-
Kiongozi: Hatua zichukuliwe dhidi ya wanaovuruga uhusiano wa Iran na Jamhuri ya Azerbaijan
Nov 02, 2017 04:45Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesisitiza kuwa kuna wanaopinga uhusiano wa karibu na wa udugu baina ya Iran na Jamhuri ya Azerbaijan, na kwa msingi huo kuna ulazima wa kukabiliana na wanaotekeleza njama hizo.
-
Kiongozi Muadhamu: Nguvu za kiulinzi za Iran si kitu cha kujadiliwa kabisa
Oct 25, 2017 16:44Amirijeshi Mkuu wa vikosi vyote vya ulinzi vya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, uwezo na nguvu za kiulinzi za Iran si kitu cha kujadiliwa kabisa kama ambavyo zana zozote za ulinzi na kitu chochote kile kinacholeta nguvu za taifa la Iran si kitu cha kufanyiwa muamala wa aina yoyote ile.
-
Kiongozi Muadhamu: Kama upande wa pili utayachana makubaliano ya JCPOA, Iran itayararua vipande vipande
Oct 18, 2017 15:21Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesisitiza kuwa, Iran haitayachana makubaliano ya nyuklia ya JCPOA maadamu upande wa pili haujayachana, lakini kama upande huo utayachana, basi Jamhuri ya Kiislamu ya Iran itayararua vipande vipande makubaliano hayo.
-
Kiongozi Muadhamu: Utawala wa Kizayuni unataka kuunda Israel mpya katika eneo hili
Oct 04, 2017 18:09Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu leo usiku ameonana na Rais Recep Tayyip Erdogan na ujumbe alioandamana nao hapa mjini Tehran na kusisitiza kwamba kuna ulazima wa kuongezwa kiwango cha ushirikiano wa nchi mbili kama ambavyo pia ni jambo muhimu sana kuweko maelewano na ushirikiano baina ya Iran na Uturuki katika masuala muhimu ya ulimwengu wa Kiislamu.
-
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu: Hija ni fursa bora ya kuzima harakati za kipropaganda za maadui
Oct 03, 2017 16:03Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kuna kambi kubwa ya kimataifa ya propaganda dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na kusisitiza kwamba: fursa ya Hija ni minbari bora kabisa ya tablighi kwa ajili ya kujenga mawasiliano na walimwengu na kuzima propaganda za upande wa pili.
-
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu: Maadui wanafanya njama za kuzuia jihadi ya taifa la Iran
Oct 03, 2017 16:01Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amezungumzia jitihada kubwa zinazofanywa na maadui kwa ajili ya kuliondoa taifa la Iran hususan vijana katika njia ya jihadi na kufa shahidi, kulifanya limsahau Imam Khomeini na kupotea njia ya wazi ya Mapinduzi ya Kiislamu na kusema kuwa: Kuvutiwa kwa nyoyo za vijana wengi kwenye masuala ya kimapinduzi katika mazingira kama haya ni jambo la kustaajabisha.
-
Kiongozi Muadhamu: Mwenyezi Mungu amemfanya shahidi Hojaji kuwa kipenzi cha watu
Sep 27, 2017 14:03Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesisitiza kuwa, ikhlasi, nia safi na kufanya harakati kwa wakati na kuhitajia jamii kuuawa shahidi kama huku ni mambo ambayo yamepelekea Mwenyezi Mungu amfanye shahidi Mohsen Hojaji kuwa kipenzi cha watu wote.
-
Kiongozi Muadhamu ashiriki katika kuuaga mwili wa shahid Hojaji
Sep 27, 2017 10:00Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, alfajiri ya leo Jumatano amekwenda katika Msikiti wa Imam Husain AS hapa Tehran na kuusomea Faatiha mwili mtoharifu wa shahid Mohsen Hojaji, aliyeuliwa shahidi na magaidi wa Daesh wakati akilinda Haram ya mjukuu wa Bwana Mtume Muhammad SAW, Bibi Zaynab al Kubra AS nchini Syria.
-
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu: Wamarekani wanapaswa kuona aibu kwa kuwa na Rais kama Trump
Sep 21, 2017 16:16Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Ali Khamenei amekosoa vikali matamshi ya kipumbavu, kijinga na yaliyojaa urongo yaliyotolewa na Rais wa Marekani katika mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mjini New York na kusema kuwa: Matamshi hayo hayakutokana na nguvu bali yametokana na ghadhabu, kuchanganyikiwa na akili finyu.
-
Kiongozi Muadhamu: Ufumbuzi wa suala la Myanmar ni nchi za Kiislamu kuchukua hatua za kivitendo
Sep 12, 2017 07:56Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amekosoa kimya na kutochukua hatua jumuiya za kimataifa na wanaojigamba kuwa watetezi wa haki za binadamu kuhusiana na matukio ya maafa yanayojiri Myanmar na kusisitiza kwamba: Njia ya utatuzi wa kadhia hii ni kuchukuliwa hatua za kivitendo na nchi za Kiislamu na kuishinikiza kisiasa na kiuchumi serikali isiyo na huruma ya Myanmar.