-
Waziri wa Afya Kenya aonya kuhusu hatari ya kuongezeka maambukizi ya COVID-19
Oct 18, 2020 23:35Waziri wa Afya nchini Kenya Mutahi Kagwe ameonya kuwa kuna uwezekano nchi hiyo ikakumbwa na maafa kutokana na wananchi, hasa vijana, kupuuza kanuni za kiafya za kuzuia maambukizi ya corona au COVID-19.
-
Somalia, Cuba zakanusha madai ya kuachiwa huru madaktari waliotekwa na al-Shabaab
Oct 08, 2020 23:07Serikali za Somalia na Cuba zimekanusha madai ya kuachiwa huru madaktari wawili wa Cuba waliotekwa nyara na kundi la kigaidi la al-Shabaab mwaka jana nchini Kenya.
-
Wanajeshi wa Kenya na Somalia washambuliana kwa risasi mpakani
Sep 27, 2020 04:32Wanajeshi wa Kenya na Somalia wamekabiliana kwa risasi katika mpaka wa pamoja wa nchi mbili hizo jirani za Afrika Mashariki.
-
Jaji Mkuu wa Kenya amtaka Rais Uhuru Kenyatta kulivunja Bunge
Sep 21, 2020 11:07Jaji Mkuu wa Kenya David Maraga Jumatatu ya leo amemshauri Rais Uhuru Kenyatta kulivunja Bunge kwa sababu ya kushindwa kutunga sheria kuhusu usawa wa kijinsia.
-
Tanzania yazuia safari za Kenya Airways nchini humo
Jul 31, 2020 23:33Tanzania imesimamisha shirika la ndege la Kenya (KQ) kufanya safari za kwenda Tanzania kuanzia leo tarehe Mosi Agosti, siku moja baada ya Kenya kutangaza kuwa itafungua anga zake kwa usafiri wa kimataifa isipokuwa kutoka baadhi ya nchi ikiwemo Tanzania.
-
Rais wa Kenya atangaza kurefusha muda wa kafyu kukabiliana na Covid-19
Jul 27, 2020 12:23Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya leo Jumatatu amerefusha kipindi cha kafyu nchini humo kwa siku nyingine 30 na kupiga marufuku uuzaji wa pombe migahawani ili kuzuia maambukizi ya COVID-19 nchini humo.
-
EABC yazitaka nchi zote za Afrika Mashariki kufungua anga zao, kuruhusu utalii na biashara
Jul 14, 2020 08:38Baraza la Biashara la Nchi za Afrika Mashariki (EABC), limezisihi nchi zote za kanda hiyo kufuata mfano wa Tanzania kwa kufungua anga zao ili kuruhusu safari za kimataifa kuingia na kutoka katika nchi zote za kanda hiyo.
-
Wasomi, wanachuo wa Kenya nchini Marekani wakosoa agizo la Trump dhidi yao
Jul 11, 2020 10:18Wahadhiri na wanachuo raia wa Kenya walioko Marekani wamekosoa vikali agizo lililotolewa na rais wa nchi hiyo, Donald Trump, la kutaka wanafunzi wote wa kigeni waondoke nchini humo ndani ya miezi miwili ijayo.
-
Kenya ni nchi ya kwanza Afrika kusambaza intaneti kupitia baluni
Jul 08, 2020 11:35Kenya imekuwa nchi ya kwanza kutoa huduma za inteneti kupitia baloni (puto) na hivyo kuwawezesha maelfu ya watu nchini humo kupata huduma za intaneti kirahisi.
-
Rais Kenyatta alegeza hatua kwa hatua sheria za kukabiliana na corona Kenya
Jul 06, 2020 06:55Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta amelegeza kwa kiasi fulani sheria kali zilizokuwa zimewekwa kwa ajili ya kukabiliana na maambukizi ya ugonjwa wa COVID-19 ambapo umeua watu 150 kufikia sasa nchini humo.