikwazo vya UN dhidi ya Jamhuri ya Kislamu maarufu kama snapback.
-
Mwakilishi wa Iran UN: Baada ya Oktoba 2025, Azimio 2231 halikuwa tena na itibari ya kisheria
Dec 24, 2025 06:47Mwakilishi wa Iran katika kikao cha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa cha kujadili Azimio 2231 amesema, Jamhuri ya Kiislamu inakubaliana na misimamo ya Russia na China ya kupinga kuitishwa kwa kikao hicho. Azimio 2231 lina kifungu kinachoeleza bayana kwamba muda wake wa kumalizika ni Oktoba 2025, na baada ya hapo hakutakuwa tena na msingi wa kisheria wa kuendelea majukumu ya azimio hilo.
-
Araqchi na Abdul Ati wakubaliana kuimarishwa uhusiano wa Iran na Misri
Dec 24, 2025 02:58Mawaziri wa Mashauri ya Kigeni wa Iran na Misri wamekubaliana kwa njia ya simu kuimarisha uhusiano wa pande mbili kati ya Tehran na Cairo na matukio muhimu ya kieneo na kimataifa.