-
Wananchi wa Kenya waandamana kulaani ukatili wa polisi ya nchi hiyo
Jun 09, 2020 03:36Wananchi wa Kenya wamefanya maandamano katika mji mkuu Nairobi, kulaani ukandamizaji na ukatili wa polisi ya nchi hiyo dhidi ya raia.
-
Maandamano ya kulaani ukatili wa polisi ya Marekani yafanyika Kenya, Nigeria
Jun 02, 2020 23:26Miji mikuu ya Kenya na Nigeria jana ilishuhudia maandamano ya kulaani ubaguzi wa rangi na mauaji ya George Floyd, raia wa Marekani mwenye asili ya Afrika aliyeuliwa kikatili na polisi mmoja mzungu katika mji wa Minneapolis, katika jimbo la Minnesota nchini Marekani wiki iliyopita.
-
SAUTI, Raia wa Kenya wakasirishwa na tabia ya Shirika la Umeme la nchi hiyo (Kenya Power) kukatakata huduma hiyo
May 09, 2020 10:26Shirika la Kusambaza Umeme nchini Kenya (Kenya Power), limetuhumiwa kwa kufanya uzembe mkubwa katika utoaji huduma za umeme kwa raia wa nchi hiyo huku wananchi wengi wakiitaka serikali kutoa vibali kwa makampuni mengine kuanza kuusambaza umeme ili kuleta ushindani wa kibiashara.
-
Ethiopia yakiri kutungua ndege ya Kenya katika ardhi ya Somalia
May 09, 2020 08:05Askari wa jeshi la Ethiopia wamekiri kuwa walitungua kimakosa ndege ndogo ya Kenya iliyokuwa imebeba misaada na vifaa vya kupambana na janga la corona katika mji wa Bardale, kusini mwa eneo la Bay nchini Somalia.
-
Mafuriko yaua watu 260 Kenya, Rwanda na Somalia
May 08, 2020 03:48Kwa akali watu 260 wamepoteza maisha kutokana na mafuriko na maporomoko ya udongo yaliyosababishwa na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha katika nchi za Afrika Mashariki za Kenya, Rwanda na Somalia.
-
Sauti, Wamiliki wa magari ya kusafirishia mizigo nchini Kenya watishia kuyaweka kando kwa kudai kuwa wananyanyaswa na serikali
May 07, 2020 12:03Wamiliki na wahudumu katika sekta ya magari ya kusafirishia mizigo (malori) kwa masafa marefu wametishia kuyasusa barabarani magari hayo hadi pale serikali za Kenya na Uganda zitakapolegeza masharti ziliyoyaweka.
-
Hatimaye serikali ya Kenya yapambana na corona kwa kufunga kikamilifu maeneo ya Nairobi na Mombasa + Sauti
May 06, 2020 11:37Hatimaye serikali ya Kenya imeamua kuchukua uamuzi mgumu wa kuifungia kikamilifu baadhi ya mitaa ya Nairobi na Mombasa kwa muda wa siku 15 kutokana na ukaidi wa baadhi ya watu wasioheshimu maagizo ya maafisa wa afya.
-
Rais Kenyatta awasihi Wakenya wachukulie kwa uzito janga la corona
Apr 22, 2020 02:44Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya amesema hatua ya Wakenya kutoupa uzito unaotakiwa ugonjwa wa COVID-19 au corona ndio changamoto kubwa zaidi ya serikali yake katika kukabiliana na ugonjwa huo hatari.
-
Mvua, mafuriko na maporomoko ya ardhi yasababisha maafa Kenya
Apr 21, 2020 03:37Kwa akali watu 12 wamepoteza maisha kutokana na mafuriko na maporomoko ya udongo yaliyosababishwa na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha katika baadhi ya maeneo ya Kenya.
-
Corona yamburuzisha mahakamani Naibu Gavana Kenya, mbunge Tanzania ataka waziri wa SMZ achukuliwe hatua
Apr 07, 2020 10:29Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya amesema ni yeye aliyeamuru Naibu Gavana wa Kaunti ya Kilifi Gideon Saburi akamatwe kwa kile alichosema, uzembe aliofanya wa kukwepa karantini baada ya kurudi safarini kutoka nchini Ujerumani, hali ambayo iliweka hatarini maisha ya Wakenya dhidi ya maambukizi ya virusi vya corona (COVID-19).