-
Mkuu wa Idara ya Mahakama amwambia Trump: Iran ndiyo mmiliki na mtawala wa Lango la Hormuz
Aug 16, 2026 05:56Mkuu wa Idara ya Mahakama ya Iran, Gholam-Hossein Mohseni-Eje’i, amezitaja kauli za hivi karibuni za Rais wa Marekani, Donald Trump, kuhusu umiliki wa Lango Bahari la Hormuz kuwa ni "upuuzi," akisisitiza kuwa Jamhuri ya Kiislamu ndiyo mmiliki na mtawala halisi wa lango hilo.
-
Qalibaf: Nilisitisha mazungumzo baada ya shambulio la Israel dhidi ya Dahiyeh huko Beirut
Aug 16, 2026 03:05Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran (Bunge) amesema kuwa alisitisha mazungumzo kufuatia shambulio la Israel dhidi ya eneo la Dahiyeh mjini Beirut nchini Lebanon, na kusema kuwa Iran itaushambulia utawala huo haraka iwezekanavyo.
-
Iran yaonyesha mabaki ya ndege za kivita za Marekani na Israel ilizozitungua +Video
Aug 15, 2026 03:54Iran imeonyesha sehemu za vifaa vilivyopatikana kutoka ndege za kivita zisizo na rubani (droni) za Marekani na Israel, pamoja na ndege ya kivita ya F-15 ambazo zilitunguliwa kwa mifumo ya ulinzi ya Iran wakati wa vita. Mifumo ya ulinzi iliyotumika kutungua ndege hizo za adui imeundwa hapa nchini.
-
Jerusalem Post: Israel imeshtushwa na kasi ya Iran ya kujiimarisha upya kijeshi
Aug 15, 2026 03:53Gazeti la kizayuni la Jerusalem Post limefichua kuwa, maafisa wa ulinzi wa Israel wameshtushwa na namna Iran ilivyojenga upya na kwa kasi uwezo wake wa kijeshi tangu baada ya mashambulizi makali ya Marekani na utawala huo wa kizayuni wakati wa kipindi cha mwanzoni mwa vita vya kichokozi vilivyoanzishwa na tawala mbili hizo dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu.
-
Mwanadiplomasia wa kizayuni: Baadhi ya Wademocrat wanaipendelea Iran kuliko serikali ya Marekani
Aug 12, 2026 03:36Mwanadiplomasia mmoja mwandamizi wa utawala wa kizayuni wa Israel amesema, ametiwa wasiwasi mkubwa na alichokiita "mabadiliko ya mwelekeo" katika sera ya Marekani, akisisitiza kwamba Tel Aviv inajiandaa kwa zama za kupunguza utegemezi kwa Washington na kujitegemea zaidi, ikiwa ni pamoja na "kuanzisha muungano na nchi zingine."
-
Kwa nini Marekani imeshindwa na Iran
Aug 11, 2026 11:38Hujambo mpenzi msikiilizaji. Je, matukio nyeti katika kanda ya Asia ya Magharibi yanaweza kueleweka vyema zaidi kwa mtazamo wa mwanadiplomasia wa Kijapani? Katika kipindi hiki, tunatupia jicho kitabu kilichopewa jina "Why America Was Defeated by Iran" (Kwa Nini Marekani Imeshindwa na Iran) kilichoandikwa na Mitsugu Saito, balozi wa zamani wa Japan nchini Iran.
-
Araqchi: Mazungumzo na Oman kuhusu Lango-Bahari la Hormuz yako katika hatua za mwisho
Aug 09, 2026 11:09Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema leo kwamba mazungumzo na Oman kuhusu Lango Bahari la Hormuz yako katika hatua za mwisho na kuongeza: "Bila shaka, hii haina maana kwamba Lango la Hormuz litafunguliwa. Ufunguzi wa Lango la Hormuz unategemea masharti mengine."
-
Iran yayaasa mataifa ya Kiislamu: Ni wakati sasa wa sisi kujitegemea, kuwa na udugu wa kweli
Aug 08, 2026 03:24Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imetoa wito wa kuwepo muunganiko na ushirikiano mkubwa wa kikanda, ikitilia mkazo udharura wa mataifa ya eneo kutegemea uwezo wao wa kikanda ili kuondoa uingiliaji wa kigeni.
-
Telegraph: Vita dhidi ya Iran vinaweza vikawa moja ya makosa ya kihistoria
Aug 08, 2026 03:22Gazeti la Telegraph linalochapishwa nchini Uingereza limekiri katika ripoti yake kwamba Marekani na Israel zimeshindwa katika vita, huku Iran ikiwa imeibuka mshindi, na kwamba vita hivi vinaweza kuwa tukio muhimu sana la kupelekea kupungua satua na ushawishi wa Marekani duniani.
-
Mkuu wa Mossad awatimua maafisa wawili wakuu kwa kufeli mpango wa kuipindua serikali ya Iran
Aug 07, 2026 12:29Mkuu wa shirika la ujasusi na ugaidi la utawala wa kizayuni wa Israel Mossad, Roman Gofman, amewafukuza kazi maafisa wawili wakuu wa intelijensia baada ya kushindwa au kutotekelezwa mpango wa kuipindua serikali ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.