-
Iran yalaani vikali shambulio la kigaidi dhidi ya khatibu wa Haram ya Bibi Zainab (AS)
May 03, 2026 10:42Iran imelaani vikali shambulio la kigaidi lililotokea katika eneo la Sayyida Zainab mjini Damascus, ambalo limepelekea kuuawa shahidi Sayyid Farhan Hassan Al‑Mansour, mmoja wa wanazuoni wa Kiislamu na khatibu wa Ijumaa katika Haram ya Bibi Zainab (AS).
-
Iran: Majigambo ya Trump kuhusu uharamia ni ‘kukiri wazi’ jinai
May 03, 2026 10:26Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imejibu kauli za Rais wa Marekani Donald Trump, ambaye amejigamba kuwa Jeshi la Wanamaji la Marekani limetekeleza operesheni “kama maharamia” katika mzingiro wa baharini usio halali dhidi ya meli na bandari za Iran.
-
Kiongozi Mudhamu: Taifa la Iran litamshinda adui katika nyuga za kiuchumi na kiutamaduni baada ya ushindi katika vita vya kijeshi
May 02, 2026 09:20Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu ameapa kuwa taifa la Iran litamshinda pia adui katika nyanja za kiutamaduni na kiuchumi baada ya kupata ushindi katika medani ya vita vya kijeshi.
-
Namna Marekani Ilivyokosa Kuwa na Mkakati Unaoeleweka Katika Kuamiliana na Iran
May 02, 2026 17:20Naibu waziri wa zamani wa mambo ya nje wa Marekani, Wendy Sherman, amekosoa namna serikali ya Donald Trump inavyosimamia suala la vita dhidi ya Iran na kusisitiza kuwa, Washington haina mkakati unaoeleweka, wala mwenendo wa uchukuaji maamuzi ulioratibika, na kwamba mgogoro wa sasa hautatatuka pasi na kuirejea tena diplomasia.
-
Manowari kubwa na ya kisasa zaidi ya Marekani yaondoka kwa fedheha katika vita dhidi ya Iran
May 02, 2026 11:31USS Gerald R. Ford, meli kubwa zaidi ya kivita na ya gharama ya juu kuwahi kuundwa na Marekani, imelazimika kujiondoa kutoka ukanda wa Asia Magharibi baada ya siku 309 za operesheni endelevu baharini, ikiwa katika jukumu la kuunga mkono vita dhidi ya Iran.
-
Mufti Mkuu wa Russia: Umma wa Kiislamu unapaswa kusimama pamoja na Iran dhidi ya njama za shetani
May 02, 2026 07:35Mufti Mkuu na Mkuu wa Idara ya Masuala ya Kidini ya Waislamu wa Russia ameeleza kuwa, Umma wa Kiislamu unapaswa kusimama pamoja na Iran dhidi ya njama za Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel na akasema: "Iwapo Waislamu watakuwa na umoja na mshikamano, kambi ya shetani haiwezi kamwe kurudia uchokozi dhidi ya Gaza, Syria, Iran na Lebanon."
-
Mbunge wa Kongresi: Ni mwehu anayedai Marekani imeshinda vita dhidi ya Iran
May 02, 2026 07:25Mwakilishi wa cha cha Democratic wa California katika Kongresi ya Marekani, Sara Jacobs, amemkosoa vikali Waziri wa Vita wa nchi hiyo, Pete Hegseth kwa kutangaza ushindi dhidi ya Iran, akitaja madai hayo kuwa ni udanganyifu.
-
Mipaka yetu ni mirefu kuliko kuta mbili kote Marekani: Spika Qalibaf akejeli mzingiro wa Marekani
May 02, 2026 07:23Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Baqer Qalibaf amekejeli mzingiro wa jeshi la majini la Marekani dhidi ya Iran, akieleza kuwa mipaka mirefu ya nchi hiyo inabatilisha jaribio lolote la kuizingira Jamhuri ya Kiislamu.
-
IRGC: Manowari za Marekani zitateketea ikiwa Iran itashambuliwa tena
May 01, 2026 08:13Kamanda wa Kikosi cha Anga cha Jeshi la Iran la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC), Brigedia Jenerali Seyyed Majid Mousavi, amesema Iran itajibu uchokozi wowote wa adui kwa mashambulizi ya muda mrefu na yenye kuumiza, akibainisha kuwa meli za kivita za Marekani zitapata hatima sawa na vituo vya kijeshi vya Marekani katika eneo la Asia Magharibi.
-
Rais wa Iran: Mzingiro wa kijeshi baharini ni tishio kwa amani ya dunia
May 01, 2026 08:04Rais wa Iran: Mzingiro wa kijeshi baharini ni tishio kwa amani ya dunia