-
Spika wa Bunge la Iran aapa kuwa mwaminifu kwa mashahidi baada ya kuwasili Uswisi kwa mazungumzo na US
Jun 21, 2026 04:41Spika wa Bunge la Iran amesisitiza tena kwamba atatetea haki za Wairani waliouawa shahidi wakati wa mashambulizi ya Marekani na Israel dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu baada ya kuwasili Uswisi kufuatilia mkataba wa Hati ya Maelewano uliosainiwa na viongozi wa nchi mbili kwa lengo la kukomesha vita.
-
Picha ya mazishi ya wanafunzi wa Shule ya Msingi ya Minab yashinda tuzo ya picha bora zaidi ya mwaka
Jun 21, 2026 02:58Picha iliyochukuliwa kutokea angani inayoonyesha mazishi ya wanafunzi 168 waliouawa shahidi wakati wa shambulio la makombora ya Marekani dhidi ya Shule ya Msingi ya Shajareh Tayyebeh huko Minab, kusini mwa Iran, imeshinda tuzo ya juu katika Kategoria ya Upigaji Picha za Habari ya tuzo za Golden Shot Photography Awards 2026.
-
Qalibaf: Tozo ya kupita Mango Bahari la Hormuz baada ya siku 60 imejumuishwa katika Hati ya Makubalino (MoU)
Jun 19, 2026 03:40Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran (Bunge), Mohammad Baqer Qalibaf, ambaye anaongoza timu ya mazungumzo na Marekani, ameeleza kuwa malipo ya kuvuka katika Lango-Bahari la Hormuz yamejumuishwa kwenye Hati ya Makubaliano baina ya pande hizo mbili na kwamba kupita katika lango hilo katika kipindi hiki cha siku 60 cha mazungumzo kutakuwa bure.
-
Pezeshkian: Hasira ya Israel dhidi ya MoU na Marekani ni 'ishara dhahiri' ya ushindi wa Iran
Jun 16, 2026 03:23Rais Masoud Pezeshkian wa Iran amesema hasira ya Israel kuhusu hati ya maelewano (MoU) ya makubaliano kati ya Iran na Marekani inaashiria wazi mafanikio na ushindi wa taifa la Iran.
-
Ayatullah Amoli Larijani: Istiqama ya taifa imeshinda 'kiburi kibaya cha US-Israel
Jun 16, 2026 02:59Mkuu wa Halmashauri ya Kuainisha Maslahi ya Mfumo wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesifu istiqama na ushujaa wa taifa kubwa la Iran mbele ya "kiburi kibaya" cha Marekani na utawala wa Israel.
-
Waziri Mkuu: Pakistani itakuwa mwenyeji wa hafla ya "kihistoria" ya kusaini makubaliano ya Iran na Marekani mjini Geneva, Juni 19
Jun 16, 2026 02:57Waziri Mkuu wa Pakistani, Shehbaz Sharif amesema kuwa hafla ya kutia saini Mkataba wa Maelewano kati ya Iran na Marekani (MOU) itaandaliwa na nchi yake mjini Geneva, Juni 19 mwaka huu.
-
Washington Post: Trump anasherehekea kurudi katika hali ya kabla ya vita na Iran
Jun 15, 2026 10:09Gazeti la Washington Post, katika ripoti yake kuhusu hati ya makubaliano kati ya Iran na Marekani, limekejeli hatua ya Rais Donald Trump wa Marekani ya kusherehekea kurejea Washington kwenye hali ya kabla ya Februari 28, hatua ambayo baadhi ya wataalamu wanaamini ni kurudi nyuma kwa maana halisi ya neno hilo mkabala wa Iran.
-
Araqchi: Jukumu la diplomasia ni kuimarisha mafanikio ya uwanja wa vita
Jun 13, 2026 03:11Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araqchi, ameelezea muundo wa makubaliano tarajiwa kati ya Iran na Marekani na kusisitiza kwamba diplomasia inakusudia kuimarisha mafanikio ya Jamhuri ya Kiislamu katika uwanja wa vita.
-
Kamanda mkuu wa Iran aonya Marekani kuhusu 'mzunguko usio na maana' wa uongo na migongano
Jun 13, 2026 03:06Kamanda wa Makao Makuu ya Majeshi ya Iran, Khatamul-Anbiya (SAW) ameionya Marekani kuhusu "mzunguko wa uongo, tasa na wenye migongano" katika mienendo yake, baada ya Washington kutishia kwanza kwamba itashambulia miundombinu ya nishati ya Iran na kisha kudai mazungumzo yameidhinishwa.
-
Baqaei: Mashambulizi ya Marekani dhidi ya meli za India ni uharamia wa serikali
Jun 13, 2026 02:41Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran Esmaeil Baqaei amelaani mashambulizi ya kikatili ya Marekani dhidi ya meli za kibiashara za India, na kusisitiza kuwa mashambulizi hayo ya Marekani katika Bahari ya Oman ni uharamia wa serikali.