-
Ulinzi mkali Iraq sambamba na kuanza maandamano ya milioni ya watu ya kuifukuza Marekani
Jan 24, 2020 04:31Duru za usalama za Iraq zimetangaza habari ya kuwekwa ulinzi mkali katika kona zote za nchi hiyo ya Kiarabu hasahasa Baghdad kufuatia kuanza maandamano ya milioni ya watu ya kushinikiza kufukuzwa wanajeshi wa Marekani nchini humo.
-
Mbunge wa Iraq: Maandamano ya Ijumaa ni kura ya maoni ya kuondoa askari wa Marekani
Jan 23, 2020 08:20Mbunge wa Muungano wa Al Fath katika Bunge la Iraq amesema maandamano ya kesho Ijumaa nchini Iraq ni sawa na kura ya maoni ya wananchi wanaopinga kuwepo wanajeshi wa Marekani katika nchi hiyo.
-
Rais wa Iraq: Kutaka majeshi ya kigeni yaondoke kumetokana na kuvunjwa heshima ya mamlaka ya kujitawala
Jan 23, 2020 04:11Rais Barham Salih wa Iraq amesema: Miito ya kutaka majeshi ya kigeni (Marekani) yaondoke Iraq ni jibu kwa kitendo cha kuvunjia heshima haki ya kujitawala ya nchi hiyo.
-
Shambulizi la maroketi lajiri karibu na ubalozi wa Marekani nchini Iraq
Jan 21, 2020 04:05Eneo lenye ulinzi mkali la Green Zone karibu na ubalozi wa Marekani katika mji mkuu wa Iraq, Baghdad limeshambuliwa kwa maroketi usiku wa kuamkia leo.
-
Mohammed Tawfiq Allawi, ateuliwa kuwa waziri mkuu mpya wa Iraq
Jan 21, 2020 00:20Duru za habari nchini Iraq zimetangaza kuwa, aliyekuwa waziri wa Mawasiliano, Mohammed Tawfiq Allawi ameteuliwa kuwa waziri mkuu mpya wa nchi hiyo.
-
Iraq: Hatua ya Marekani ya kujiondoa JCPOA, ndio chanzo cha mzozo Asia Magharibi
Jan 19, 2020 01:04Wizara ya Mambo ya Nje ya Iraq imesema kuwa hatua ya Marekani ya kujiondoa kwenye mapatano ya nyuklia mashuhuri kama JCPOA ndio sababu kuu ya ongezeko la mzozo wa hivi karibuni katika eneo la Asia Magharibi.
-
Mufti 'tipwatipwa' wa DAESH mwenye uzito wa kilo 245 atiwa nguvuni mjini Mosul, Iraq
Jan 18, 2020 10:37Vikosi vya usalama vya Iraq vimemtia nguvuni Abu Abdul Bari, mufti wa kundi la kigaidi na ukufurishaji la DAESH (ISIS) katika mji wa Mosul, kaskazini mwa nchi hiyo. Abu Abdul Bari ni maarufu kwa utoaji fatua za kuwafanya wanawake watumwa, za ubakaji, utesaji na uangamizaji wa kimbari.
-
CNN: Marekani inakaribia kuondoka kimadhila katika ardhi ya Iraq
Jan 18, 2020 11:23Kanali ya televisheni ya CNN imeeleza kuhusu kuongezeka mashinikizo ya kulitaka jeshi la Marekani liondoke Iraq na kubainisha kuwa: Huo ni mwisho wa kimadhila wa kazi maalumu na ya muda mrefu iliyofanywa na jeshi la Marekani; kazi ambayo imeteketeza mabilioni ya dola.
-
Kamati ya usalama Iraq: Marekani haijawa na nafasi yoyote ya kuimarisha usalama nchini
Jan 16, 2020 23:22Mjumbe mwandamizi wa kamati ya usalama na ulinzi ya bunge la Iraq amesema kuwa askari vamizi wa Marekani hawajawahi kuwa na nafasi yoyote ya kuimarisha usalama na amani nchini humo.
-
Sadr aitisha maandamano ya "watu milioni moja" Iraq ya kulaani kuwepo kijeshi kwa Marekani
Jan 15, 2020 04:35Kiongozi wa Harakati ya Sadr nchini Iraq ametoa mwito kwa wananchi kufanya maandamano ya watu wasiopungua milioni moja ya kulaani kuwepo kijeshi Marekani nchini humo.