-
Qalibaf: Vita vya siku 12 vimethibitisha kuwa 'uadui' wa Marekani dhidi ya Iran 'unaendelea'
Nov 04, 2025 12:48Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Baqer Qalibaf, ametangaza kwamba vita vya hivi karibuni vya siku 12 vimefichua uadui unaoendelea wa Marekani, akisisitiza kwamba ingawa mbinu zake zimebadilika, lakini lengo lake la msingi la kupinga Iran yenye nguvu na huru bado halijabadilika.
-
Tehran yasema 'vita halisi vya kikanda' na Israel vinaendelea, yapuuza mazungumzo na Marekani
Nov 04, 2025 11:37Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje ya Iran amesema kwamba eneo la Magharibi mwa Asia kwa sasa limo katika na "vita halisi" na utawala wa Israel, akisisitiza kwamba hali ya eneo hilo iimekwenda mbali zaidi ya vitisho tu.
-
Tarehe 13 Aban; dhihiriisho la mshikamano wa kitaifa kwa ajili ya kukabiliana na sera za uingiliaji kati za Marekani nchini Iran
Nov 04, 2025 10:32Tarehe 13 Aban (4 Novemba) inafahamika katika kalenda ya Iran kama "Siku ya Taifa ya Kupambana na Uistikbari Duniani".
-
Maandamano ya Siku ya Kupambana na Ubeberu yanaendelea hivi sasa kwenye miji 900 ya Iran
Nov 04, 2025 07:01Maandamano ya Siku ya Mwenyezi Mwenyezi Mungu yaani Aban 13 ambayo ni Siku ya Taifa ya Iran ya Kupambana na ubeberu na uistikbari yanaendelea hivi sasa hapa mjini Tehran na katika zaidi ya miji 900 kote humu nchini.
-
Jeshi la Iran lasema limejiandaa kulinda usalama wa taifa dhidi ya vitisho
Nov 04, 2025 02:55Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran limesema limejiandaa na limesimama thabiti mbele ya vitisho vya maadui, na linaendelea kujitolea kulinda mipaka ya ardhi na mfumo wa Kiislamu.
-
Kwa nini Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inasisitiza kulinda mafanikio ya sekta ya nyuklia?
Nov 04, 2025 02:22Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ametembelea Shirika la Nishati ya Atomiki la Iran (AEOI) na kushuhudia kwa karibu mafanikio ya karibuni ya wanasayansi wa sekta ya nyuklia katika nyanja za afya, tiba na utengenezaji dawa za radiopharmaceutical na kisha kuzungumza na maafisa wa ngazi ya juu wa sekta hiyo.
-
Kiongozi wa Mapinduzi: Mzozo uliopo kati ya Iran na Marekani ni wa dhati halisi na wa migongano ya maslahi
Nov 03, 2025 13:25Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyid Ali Khamenei amesema, mzozo uliopo kati ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Marekani ni wa "dhati halisi" na wala hautokani na kauli mbiu; na chimbuko lake liko kwenye mgongano wa kimsingi wa maslahi; na akaeleza bayana kwamba, suala la ushirikiano na Marekani linaweza kuja kufikiriwa siku za usoni na si sasa hivi wala katika muda wa karibu,
-
Baghaei: Utawala wa Israel ulikiuka usitishaji vita Gaza tangu mwanzo
Nov 03, 2025 10:12Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Iran ameashiria kuendelea jinai za utawala wa Kizayuni wa Israel huko Gaza na kusisitiza kuwa: "Tangu maelewano ya amani yalipoanzishwa na kuanzishwa usitishaji vita huko Gaza, badala ya dhana ya "kusitisha mapigano," tunakabiliwa na ukweli wa "ukiukaji wa usitishaji vita."
-
Iran: Tumejiandaa zaidi hivi sasa hata kuliko kabla ya vita vya siku 12
Nov 03, 2025 06:34Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Sayyid Abbas Araghchi amesema kwamba Jamhuri ya Kiislamu imejiandaa zaidi kwa vita hivi sasa kuliko hata ilivyokuwa kabla ya vita vya siku 12 akisisitiza kwamba Tehran haiziamini ahadi za Israel wala Marekani lakini iko tayari kwa mazungumzo ya kiuadilifu yaatakayolinda haki zake zote za nyuklia.
-
Araqchi akadhibisha madai ya Marekani na Israel kuhusu mpango wa nyuklia wa Iran, asema ni uongo mtupu
Nov 03, 2025 03:01Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araqchi, kwa mara nyingine tena amepinga hatua ya Marekani na Israel ya kuhalalisha mashambulizi dhidi ya vituo vya nyuklia vya Iran, akiitaja kuwa ni uongo mkubwa.