-
Pezeshkian amwambia Macron: Iran yataka diplomasia huku ikisisitiza kulinda haki za taifa
May 07, 2026 08:07Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Masoud Pezeshkian, amemwambia mwenzake wa Ufaransa, Emmanuel Macron, kuwa Tehran iko tayari kuendelea kwa dhati na njia za kidiplomasia ili kukomesha vita, huku ikisisitiza umuhimu wa kulindwa haki za taifa la Iran.
-
China yalaani vita dhidi ya Iran, yataka usitishaji kamili wa mapigano
May 07, 2026 08:03China imemkaribisha Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, kwa mazungumzo mjini Beijing, huku Waziri wa Mambo ya Nje wa China, Wang Yi, akivitaja vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran kuwa “visivyo halali” na kutoa wito wa kusitishwa kabisa kwa mapigano.
-
Iran imewasilisha nyaraka kuhusu jinai za kivita za Marekani na Israel
May 07, 2026 07:53Mkuu wa Shirika la Hilali Nyekundu la Iran amesema wamewasilisha nyaraka 35 zinazoonyesha wazi jinai za kivita zilizofanywa na Marekani na Israel wakati wa mashambulizi ya hivi karibuni dhidi ya Iran, katika taasisi mbalimbali za kimataifa.
-
Sababu Gani Zinaifanya UAE Ishupalie Vita Dhidi ya Iran?
May 06, 2026 11:21Muungano wa Falme za Kiarabu, UAE au Imarati umechukua msimamo wa waziwazi wa kushupalia vita hususan dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Pezeshkian: Iran inasimamia nguvu ya Maadili na Uwajibikaji
May 06, 2026 10:58Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza kuwa Iran inasimamia nguvu inayojali maadili na uwajibikaji huku akiwatuhumu maadui zake kwa kuwakilisha nguvu zisizo na uwajibikaji.
-
Iravani akanusha vikali azimio la Arab League dhidi ya Iran, asema ni la upendeleo
May 06, 2026 10:43Balozi wa Iran katika Umoja wa Mataifa amejibu azimio la kikao cha Jumuiya ya Nchi za Kiarabu (Arab Legue) dhidi ya Iran kilichofanyika mjini Cairo akisema kuwakingia kifua wavamizi hakuwezi kubadili ukweli wa kisheria.
-
Iran yazindua utaratibu mpya wa kudhibiti meli zinazopita Mlango Bahari wa Hormuz
May 06, 2026 08:07Iran imezindua rasmi mfumo mpya wa udhibiti wa usafiri wa majini katika Mlango Bahari wa Hormuz.
-
Trump ataka kufichwa picha za vituo vya Marekani vilivyoharibiwa na Iran
May 05, 2026 11:44Donald Trump, Rais wa Marekani, amezitaka kampuni za satalaiti kuficha picha za vituo na kambi za kijeshi za Marekani zilizoharibiwa na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika eneo la Asia ya Magharibi.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran: Matukio ya Hormuz yadhihirisha kuwa suluhisho la kijeshi halipo
May 05, 2026 05:39Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Seyed Abbas Araghchi, amesema kuwa matukio ya karibuni katika Mlango wa Bahari wa Hormuz yameweka wazi tena kwamba hakuna suluhisho la kijeshi kwa mgogoro wa kisiasa unaoikumba kanda ya Asia Magharibi, akisisitiza upya sera ya Jamhuri ya Kiislamu ya kufuatilia diplomasia kutoka katika nafasi ya nguvu.
-
Viongozi wa Kisunni watoa wito wa msaada wa ulimwengu kwa Iran
May 05, 2026 05:34Wanazuoni wa Kisunni kutoka pembe zote za dunia wamehimiza umoja wa Kiislamu na kutoa wito wa kuungwa mkono kwa Iran, katika kongamano la kipekee lililofanyika Jumatatu asubuhi chini ya uratibu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Kukurubisha Madhehebu za Kiislamu yenye makao yake Tehran.