-
Foreign Policy yafichua taasisi bandia inayodai kuwa na uhusiano na UN, inahusishwa na uhalifu wa kimataifa
Mar 25, 2021 02:34Uchunguzi uliofanywa na gazeti la Foreign Policy umefichua habari za taasisi moja inayodai kuwa na uhusiano na Umoja wa Mataifa na kutetea haki za binadamu ambayo viongozi wake wanatuhumiwa kuhusika na uhalifu na jinai nyingi zikiwemo za kutakatisha fedha chafu na kutorosha mabilioni ya dola za Marekani zilizokuwa zimeporwa kutoroshwa nje ya nchi na kiongozi wa zamani wa Libya, Muammar Gaddafi kabla ya kuuawa kwake.
-
Waziri wa Polisi Afrika Kusini: Uhalifu “umeenda likizo” katika kipindi cha maambukizi ya corona
Aug 15, 2020 10:39Takwimu zinaonesha kuwa kesi za visa vya uhalifu, katika nchi iliyoathiriwa sana na kiwango cha juu cha jinai na uhalifu ya Afrika Kusini, zimepungua sana katika kipindi cha miezi mitatu ya kwanza ya utekelezaji wa sheria kali za kupambana na maambukizi ya virusi vya corona nchini humo.
-
Uturuki: Imarati imefanya jinai za kivita na mauaji ya kimbari huko Yemen
Jul 03, 2020 09:46Mwakilishi wa kudumu Uturuki katika Umoja wa Mataifa amesema kuwa serikali ya Umoja wa Falme za Kiarabu (Imarati) imefanya jinai za kivita na mauaji ya kimbari katika vita vya Yemen.
-
Mahakama ya Kimataifa ya Jinai yamkamata kiongozi wa Janjaweed
Jun 10, 2020 05:24Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) imetangaza kuwa, kiongozi wa wanamgambo wa Janjaweed Ali Kosheib ambaye alikuwa mtu wa karibu kwa rais wa zamani wa Sudan, Omar al Bashir amejisalimisha kwa mahakama hiyo na kwamba anakabiliwa na tuhuma za kutenda jinai za kivita katika jimbo la Darfur huko magharibi mwa Sudan tangu mwaka 2003.
-
Maafisa wa Imarati wafunguliwa mashtaka ya kufanya uhalifu wa kivita huko Yemen
Feb 13, 2020 11:28Shirika moja la mawakili la Uingereza limefungua mashtaka dhidi ya maafisa wa serikali ya Imarati kwa tuhuma za kutenda jinai za kivita nchini Yemen.
-
Serikali ya Sudan na wapinzani wa Darfur wakubaliana kuwakabidhi watenda jinai kwa mahakama ya ICC
Feb 12, 2020 02:58Serikali ya Sudan na viongozi wa makundi ya upinzani katika eneo la Darfur wamefikia makubaliano ya kuwakabidhi watenda jinai za kivita katika eneo hilo lililoko magharibi mwa Sudan kwa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) akiwemo rais wa zamani wa nchi hiyo, Omar al Bashir.
-
Serikali ya Sudan yatwaa mali za chama cha rais wa zamani wa nchi hiyo, al Bashir
Jan 09, 2020 08:02Serikali ya Sudan imetwaa mali za chama kilichovunjwa cha rais wa zamani wa nchi hiyo, Omar al Bashir kilichovunjwa na kupigwa marufuku nchini humo.
-
Ripoti: Wasudani hawaridhishwi na hukumu iliyotolewa dhidi ya Omar al Bashir
Dec 15, 2019 13:27Vyombo vya habari vimeripoti kuwa, wananchi wa Sudan hawakuridhishwa na hukumu ya kifungo cha miaka miwili katika kituo cha marekebisho ya kitabia iliyotolewa dhidi ya kiongozi aliyeondolewa madarakani wa nchi hiyo, Omar al Bashir, baada ya kupatikana na hatia ya ubadhirifu wa fedha za umma na ufisadi.
-
Suu Kyi afunguliwa mashtaka kwa mara ya kwanza kwa jinai dhidi ya Wislamu wa Myanmar
Nov 15, 2019 01:24Makundi ya kutetea haki za binadamu huko Amerika ya Latini yamewasilisha kesi dhidi ya Aung San Suu Kyi Mshauri wa ngazi ya juu wa serikali ya Myanmar na maafisa wa ngazi za juu wa jeshi la nchi hiyo kwa tuhuma za kuhusika na jinai na uhalifu uliofadhiliwa na serikali ya nchi hiyo dhidi ya Waislamu wa kabila la waliochache la Rohingya.
-
Ntaganda ahukumiwa kifungo cha miaka 30 jela kwa kutenda jinai za kivita Congo DR
Nov 07, 2019 13:32Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) imemhukumu kifungo cha miaka 30 jela mbabe wa zamani wa vita katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Bosco Ntaganda baada ya kumpata na hatia ya kufanya ukatili ikiwa ni pamoja na kuua, kubaka na kuwatumikisha watoto kama askari vitani.