-
Vibaraka wawili wa Mossad wanyongwa nchini Iran kwa kutoa taarifa za usalama kwa Israel
Aug 03, 2026 09:48Wanaume wawili waliopatikana na hatia ya kufanya ujasusi kwa maslahi ya shirika la ujasusi la Israel, Mossad, wamenyongwa kwa kosa la kutoa taarifa nyeti kuhusu jeshi na maeneo ya usalama ya Iran katika vita vya hivi karibuni vya Marekani na Israel.
-
Baada ya Iran kuapa kuwa itajibu mapigo makali, Trump asitisha mashambulizi dhidi ya miundombinu
Aug 02, 2026 13:15Rais wa Marekani Donald Trump amesema amefuta mashambulizi aliyotangaza kuwa yatafanywa dhidi ya Iran baada ya nchi za eneo kuomba yasitishwe wakati juhudi zinafanywa ili kufikia makubaliano, na kufuatia maonyo yaliyotolewa na Tehran kwamba uchokozi wowote mpya wa Marekani au Israel utakabiliwa na jibu la mapigo makali.
-
Abdel Bari Atwan: Makamanda wa jeshi la Marekani wanahofia kurudiwa "tajiriba ya Vietnam"
Aug 02, 2026 13:06Abdel Bari Atwan, mchambuzi mashuhuri katika Ulimwengu wa Kiarabu ameashiria jinsi Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ilivyojiandaa kutoa kipigo kikali dhidi ya uchokozi wowote, na hofu ya makamanda wa kijeshi wa Marekani ya kujirudia tajriba ya Vita vya Vietnam, na kutaja sababu tano zilizomfanya Trump arudi nyuma katika kutekeleza vitisho vyake.
-
Araqchi: Iran iko tayari kukabiliana na uvamizi wowote mpya wa Marekani
Aug 02, 2026 03:14Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araqchi ameonya dhidi ya kitendo chochote kipya cha uvamizi cha Marekani dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu, akisisitiza kwamba Tehran iko tayari kikamilifu kukabiliana na makosa yoyote kama hayo.
-
Umoja wa Mataifa waonya kuhusu utumiaji wa mada zilizopigwa marufuku dhidi ya raia wa Iran
Aug 01, 2026 11:26Maripota wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa wametoa taarifa ya pamoja, wakisema kuwa raia 3,375 wa Iran wameuawa katika mashambulizi ya kikatili ya Marekani na Israel (wakiwemo wanawake wapatao 500), na kutoa wito wa kuwajibishwa Marekani na Israel kwa uhalifu wao wa kivita, hasa kuhusu janga la shule ya msingi ya Minab.
-
Droni za Jeshi la Iran zashambulia vituo vya kimkakati vya Marekani nchini Kuwait
Jul 31, 2026 09:59Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran limeshambulia vituo vya kimkakati vya jeshi la kigaidi la Marekani katika kambi ya Ahmed al-Jaber huko Kuwait kwa kutumia ndege zisizo na rubani zenye uharibifu mkubwa.
-
Baghaei amhoji Guterres; kwa nini unahepa kuwataja wavurugaji wawili wakuu wa sheria za kimataifa?
Jul 31, 2026 03:40Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameashiria matamshi ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu kupuuzwa kwa sheria za kimataifa kwa namna inayotisha, na kumhutubu yeye kwa kumwambia: "Sasa ni wakati wa kutimiza jukumu lako zito na kusaidia kuzuia Umoja wa Mataifa na mfumo wa kanuni zake kutofikwa na hatima ya Jumuiya ya Mataifa."
-
Zaidi ya watu milioni 2 wavuka mipaka ya Iran kwa ajili ya Arubaini ya Imam Hussein (AS)
Jul 31, 2026 03:33Zaidi ya mazuwari milioni mbili wa Iran wamevuka salama mipaka ya nchi ili kuhudhuria shughuli ya kila mwaka ya Arubaini ya Imam Hussein, mojawapo ya mikusanyiko mikubwa zaidi ya kidini duniani, inayofanyika katika mji mtakatifu wa Karbala nchini Iraq.
-
Mashambulizi ya kulipiza kisasi ya Iran yaharibu ndege tatu za F-35 katika kambi ya Marekani huko Jordan
Jul 30, 2026 14:59Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran (IRGC) limetangaza kuwa limefanya mashambulizi ya makombora ya balestiki kwenye Kituo cha Anga cha Muwaffaq Salti kinachoendeshwa na jeshi la Marekani huko Azraq, nchini Jordan, na kuharibu ndege tatu za kivita za Marekani aina ya F-35 na kusababisha madhara makubwa kwa ndege nyingine tatu, katika operesheni ya kulipiza kisasi kwa shambulio la anga la Marekani lililoua watu watatu wa familia moja kwenye Kisiwa cha Qeshm nchini Iran.
-
Vikosi vya Ulinzi: Vitisho vya US dhidi ya meli za Iran havitaachwa bila ya jibu
Jul 28, 2026 14:12Kamandi Kuu ya operesheni za kijeshi ya Iran imeionya Marekani kwamba vitisho inavyotoa dhidi ya meli za Jamhuri ya Kiislamu za kibiashara na za mafuta havitaachwa bila ya jibu.