-
Kiongozi Muadhamu: Kulindwa moyo wa kimapinduzi na kidini katika udiplomasia ni jambo la dharura
Aug 26, 2017 15:52Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu leo Jumamosi ameonana na Rais Rouhani na baraza lake la mawaziri na kusema kuwa, kulindwa msimamo na muelekeo wa kimapinduzi na kidini katika siasa za kigeni za Iran ni jambo muhimu sana.
-
Ayatullah Shahroudi ateuliwa Mkuu wa Halmashauri ya Kuainisha Maslahi ya Mfumo wa Jamhuri ya Kiislamu
Aug 14, 2017 15:22Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amemteua Ayatullah Sayyid Mahmoud Hashemi Shahroudi kuwa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kuainisha Maslahi ya Mfumo wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kwa muhula wa miaka mitano.
-
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi aidhinisha kura za wananchi na kumpasisha Rouhani kuwa Rais wa Iran
Aug 03, 2017 08:21Sherehe ya kuidhinisha kura za wananchi kwa Rais wa Jamhuri ya Kiislamu zimefanyika leo asubuhi katika Husseiniya ya Imamu Khomeini (M.A) hapa Tehran kwa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu kumpasisha Hassan Rouhani kuwa Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Kiongozi Muadhamu alishukuru jeshi la SEPAH, kwa kushambulia maeneo ya magaidi Syria
Jul 06, 2017 04:10Saa moja baada ya Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran SEPAH kushambulia kwa makombora maeneo ya magaidi wa kundi la Daesh huko Deir Ezzor nchini Syria, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, alikutana na makamanda wa SEPAH na kuwashukuru kutokana na hatua yao hiyo.
-
Kiongozi Muadhamu: Ni wajibu kwa Umma wa Kiislamu kupambana na Israel
Jun 26, 2017 16:29Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Ali Khamenei amesema kuwa, kwa mujibu wa fiqhi ya Kiislamu, Waislamu wote wanawajibika kupambana na kupigana jihadi kwa kutumia njia zote zinazowezekana dhidi ya adui anayevamia na kukalia kwa mabavu ardhi ya Kiislamu; kwa msingi huo hii leo ni wajibu kwa ulimwengu mzima wa Kiislamu kupambana na utawala ghasibu wa Israel.
-
Mtazamo wa Kiongozi Muadhamu: Wajibu wa kupambana na utawala wa Kizayuni wa Israel
Jun 26, 2017 13:47Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Ali Khamenei leo amehutubia Baraza la Iddil Fitri lililowakutanisha pamoja viongozi, matabaka mbalimbali ya wananchi na mabalozi wa nchi za Kiislamu mjini Tehran na akisisitiza kuwa kupuuza na kulisahaulisha suala la Palestina ni hatari kubwa.
-
Kiongozi Muadhamu: Siku ya Quds; nembo ya mapambano dhidi ya uistikari na mabeberu
Jun 22, 2017 13:36Akizungumza hapo siku ya Jumatano alasiri na wahadhiri, wanachama wa majopo ya kielimu, watafiti na wasomi wa vyuo vikuu, Ayatullah Ali Khamenei, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ameashiria nafasi muhimu na isiyo na mbadala ya wahadhiri katika malezi ya wanachuo na kuainisha muelekeo wa Iran katika ulimwengu wa leo uliojaa matukio na kusema kuwa Siku ya Kimataifa ya Quds ina umuhimu mkubwa.
-
Kiongozi: Kupambana na utawala wa Kizayuni ni kupambana na ubeberu na uistikbari
Jun 22, 2017 03:36Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ameitaja Siku ya Kimataifa ya Quds kuwa yenye umuhimu mkubwa na kuongeza kuwa: "Siku hii mbali na kuwa ni siku ya kuunga mkono taifa lililodhulumiwa pia ni nembo ya kupambana na uistikbari na ubeberu duniani."
-
Kiongozi: Jamhuri ya Kiislamu ya Iran iko imara, itatoa pigo kwa adui
Jun 19, 2017 03:53Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imesimama imara na kwamba taifa la Iran litatoa pigo kwa adui.
-
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu: Mashambulizi ya kigaidi ya Tehran hayatavuruga azma ya taifa la Iran
Jun 09, 2017 08:21Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Ali Khamenei ametoa ujumbe wa rambirambi kwa mnasaba wa mashambulizi ya kigaidi yaliyofanyika siku chache zilizopita mjini Tehran akisisitiza kuwa, jinai hiyo haiwezi kutia doa katika irada na azma ya taifa la Iran.