-
Tume ya Uchunguzi ya Umoja wa Mataifa: Marekani imetenda uhalifu wa kivita nchini Iran
Sep 18, 2026 03:54Tume ya Kutafuta Ukweli ya Umoja wa Mataifa imetangaza kwamba, baada ya kufanya uchunguzi na kuchambua ushahidi, imefikia hitimisho kwamba mashambulizi ya Marekani dhidi ya Minab na Lamerd yalikuwa ni uhalifu wa kivita.
-
Baghaei ajibu madai ya Saudi Arabia kuhusu kushambuliwa mji mtakatifu wa Makka
Sep 18, 2026 03:52Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kuwa, madai ya kuzuia ndege isiyo na rubani iliyokuwa ikielekea katika mji mtakatifu wa Makka hayawezi kuwa msingi wa kuutuhumu upande wowote.
-
Iran yajibu mapigo, yamtimua mwanadiplomasia wa Sweden
Sep 18, 2026 03:50Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, sanjari na kukanusha madai ya Sweden dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu, imempa mwanadiplomasia wa nchi hiyo aliyeko Tehran muda wa saa 48 kuondoka nchini, ikiwa ni hatua ya kulipiza kisasi kwa uamuzi wa Stockholm wa kukataa kumruhusu mwanadiplomasia wa Iran kuendelea na shughuli zake.
-
Araghchi: Mashauriano ya Beijing yamefanikiwa; Iran yathamini “ushirikiano wa kimkakati” na China
Sep 17, 2026 12:09Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, ameelezea mashauriano yake mjini Beijing kama “yaliyofanikiwa,” akizungumzia maudhui ya safari yake katika mji mkuu huo wa China, ambapo alikutana na mwenzake, Wang Yi.
-
Iran yashika nafasi ya tatu duniani katika kutibu ugumba, yakamilisha mpango wa chanjo
Sep 16, 2026 02:56Mkuu wa Shirika la Madaktari la Iran amesema kuwa, Jamhuri ya Kiislamu imeshika nafasi ya kwanza duniani katika utoaji wa chanjo na nafasi ya tatu duniani katika kutibuu tatizo la ugumba.
-
Meli kubwa ya mafuta yalipuka baada ya kukanyaga mabomu ya majini kwenye njia haramu kusini mwa Hormuz
Sep 15, 2026 04:15Kikosi cha Wanamaji cha Jeshi la Iran la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) kimetangaza kuwa meli kubwa ya kubeba mafuta ghafi (supertanker) iliyojaribu kupita bila idhini katika eneo lililopigwa marufuku kusini mwa Lango Bahari la Hormuz imelipuka baada ya kukanyaga mabomu ya kutega majini, huku chombo hicho chote kikiwa kimeteketea na kufunikwa na miali mikubwa ya moto.
-
Rais wa Iran aihimiza BRICS kulinda kanuni ya kutotumia mabavu
Sep 13, 2026 11:29Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Dkt. Masoud Pezeshkian, ametoa wito kwa kundi la mataifa yanayoinukia kiuchumi la BRICS kuchukua jukumu “lenye ufanisi zaidi” katika kulinda mamlaka ya kitaifa na kusimamia kanuni ya kimataifa ya kutotumia nguvu, hasa katika kipindi hiki cha sasa chenye changamoto nyingi.
-
Pezeshkian ahimiza BRICS kuunda mtandao imara wa kibiashara na kutumia sarafu za kitaifa
Sep 12, 2026 04:34Rais Masoud Pezeshkian amezihimiza nchi wanachama wa jumuiya ya BRICS kujenga mtandao thabiti na wenye uwezo wa kustahimili misukosuko ya kibiashara, sambamba na kupanua matumizi ya sarafu za kitaifa ili kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi na kupunguza uwezekano wa kuathiriwa na mshtuko wa kisiasa.
-
Iran: Mamlaka ya kujitawala ya Yemen lazima yaheshimiwe, mzingiro haramu lazima ukomeshwe
Sep 12, 2026 04:31Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imesisitiza tena msimamo wake thabiti na wa kimisngi kuhusu ulazima wa kuheshimiwa uhuru, mamlaka ya kitaifa ya kujitawala na umoja wa ardhi yote ya Yemen, na kutoa wito wa kukomeshwa mara moja mzingiro haramu na usio wa kibinadamu uliowekwa dhidi ya nchi hiyo.
-
Iran yazindua programu mpya ya kinga-virusi iliyotengenezwa nchini
Sep 08, 2026 04:39Sambamba na maonyesho ya kimataifa ya Iran ya ELECOMP 2026, ambayo ni maonyesho makubwa zaidi ya nchi kwa sekta za elektroniki, teknolojia za kompyuta, na biashara pepe (e-commerce), Iran imezindua programu yake ya pili ya kinga-virusi (antivirus) iliyotengenezwa nchini, ijulikanayo kama Ayyza. Programu hii hutumia akili mnemba (AI) na mbinu za kujifunza kwa mashine (machine learning) kutambua virusi vipya visivyojulikana na vitisho vya mtandaoni ambavyo havijatambulika awali.