-
Mtazamo wa Kiongozi Muadhamu: Kushadidisha Mapambano na Israel; Tiba Pekee ya Palestina
Apr 05, 2018 08:02Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu katika kujibu barua ya hivi karibuni ya Ismail Hania Mkuu wa Idara ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina, Hamas, ametilia mkazo msimamo wa daima wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran wa kuiunga mkono kikamilifu Palestina na wapigana jihadi wake na kusema kuwa, tiba ya kadhia ya Palestina ni kuimarishwa mrengo wa mapambano na muqawama.
-
Kiongozi Muadhamu: Iran imesambaratisha njama za Marekani katika Mashariki ya Kati
Mar 21, 2018 13:34Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kuwa, katika miaka iliyopita, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imeweza kutundika juu bendera ya izza, heshima na uwezo wa kitaifa katika Mashariki ya Kati na imekuwa na nafasi muhimu mno katika kuwasambaratisha matakfiri na kuleta amani na usalama.
-
Ujumbe wa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu kwa mnasaba wa kuwadia mwaka mpya wa Kiirani
Mar 21, 2018 10:01Taifa la Iran limeanza sherehe za mwaka mpya wa Nairuzi kwa ujumbe muhimu wa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, ujumbe ambao una nukta muhimu zinazotia matumaini kuhusiana na mustakbali wa taifa.
-
Kiongozi Muadhamu: Mwaka 1397 hijria shamsia, mwaka wa "kuunga mkono bidhaa za Iran"
Mar 20, 2018 13:46Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyed Ali Khamenei, ameutangaza mwaka mpya wa 1397 hijria shamsia kuwa mwaka wa "kuunga mkono bidhaa za Iran".
-
Kiongozi: Vita vya Miaka Minane vilikuwa na lengo la kuangamiza Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran
Mar 10, 2018 11:23Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema: "Madola makubwa ya kimataifa, yalianzisha vita vya miaka minane vya kulazimishwa dhidi ya taifa la Iran kwa lengo la kuangamiza Mapinduzi ya Kiislamu lakini kutokana na adhama, kujitolea, imani, tadbiri, ushujaa, na uono wa mbali wa vijana, vita hivyo vilimalizika kwa manufaa ya taifa na Mapinduzi ya Kiislamu yakawa yameimarika na kukita mizizi zaidi."
-
Kiongozi: Kujishughulisha Iran na masuala ya eneo hakuna uhusiano wowote na Marekani na Ulaya
Mar 08, 2018 13:06Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyed Ali Khamenei amesema: wakati Marekani inajiingiza kila mahali kwa kuzusha fitina na kufanya uharibifu, kila mara inatilia shaka kuwepo na kujishughulisha Iran na masuala ya eneo la Mashariki ya Kati.
-
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu asisitiza umuhimu wa kupanda miti
Mar 06, 2018 13:45Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu mapema leo amepanda miti miwili ya matunda katika maadhimisho ya Siki ya Kupanda Miti na Wiki ya Maliasili.
-
Kushindwa maadui mbele ya mhimili wa muqawama kwa mtazamo wa Kiongozi Muadhamu
Mar 02, 2018 04:33Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kuwa, Syria leo hii iko katika mstari wa mbele wa muqawama hivyo basi ni jukumu letu kuunga mkono kusimama kidete nchi hiyo na kwamba, Rais wa Syria Bashar al Assad amedhihirika katika sura moja ya mwana muqawama mkubwa na kwamba yupo imara na hakuna shaka yoyote kuhusu Rais Assad; na jambo hilo ni muhimu sana kwa nchi yoyote ile.
-
Kiongozi Muadhamu: Siku ya kusali sala ya jamaa Quds itafika karibuni hivi
Mar 01, 2018 12:10Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, leo Alkhamisi ameonana na kundi la maulamaa wa Syria na kusisitizia wajibu wa kushikamana vilivyo na mambo yanayowaunganisha Waislamu wote. Amesema: Ni matumaini yetu sote tutaiona siku ambayo mtasali sala la jamaa mjini Quds na siku hiyo haiko mbali tena bali itafika karibuni hivi, ni sawa tu kama watu kama sisi tutakuwa bado tupo au hatupo tena.
-
Kiongozi Muadhamu: Vibarua walionyesha uono wa mbali katika matukio ya Mapinduzi na Kujihami Kutakatifu
Feb 26, 2018 11:01Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema, kuwaenzi mashahidi wa baadhi ya matabaka kama vile mashahidi vibarua ni jambo lenye thamani maradufu kwa sababu katika matukio yote ya Mapinduzi ya Kiislamu, na kukabiliana na makundi potovu na pia katika zama za kujihami kutakatifu, vibarua nchini Iran walionyesha ghera na uono wa mbali na kujitokeza katika medani.