-
Jeshi la Iran: Medani mpya za mapambano zitafunguliwa ikiwa adui atatumbukia katika mtego wa Israel
May 20, 2026 03:26Jeshi la Iran limeonya kuwa iwapo adui ataanguka tena katika mtego wa Israel na kuanzisha uchokozi mwingine dhidi ya Iran, jeshi la taifa litafungua medani mpya ya mapambano kwa kutumia zana na mbinu mpya.
-
Kulegeza kamba mara kwa mara Trump, ishara ya kuemewa mbele ya Iran
May 20, 2026 03:01Pars Today - Rais wa Marekani Donald Trump, kwa mara ya kumi na moja katika kipindi cha wiki chache tu, amerudia tena majigambo yake ya kuishambulia Iran lakini baadaye anatafuta kisingizio cha kuakhirisha kushambulia.
-
Intelijensia ya Iran yasambaratisha kundi la magaidi wa kitakfiri wenye uhusiano na Israel
May 20, 2026 02:50Timu za upelelezi za Iran zimefanikiwa kusambaratisha seli nne za wanamgambo wa Kitakfri wenye mfungamano na utawala wa Israel katika mkoa wa Sistan na Baluchistan, kusini mashariki mwa Iran mkoa unaopakana na Pakistan.
-
Mshauri wa Kiongozi Muadhamu: Taifa la Iran na vikosi vya jeshi vitailazimisha Marekani kusalimu amri
May 19, 2026 12:48Mshauri mkuu wa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyid Mojtaba Khamenei amesema kwamba mkono wa chuma wa vikosi vya jeshi na taifa thabiti la Iran vitailazimisha Marekani kurudi nyuma na kusalimu amri.
-
'Hatutasalimu amri kamwe': Pezeshkian aapa kuendeleza mapambano huku Trump akizidi kupiga ngoma za vita
May 19, 2026 05:51Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian, ameapa kutosalimu amri kamwe mbele ya dola lolote au kutoa kafara heshima ya taifa kwa ajili ya faraja.
-
Rais wa Iran: Marekani, Israel zinapandikiza chuki baina ya Waislamu
May 18, 2026 12:11Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian, amesema kwamba tawala za Marekani na Israel zinaendeleza miradi ya kuzusha migawanyiko na kueneza hali ya kutoaminiana ili kuyagonganisha mataifa ya Kiislamu.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran azungumza na wenzake huku mvutano na Marekani ukitokota
May 18, 2026 12:08Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, amefanya mazungumzo ya simu kwa nyakati tofauti na mawaziri wenzake wa Ufaransa, Qatar, Uturuki, na Korea Kusini, siku ya Jumapili, ili kutathmini mahusiano ya pande mbili, matukio ya kieneo na mchakato wa kidiplomasia unaoendelea.
-
Velayati aikosoa Marekani kwa vitisho dhidi ya Iran, aonya inaangukia “mtego” wa Israel
May 18, 2026 04:40Ali Akbar Velayati, mshauri mwandamizi wa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, ameonya kuwa Marekani inaangukia “mtego wa kimkakati” uliotegwa na Israel, akisema kuwa Marekani itapoteza kabisa mabaki ya uaminifu wake katika eneo la Asia Magharibi iwapo itaanzisha vita vingine dhidi ya Iran.
-
Spika Qalibaf: Muqawama wa kihistoria wa Iran unaongeza kasi ya mabadiliko ya kimataifa ambayo hayajawahi kutokea
May 17, 2026 11:25Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran (Bunge) Mohammad Baqir Qalibaf amesema kuwa muqawama wa kishujaa wa taifa la Iran kwa muda wa siku 70 umekuwa msukumo katika kuharakisha mageuzi ambayo hayajaonekana katika karne moja, na hivyo kuashiria mapambazuko ya mfumo mpya wa kambi kadhaa.
-
Mshauri wa ngazi ya juu wa Kiongozi Muadhamu: Uvumilivu haupo siku zote/ Azitahadharisha nchi za Kiarabu za Ghuba ya Uajemi
May 17, 2026 11:10Mshauri wa ngazi ya juu wa Kiongozi Muadhamu: Uvumilivu haupo siku zote/ Azitahadharisha nchi za Kiarabu za Ghuba ya Uajemi