-
Pezeshkian: Kuimarisha mshikamano wa nchi za Kiislamu ni jambo la msingi katika kudumisha utulivu
Aug 26, 2026 03:33Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameonya kwamba maadui, wenye tamaa ya utajiri na rasilimali za eneo la Magharibi mwa Asia, wanataka kuibua hitilafu, vita na migogoro ili kunyakua utajiri huo, na njia pekee ya kukabiliana nao ni kudumisha umakini na umoja miongoni mwa mataifa ya Waislamu.
-
China yapinga vitisho vya Marekani na vikwazo haramu dhidi ya nchi zinazofanya biashara na Iran
Aug 26, 2026 03:27China imepinga vitisho vya Marekani vya kuziwekea vikwazo nchi zinazofanya biashara na Iran, ikisema kuwa ushirikiano wa Beijing na Tehran unafanyika kwa mujibu wa sheria za kimataifa na haupaswi kuvurugwa.
-
Taasisi ya Royan ya Iran ni miongoni mwa vituo 10 bora duniani vya tiba ya uzazi
Aug 26, 2026 03:22Kwa mujibu wa takwimu za SCImago; Taasisi ya Royan ya Iran ni miongoni mwa vituo 10 bora duniani katika nyanja ya tiba ya uzazi. Haya yameelezwa na Naibu Mkuu wa taasisi hiyo anayesimamia masuala ya utafiti.
-
Mkuu wa Umoja wa Mataifa: Vita dhidi ya Iran vimefichua mapungufu ya mataifa makubwa
Aug 25, 2026 11:28Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, amesema kwamba uvamizi wa kijeshi wa hivi karibuni wa Marekani na Israel dhidi ya Iran umefichua mapungufu ya udhibiti wa madola makubwa, na kuashiria mabadiliko ya uhakika na yasiyoweza kurekebishwa kuelekea mfumo wa kimataifa wa kambi nyingi.
-
Taasisi ya Brookings: Vikwazo vipya vya Marekani dhidi ya Iran ni vya kimaonyesho tu
Aug 25, 2026 10:12Mjumbe mkuu wa taasisi ya wanafikra ya Brookings amezungumzia mpango wa Marekani wa eti kuzidisha mashinikizo ya kiuchumi dhidi ya Iran na kusema: Kwa mujibu wa matarajio, mpango huu si chochote ila kampeni ya kipropaganda yenye makelele mengi.
-
PGSA: Iran itazuilia na kutwaa meli zinazokiuka sheria za Lango-Bahari la Hormuz
Aug 24, 2026 06:15Mamlaka ya Lango-Bahari la Ghuba ya Uajemi (PGSA), ambayo ni chombo cha udhibiti cha Iran cha Lango-Bahari la Hormuz, imetangaza kwamba meli zinazokiuka itifaki za Iran za njia hiyo ya majini ya kimkakati zitakabiliwa na vikwazo kwenye njia za baadaye, ikiwa ni pamoja na faini, kuzuiliwa, au kutwaliwa.
-
Mufti Mkuu wa Russia asifu juhudi za Iran za kuunganisha Umma wa Kiislamu
Aug 24, 2026 04:38Mkuu wa Baraza la Mufti na Idara ya Masuala ya Kidini ya Waislamu wa Russia amepongeza hatua za Tehran kuimarisha umoja wa Umma wa Kiislamu.
-
Pezeshkian: Ulimwengu umeshangazwa na ustahimilivu wa Iran katika vita vya Marekani na Israel
Aug 23, 2026 14:26Rais Masoud Pezeshkian amesema kuwa tathmini ya adui kwamba Iran itasambaratika kutokana na mashinikizo makubwa haikuwa sahihi na kwamba mshikamano na umoja wa taifa hili vimeishangaza dunia.
-
Mkuu wa Usalama: Iran itaendelea kufunga Hormuz hadi Marekani itimize majukumu yake
Aug 23, 2026 14:24Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran amesema Jamhuri ya Kiislamu itafubaza mashinikizo ya kiuchumi ya Marekani ikiwa ni pamoja na kuzichukulia hatua nchi ambazo zinashiriki katika “vita vya kiuchumi” vya Marekani dhidi ya Iran.
-
Kaimu Waziri wa Ulinzi: Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katu haitasalimu amri kwa kuwekewa mashinikizo
Aug 23, 2026 03:28Kaimu Waziri wa Ulinzi wa Iran amesema, taifa hili limeishinda kimkakati Marekani na utawala wa Kizayuni kwa kutegemea uwezo wake wa ndani, na akasisitiza kwamba: Jamhuri ya Kiislamu haitasalimu amri katu kwa kuwekewa mashinikizo.