Jun 24, 2023 10:43
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia, Sergei Ryabkov alitangaza Alhamisi iliyopita kwamba Moscow haidhani kuwa Rais wa Ufaransa, Emmanuel Macron, ataruhusiwa kuhudhuria mkutano ujao wa kundi la BRICS nchini Afrika Kusini, kwa sababu Paris inatekeleza sera ya chuki dhidi ya Moscow.