-
Iran yailaani Israel kwa kuendelea kuua wanawake na watoto Gaza
Oct 19, 2025 03:10Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje wa Iran, Esmaeil Baghaei amelaani ukiukaji wa mara kwa mara wa makubaliano ya usitishaji vita katika Ukanda wa Gaza unaofanywa na utawala ghasibu wa Israel, likiwemo shambulio la hivi karibuni dhidi ya gari lililokuwa limebeba familia ya Kipalestina wakati ikirejea kwenye makazi yao.
-
ICC yatupilia mbali rufaa ya Israel dhidi ya hati za kutiwa nguvuni Netanyahu na Gallant
Oct 18, 2025 23:11Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) imekataa ombi la utawala wa kizayuni wa Israel la kukata rufaa dhidi ya hati za kukamatwa waziri mkuu wake Benjamin Netanyahu na aliyekuwa waziri wa vita wa utawala huo ghasibu Yoav Gallant kuhusiana na mauaji ya kimbari yaliyofanywa na jeshi la kizayuni katika Ukanda wa Ghaza.
-
Taa ya kijani ya Trump kwa Israel; Je vita vya Gaza vitaanza tena?
Oct 17, 2025 22:59Rais Donald Trump wa Marekani ameionyesha Israel taa ya kijani ili ianzishe tena vita katika Ukanda wa Gaza.
-
Mkuu wa majeshi ya Yemen auawa katika mashambulizi ya Israel
Oct 17, 2025 03:26Mkuu wa Majeshi ya Yemen, Meja Jenerali Mohammad Abd al-Karim al-Ghamari ameripotiwa kuuawa shahidi katika mashambulizi ya anga ya Israel, pamoja wapamba wake kadhaa na mtoto wake wa kiume aliyekuwa na umri wa miaka 13, Hussein al-Ghamari.
-
Israel yaanza ukhabithi wake, yapunguza misaada ya kuingizwa Ghaza hadi nusu, yazuia fueli kikamilifu
Oct 15, 2025 02:33Utawala wa kizayuni wa Israel umeueleza Umoja wa Mataifa kwamba, kuanzia leo Jumatano utaruhusu malori 300 tu ya misaada kwa siku, ikiwa ni nusu ya idadi iliyokubaliwa kuingia katika Ukanda wa Ghaza na kwamba hakuna mafuta yoyote au gesi itakayoruhusiwa kuingizwa katika eneo hilo isipokuwa kwa mahitaji maalumu yanayohusiana na miundombinu ya kibinadamu.
-
Afrika Kusini: Kesi ya mauaji ya kimbari tuliyofungua ICJ dhidi ya Israel itaendelea licha ya vita kusitishwa
Oct 15, 2025 02:32Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa amesema usitishaji vita wa Ghaza hautaathiri kesi ya mauaji ya kimbari iliyofunguliwa na nchi yake dhidi ya utawala wa kizayuni wa Israel katika Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ).
-
Iran: Dunia iwe macho, isikubali Israel ikiuke usitishaji vita Gaza
Oct 13, 2025 08:47Iran imesisitiza uungaji mkono wake usioyumba kwa juhudi zozote zinazolenga kukomesha mauaji na mauaji ya halaiki ya Israel huko Gaza, ikionya kuhusu historia ya utawala unaoikalia kwa mabavu Quds ya kukanyaga mikataba na makubaliano.
-
Hamas yaonya; Israel inaendelea kuchuja orodha ya mateka
Oct 13, 2025 06:12Mjumbe wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina Hamas kuushutumu utawala ghasibu wa Israel kwa 'kutia mkono' orodha ya mateka wa Kipalestina, na kukwepa kutekelezwa masharti na vipengee vya makubaliano ya usitishaji vita Gaza, licha ya ahadi zake kwa wapatanishi wa kimataifa.
-
Je, ni upi msimamo wa Umoja wa Ulaya kuhusu mpango wa Trump na usitishaji vita huko Gaza?
Oct 12, 2025 22:53Umoja wa Ulaya umeeleza kuwa usitishaji vita huko Gaza ni fursa ya kweli ya kuhitimisha vita vya uharibifu.
-
Iran yalaani vikali shambulio la Israel kusini mwa Lebanon lililoua watu na kusababisha hasara kubwa
Oct 12, 2025 02:55Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amelaani vikali mashambulio ya kijeshi yanayofanywa kila mara na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Lebanon na kuendelea kukiuka mamlaka ya utawala na umoja wa ardhi ya nchi hiyo hususan shambulio la jana Jumamosi la ndege zisizo na rubani lililolenga kijiji cha Al-Musayleh.