Pars Today

Kiswahili
  • Nyumbani
  • Radio
  • Albanian shqip
  • Armenian Հայերեն
  • Assyrian ܐܬܘܪ̈ܝܐ
  • Azeri Azəri
  • Bangla বাংলা
  • Chinese 中文
  • Dari دری
  • English English
  • French français
  • German Deutsch
  • Hausa Hausa
  • Hebrew עברית
  • Hindi हिन्दी
  • Indonesian Bahasa Indonesia
  • Italian Italiano
  • Japanese 日本語
  • Kazakh қазақ тілі
  • Kiswahili Kiswahili
  • Pashto پښتو
  • Persian فارسی
  • Russian Русский
  • Spanish Español
  • Tajik Тоҷик
  • Taleshi Tolışə
  • Turkish Türkçe
  • Turkmen Türkmen
  • Uzbek узбек
  • Dunia
  • Asia Magharibi
  • Iran
  • Afrika
  • Dini
  • Parspedia
  • Disinfo

Iran

  • Rais wa Iran aihimiza BRICS kulinda kanuni ya kutotumia mabavu

    Rais wa Iran aihimiza BRICS kulinda kanuni ya kutotumia mabavu

    Sep 13, 2026 11:29

    Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Dkt. Masoud Pezeshkian, ametoa wito kwa kundi la mataifa yanayoinukia kiuchumi la BRICS kuchukua jukumu “lenye ufanisi zaidi” katika kulinda mamlaka ya kitaifa na kusimamia kanuni ya kimataifa ya kutotumia nguvu, hasa katika kipindi hiki cha sasa chenye changamoto nyingi.

  • Pezeshkian ahimiza BRICS kuunda mtandao imara wa kibiashara na kutumia sarafu za kitaifa

    Pezeshkian ahimiza BRICS kuunda mtandao imara wa kibiashara na kutumia sarafu za kitaifa

    Sep 12, 2026 04:34

    Rais Masoud Pezeshkian amezihimiza nchi wanachama wa jumuiya ya BRICS kujenga mtandao thabiti na wenye uwezo wa kustahimili misukosuko ya kibiashara, sambamba na kupanua matumizi ya sarafu za kitaifa ili kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi na kupunguza uwezekano wa kuathiriwa na mshtuko wa kisiasa.

  • Iran: Mamlaka ya kujitawala ya Yemen lazima yaheshimiwe, mzingiro haramu lazima ukomeshwe

    Iran: Mamlaka ya kujitawala ya Yemen lazima yaheshimiwe, mzingiro haramu lazima ukomeshwe

    Sep 12, 2026 04:31

    Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imesisitiza tena msimamo wake thabiti na wa kimisngi kuhusu ulazima wa kuheshimiwa uhuru, mamlaka ya kitaifa ya kujitawala na umoja wa ardhi yote ya Yemen, na kutoa wito wa kukomeshwa mara moja mzingiro haramu na usio wa kibinadamu uliowekwa dhidi ya nchi hiyo.

  • Iran yazindua programu mpya ya kinga-virusi iliyotengenezwa nchini

    Iran yazindua programu mpya ya kinga-virusi iliyotengenezwa nchini

    Sep 08, 2026 04:39

    Sambamba na maonyesho ya kimataifa ya Iran ya ELECOMP 2026, ambayo ni maonyesho makubwa zaidi ya nchi kwa sekta za elektroniki, teknolojia za kompyuta, na biashara pepe (e-commerce), Iran imezindua programu yake ya pili ya kinga-virusi (antivirus) iliyotengenezwa nchini, ijulikanayo kama Ayyza. Programu hii hutumia akili mnemba (AI) na mbinu za kujifunza kwa mashine (machine learning) kutambua virusi vipya visivyojulikana na vitisho vya mtandaoni ambavyo havijatambulika awali.

