-
Nujaba kwa maadui wa Iran: Vita vinaweza kufika milangoni kwenu
Jan 29, 2026 06:27Katibu Mkuu wa kundi la kupambana na ugaidi la Harakat al-Nujaba la Iraq amewaonya vikali maadui wa Iran kuhusu matokeo mabaya ya uchokozi wowote mpya ambao wanaweza kufanya dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu.
-
Araghchi: Mazungumzo hayawezi kufanikiwa chini ya vitisho
Jan 29, 2026 03:49Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Sayyid Abbas Araghchi ameonya kwamba, kutwisha diplomasia kupitia vitisho vya kijeshi hakuwezi kuwa na ufanisi au tija, akisema kwamba hakuna uamuzi wowote ambao umefanywa na Tehran kufikia juu ya kufanya mazungumzo na Marekani.
-
Iran: Maadui wajiandae kwa 'jibu la uharibifu' wakituchokoza
Jan 29, 2026 03:48Kamanda mwandamizi wa Jeshi la Iran ameonya kwamba, hatua yoyote ghalati dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu itawasababishia maadui uharibifu mkubwa, akisisitiza kwamba vitisho dhidi ya Tehran kupitia maonyesho ya kijeshi havilishughulisha taifa hili.
-
Mtaalamu wa kijeshi: Utitiri wa droni za Iran ni 'tishio halisi' kwa vyombo vya majini vya Marekani
Jan 28, 2026 10:32Mtaalamu wa kijeshi wa ndege zisizo na rubani ameonya kuwa, utitiri wa ndege zisizo na rubani za Iran ni "tishio halisi" kwa vyombo vya jeshi la wanamaji la Marekani vyenye thamani kubwa, wakati huu ambapo Washington inaripotiwa kuwa inaendelea kujizatiti kijeshi katika eneo la Asia Magharibi.
-
Iran ilivyofanikiwa kuvunja mtandao wa mawasiliano ya kigaidi kwa kukata intaneti
Jan 28, 2026 08:00Iran ilifanikiwa kuvuruga na hatimaye kuvunja mtandao wa mawasiliano wa makundi ya kigaidi na washirika wao wa nje kwa hatua ya kukata intaneti wakati wa machafuko ya Januari 2026.
-
Waziri wa Usalama: Umoja wa kitaifa utazuia vitisho kwa umoja wa kitaifa wa Iran
Jan 28, 2026 07:58Waziri wa Usalama wa Iran amesema kuwa taifa la Iran halitaruhusu umoja wa kitaifa wa nchi hii udhoofishwe akisisitiza kuwa umoja wa taifa la Iran ndiyo nguzo kuu ya kukabiliana na vitisho vya nje.
-
Katibu Mkuu wa Hizbullah asema hawatakuwa watazamaji katika uchokozi wowote dhidi ya Iran
Jan 27, 2026 06:39Katibu Mkuu wa harakati ya Hizbullah ya Lebanon amesisitiza kwa kusema: "Imam Khamenei, Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran ni Faqihi wetu Mtawala na sisi hatutabaki kuwa watazamaji mbele ya uchokozi wowote utakaofanywa dhidi ya Iran".
-
Mwanamke Muisraeli ashtuka kujiona kwenye orodha ya 'waliofariki' kwenye machafuko ya Iran
Jan 27, 2026 06:38Kijana wa kike wa kiisraeli aitwaye Noya Zion ameshtuka baada ya kuona picha yake inaonyeshwa kwenye televisheni ya taifa ya Israel kama mmoja wa watu waliouawa katika maandamano nchini Iran, mkasa ambao umezidi kudhihirisha jinsi utawala huo wa kizayuni unavyosambaza habari feki na za uwongo kuhusu machafuko ya hivi karibuni nchini Iran na namna serikali ya Jamhuri ya Kiislamu ilivyokabiliana nayo.
-
Ugaidi wa ndani nchini Marekani na mtazamo wa undumakuwili wa Washington
Jan 27, 2026 02:32Waziri wa Usalama wa Ndani wa Marekani ametaja aina yoyote ya uchochezi au utekelezaji wa vurugu dhidi ya serikali kuwa ni mfano wa ‘ugaidi wa ndani’.
-
Je, vyombo vya habari vinavyohasimiana na Iran vinakiuka sheria za kimataifa katika upotoshaji?
Jan 26, 2026 12:56Kadiri wimbi la fitina, vurugu na machafuko yanayohusishwa na ushawishi wa Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel nchini Iran lilivyozidi kupamba moto, nafasi ya vyombo vya habari hasimu katika kuchochea vitendo vya ugaidi na kukiuka wazi misingi ya sheria za kimataifa imejitokeza kwa uwazi tena.