-
Hatua ya pili; kiwango cha urutubishaji urani ni cha kudhamini mahitaji ya Iran na sio ya JCPOA
Jul 08, 2019 07:14Baada ya kumalizika muhula wa kwanza wa siku 60 zilizotolewa na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kwa anchi za Ulaya ili zitekeleze ahadi zao za mapatano ya kimataifa ya nyuklia mashuhuri kama JCPOA, Tehran imetangaza kuanza hatua ya pili ya kupunguza ahadi zake kwa mujibu wa vipengee vya 26 na 36 vya mapatano hayo, kwa kuongeza kiwango cha urutubishaji wake wa madini ya urani.
-
Iran yaingia hatua ya pili ya kupunguza uwajibikaji wake kwa mujibu wa makubaliano ya nyuklia ya JCPOA
Jul 07, 2019 07:43Jamhuri ya Kiislamu ya Iran leo imetangaza kuanza kutekeleza hatua ya pili ya kupunguza uwajibikaji wake kwa mujibu wa makubaliano ya nyuklia ya JCPOA.
-
Ukosoaji wa Russia kuhusu mkinzano uliopo kati ya shaari na hatua za Ulaya katika kulinda makubaliano ya JCPOA
Jul 06, 2019 07:19Umoja wa Ulaya na Troika ya Ulaya inayoundwa na Ujerumani, Ufaransa na Uingereza ambazo ni nchi wanachama wa Ulaya katika kundi la 4+1 mara kwa mara zimekuwa zikisisitiza juu ya ulazima wa kulindwa makubaliano ya nyuklia ya JCPOA; na hata kudai kuwa zimeanzisha mfumo maalumu kwa lengo hilo. Pamoja na hayo, shaari na nara zinaotolewa na pande hizo za Ulaya zinakinzana na matendo yao.
-
Sisitizo la Russia la nafasi hasi ya vikwazo vya Marekani katika hatua za hivi karibuni za Iran
Jul 05, 2019 23:36Russia ambayo ni moja ya wanachama muhimu wa kundi la 4+1 la mapatano ya nyuklia ya JCPOA imesisitizia haja ya kuendelezwa mapatano hayo kwa hali yoyote ile.
-
Zarif: Hatua ya Iran kupunguza ahadi ilizojifunga nazo itazuia JCPOA kuvunjika kikamilifu
Jul 05, 2019 02:54Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameashiria ukiukaji ahadi wa madola ya Ulaya katika kutekeleza makubaliano ya nyuklia ya Iran na kueleza bayana kwamba, hatua ya kupunguza ahadi ilizojifunga nazo Iran kwa mujibu wa mapatano hayo inachukuliwa kwa shabaha ya kuzuia JCPOA isivunjike kikamilifu.
-
Uhispania: Iran haijavunja hata mara moja mapatano ya JCPOA
Jul 03, 2019 22:12Waziri wa Mambo ya Nje wa Uhispania ambaye anatarajiwa kuchukua nafasi ya Federica Mogherini, Mkuu wa Sera za Kigeni wa Umoja wa Ulaya amesisitiza kuwa, uamuzi wa hivi karibuni wa Iran haujavunja vipengee vya mapatano ya nyuklia ya JCPOA na kimsingi hilo ni suala la kiufundi.
-
Rais Rouhani: Kama Marekani inaogopa moto basi haipaswi kuwasha muale
Jul 03, 2019 08:31Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa makubaliano ya nyuklia ya JCPOA yana manufaa kwa mataifa yote, eneo la Mashariki ya Kati na dunia nzima na kuongeza kuwa, Kama Marekani inaogopa moto haipaswi kuwasha muale na itekeleze maazimio ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
-
Hatua mpya ya Iran katika kujibu ukiukaji ahadi wa madola ya Ulaya; Iran yavuka kiwango cha kilo 300 za urani iliyorutubishwa
Jul 02, 2019 22:04Kwa mujibu wa kifungu nambari 36 cha makubaliano ya nyuklia ya Mpango Kamili wa Pamoja wa Utekelezaji JCPOA, Iran imevuka kiwango cha kilo 300 za urani iliyorutubishwa.
-
Balozi wa Iran UN: INSTEX bila mtaji ni sawa na gari zuri bila mafuta
Jun 30, 2019 03:09Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa amesema mfumo maalumu wa mabadilishano ya fedha kati ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Umoja wa Ulaya (INSTEX) ni sawa na gari zuri ambalo halina mafuta.
-
Taarifa ya mwisho ya kikao cha kamisheni ya JCPOA yatolewa Vienna
Jun 29, 2019 12:24Kamisheni ya makubaliano ya nyuklia ya JCPOA imetoa taarifa mwishoni mwa kikao chake huko Vienna na kutangaza kuwa wanachama wa JCPOA wanafanya jitihada za kufungua mfumo maalumu wa mabadilishano ya fedha kati ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Umoja wa Ulaya, Instex mbele ya wadau wa masuala ya uchumi wa nchi nyingine.