  • Qatar imethibitisha kuwa mashambulio ya Iran ndani ya ardhi ya nchi hiyo yalilenga vituo vya kijeshi tu vya Marekani

    Qatar imethibitisha kuwa mashambulio ya Iran ndani ya ardhi ya nchi hiyo yalilenga vituo vya kijeshi tu vya Marekani

    Sep 04, 2026 03:22

    Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Esmaeil Baghaei, ameashiria hati rasmi ya Qatar iliyowasilishwa kwa Umoja wa Kimataifa wa Mawasiliano (ITU) ikithibitisha kwamba operesheni halali za kujihami za Jamhuri ya Kiislamu dhidi ya vikosi vya Marekani vilivyoko katika ardhi ya Qatar zilielekezwa kwenye vituo vya kijeshi tu vya Marekani.

  • Qalibaf: Iran na kambi ya Muqawama wako katika njia moja dhidi ya ubeberu

    Qalibaf: Iran na kambi ya Muqawama wako katika njia moja dhidi ya ubeberu

    Sep 03, 2026 03:26

    Spika wa Bunge la Iran amesema kuwa Iran na kambi ya Muqawama wako katika njia moja kukabiliana na ubeberu.

  • Pezeshkian: Marekani ilikiuka MoU ya Islamabad, ikahamia kwenye madai ya kuchupa mipaka ndani ya wiki mbili

    Pezeshkian: Marekani ilikiuka MoU ya Islamabad, ikahamia kwenye madai ya kuchupa mipaka ndani ya wiki mbili

    Sep 01, 2026 14:56

    Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza kwamba usalama endelevu haupatikani kupitia makabiliano, bali kupitia njia ya kuaminiana, kuheshimu mamlaka ya kujitawala ya nchi nyingine, kutoingilia mambo yao ya ndani, na ushirikiano kati ya serikali, na ametoa wito wa kuimarishwa ushirikiano wa kiusalama na kiuchumi katika Shirika la Ushirikiano la Shanghai.

  • Iran yatangaza mashtaka rasmi dhidi ya Marekani na Israel kuhusu mauaji ya kigaidi ya Kiongozi Muadhamu na wanafunzi wa Minab

    Iran yatangaza mashtaka rasmi dhidi ya Marekani na Israel kuhusu mauaji ya kigaidi ya Kiongozi Muadhamu na wanafunzi wa Minab

    Aug 30, 2026 03:48

    Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imetoa hati rasmi za mashtaka kufuatia vitendo vya kigaidi vilivyofanywa na muungano wa Marekani na Israel, ambavyo vilisababisha kuuawa kishahidi kwa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, pamoja na wanafamilia wake wanne, sambamba na wanafunzi na walimu katika shule moja mjini Minab.

  • Mauzo ya Mafuta ya Iran kwa China yaimarika licha ya vita vya kiuchumi vya Marekani

    Mauzo ya Mafuta ya Iran kwa China yaimarika licha ya vita vya kiuchumi vya Marekani

    Aug 30, 2026 03:35

    Takwimu mpya zinaonyesha kuwa mauzo ya mafuta ya petroli ya Iran kuelekea China yameendelea kuwa imara kwa kiasi kikubwa mwaka huu, licha ya Marekani kushadidisha vita vyake vya kiuchumi na kijeshi dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu, huku Tehran ikithibitisha kuendelea kwa usambazaji wa mafuta ghafi kwa wateja wake wa kimataifa bila kusitishwa.

  • Kiongozi Mkuu: Utatuzi wa masuala ya kiuchumi uko kwenye uzalishaji wa ndani na kufuta sarafu ya dola

    Kiongozi Mkuu: Utatuzi wa masuala ya kiuchumi uko kwenye uzalishaji wa ndani na kufuta sarafu ya dola

    Aug 29, 2026 04:46

    Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyid Mojataba Khamenei ameipongeza serikali ya Rais Masoud Pezeshkian kwa kushughulikia mahitaji ya wananchi wakati nchi inakabiliwa na vita vya kichokozi vya Marekani na Israel na mzingiro wa baharini wa Marekani na akahimiza kuongezwa uzalishaji wa ndani na kuifuta sarafu ya dola ya Marekani katika miamala ya kifedha.

Onesha Zaidi
Pars Today

© 2026 PARS TODAY. All Rights Reserved.

Habari
    Dunia
    Asia Magharibi
    Iran
    Afrika
    Dini
    Parspedia
    Disinfo
Pars Today
    SISI NI
    Wasiliana Nasi
    RSS