-
Mamilioni ya Wairani washiriki maombolezo kuelekea siku ya Ashura
Jun 24, 2026 11:04Mamilioni ya Waislamu katika Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na maeneo mengine ya dunia leo mchana wameshiriki katika maombolezo ya kumbukumbu ya Ta'asua na jioni hii wanashiriki katika hafla za mkesha wa Ashura ambayo ni kukumbuka siku ya kuuliwa shahidi mjukuu wa Mtume Muhammad (SAW), Imam Hussein bin Ali bin Abi Twalib (AS).
-
Pezeshkian: Iran haitazungumzia uwezo wake wa kjeshi, asema makombora yameiepusha Iran na hatima ya Gaza
Jun 24, 2026 10:59Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian, amesisitiza kuwa Tehran haitawahi kamwe kufanya mazungumzo yoyote kuhusu uwezo wake wa ulinzi na kuzuia uchokozi (deterrence), akibainisha kuwa ghala la makombora la nchi hii ndilo limeiweka Iran salama dhidi ya kukumbwa na hatima ya Gaza.
-
Seneti yapitisha azimio la kuondoa wanajeshi wa Marekani kwenye vitani na Iran
Jun 24, 2026 03:55Seneti ya Marekani imepiga kura ya kuidhinisha azimio la kuwaondoa wanajeshi wa Marekani kwenye vita na Iran, katika hatua ambayo imetajwa na wachambuzi wa mambo kuwa ni kielelezo cha pigo la kisiasa kwa Rais Donald Trump.
-
Kamanda: Jeshi la Iran bado halijaonesha uwezo wake kamili
Jun 24, 2026 03:45Majeshi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran yamebadili mwelekeo wa kimkakati kutoka kwenye ulinzi pekee na kuelekea kwenye mafundisho ya kijeshi ya mashambulizi (offensive military doctrine), huku operesheni za kutangulia kumzuia adui (preemptive operations) zikiwa sasa mezani.
-
Spika Qalibaf akutana na Sultani wa Oman kufuatia mazungumzo ya Uswisi
Jun 24, 2026 03:40Spika wa Bunge la Iran ambaye pia ni mkuu wa timu ya mazungumzo na Marekani, Mohammad Baqer Qalibaf, amekutana na Sultani Haitham bin Tariq wa Oman jijini Muscat, ambapo wamejadili uhusiano wa nchi mbili na matukio ya hivi karibuni kuhusu Mkataba wa Maelewano (MoU) kati ya Tehran na Washington.
-
Iran na Oman zajadili utaratibu mpya wa kusimamia Lango-Bahari la Hormuz
Jun 23, 2026 10:49Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Baqer Qalibaf na Waziri wa Mambo ya Nje Abbas Araghchi wamekutana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Oman, Sayyid Badr bin Hamad al-Busaidi, kujadili utaratibu mpya wa kusimamia Lango-Bahari la kimkakati la Hormuz.
-
Pezeshkian: Kuwajibika kwa Marekani ndio sharti la kuendelea mazungumzo
Jun 23, 2026 10:33Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ametilia mkazo umuhimu wa kutekelezwa makubaliano yaliyofikwa baina ya Iran na Marekani kwa ajili ya kuendelezwa mazungumzo kati ya pande hizo kuhusu utekelezaji wa mkataba wa maelewano uliosainiwa hivi karibuni.
-
Spika wa Bunge la Iran aapa kuwa mwaminifu kwa mashahidi baada ya kuwasili Uswisi kwa mazungumzo na US
Jun 21, 2026 04:41Spika wa Bunge la Iran amesisitiza tena kwamba atatetea haki za Wairani waliouawa shahidi wakati wa mashambulizi ya Marekani na Israel dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu baada ya kuwasili Uswisi kufuatilia mkataba wa Hati ya Maelewano uliosainiwa na viongozi wa nchi mbili kwa lengo la kukomesha vita.
-
Picha ya mazishi ya wanafunzi wa Shule ya Msingi ya Minab yashinda tuzo ya picha bora zaidi ya mwaka
Jun 21, 2026 02:58Picha iliyochukuliwa kutokea angani inayoonyesha mazishi ya wanafunzi 168 waliouawa shahidi wakati wa shambulio la makombora ya Marekani dhidi ya Shule ya Msingi ya Shajareh Tayyebeh huko Minab, kusini mwa Iran, imeshinda tuzo ya juu katika Kategoria ya Upigaji Picha za Habari ya tuzo za Golden Shot Photography Awards 2026.
-
Qalibaf: Tozo ya kupita Mango Bahari la Hormuz baada ya siku 60 imejumuishwa katika Hati ya Makubalino (MoU)
Jun 19, 2026 03:40Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran (Bunge), Mohammad Baqer Qalibaf, ambaye anaongoza timu ya mazungumzo na Marekani, ameeleza kuwa malipo ya kuvuka katika Lango-Bahari la Hormuz yamejumuishwa kwenye Hati ya Makubaliano baina ya pande hizo mbili na kwamba kupita katika lango hilo katika kipindi hiki cha siku 60 cha mazungumzo kutakuwa bure.