-
Guterres: Mapatano ya JCPOA ni muhimu mno kwa usalama wa Ghuba ya Uajemi
Oct 21, 2020 04:00Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres amesema katika mkutano uliofanyika kwa njia ya Intaneti kwamba kulindwa na kuhifadhiwa mapatano ya kimataifa ya nyuklia yanayojulikana kwa jina maarufu la JCPOA ni muhimu mno kwa usalama wa eneo la Ghuba ya Uajemi.
-
Iran: Leo ni siku muhimu kwa walimwengu baada ya kufikia tamati vikwazo vya silaha dhidi ya Tehran
Oct 18, 2020 04:50Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imetoa taarifa rasmi kwa mnasaba wa siku ya leo ya tarehe 18 Oktoba ya kufikia tamati muda wa vikwazo vya silaha dhidi ya taifa hili na kueleza kwamba, hii ni siku muhimu kwa jamii ya kimataifa.
-
Mitazamo ya Trump na Biden kuhusu Iran; madai ya ushindi mkabala na kukiri kwamba Marekani imetengwa
Oct 17, 2020 22:58Katika kipindi hiki cha kukaribia uchaguzi wa Rais nchini Marekani tarehe 3 Novemba mwaka huu Rais Donald Trump wa nchi hiyo ambaye ni mgombea wa chama cha Republican na Joe Biden wa chama cha Democratic wamekuwa wakizungumzia kadhia ya Iran na mapatano ya nyuklia ya JCPOA katika kampeni zao za uchaguzi lakini kwa mitazamo tofauti na inayokinzana.
-
Ndoto za alinacha za Trump za kufanya mazungumzo na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran
Oct 13, 2020 22:53Rais Donald Trump wa Marekani akiwa na lengo la kujijengea nafasi nzuri wakati huu wa kukaribia uchaguzi nchini humo, anahitajia kutoa madai ya kufanikiwa katika sera za kigeni za nchi hiyo hasa kuhusiana na Iran.
-
Borell akiri udharura wa Iran kunufaika na mkataba wa JCPOA
Oct 09, 2020 03:43Licha ya kuwa Umoja wa Ulaya na Troika ya Ulaya ambayo inajumuisha nchi za Ujerumani, Ufaransa na Uingereza zilikuwa na mchango mkubwa katika kufanikisha mapatano ya nyuklia ya Iran yanayojulikana kama JCPOA, lakini baada ya Marekani kujitoa katika mapatano hayo, pande hizo zimekuwa na utendaji mbaya usioweza kutetewa kutokana na kuwa zimeshindwa kuyalinda na pia kutotekeleza ahadi zao, na hasa kuhusu kutofanikisha mfumo wa mabadilishano ya kifedha na kibiashara unaojulikana kama Instex.
-
Kurejea kwenye mapatano ya nyuklia ya JCPOA, hatua ya kwanza inayopasa kuchukuliwa na Marekani
Sep 27, 2020 00:38Rais Donald Trump wa Marekani amekuwa akiyataja mapatano ya nyuklia ya JCPOA kuwa ndiyo mapatano mabaya zaidi kwa nchi yake na hatimaye mwezi Mei mwaka 2018 aliiondoa nchi hiyo kwenye mapatano hayo na kuiwekea Jamhuri ya Kiislamu ya Iran vikwazo vikali. Hivi sasa Joe Biden mgombea wa kiti cha urais wa chama cha Democratic huko Marekani amesema iwapo atashinda uchaguzi huo wa mwezi Novemba mwaka huu atairejesha Marekani katika mapatano hayo ya JCPOA.
-
Tarehe 20 Septemba; Marekani kupata pigo jingine?
Sep 18, 2020 23:57Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, hakuna kitu kipya kitakachotokea kesho tarehe 20 Septemba na kwamba, inamtosha kwa Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Marekani kulisoma azimio nambari 2231 la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
-
Ombi la Guterres kwa nchi mbalimbali kufanya juhudi za pamoja ili kuyalinda mapatano ya JCPOA
Sep 17, 2020 04:20Baada ya Marekani kujitoa kwa upande mmoja katika mapatano ya nyuklia ya JCPOA mwezi Mei mwaka 2018 hivi sasa nchi wanachama zilizosalia katika kundi la 4+1 zinasisitiza kuendelea kuwepo mapatano hayo kinyume na mtazamo wa Washington ambayo ilitaka kuchukuliwa hatua sawa na hiyo kutoka kwa wanachama wengine wa kundi la 5+1. Hvi sasa Marekani inafanya njama zake zote kujaribu kuyasambaratisha mapatano hayo ya JCPOA.
-
Iran: Makubaliano yoyote hayatodumu mpaka yatekeleze sawa haki na majukumu
Sep 16, 2020 21:52Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika masuala ya haki za kimataifa amesema kuwa, makubaliano yoyote yale ya kimataifa hayawezi kudumu bila ya kuweko mlingano sawa katika utekelezaji wa haki na majukumu, na kwamba mapatano ya nyuklia ya JCPOA nayo hayawezi kutoka kwenye msingi huo.
-
Kukiri Biden kufeli siasa za Trump mbele ya Iran
Sep 15, 2020 02:51Huku wakati wa kufanyika uchaguzi wa Rais wa mwezi Novemba 2020 ukizidi kukabiria nchini Marekani, wagombea wawili wa uchaguzi huo, yaani rais wa hivi sasa Donald Trump na mpinzani wake Joe Biden wa chama cha Democrats kila mmoja amekuwa akitangaza misimamo yake kuhusu masuala mbalimbali ikiwemo misimamo yao kuhusu Iran na mapatano ya nyuklia ya JCPOA.