-
Ayatullah Khamenei: Utawala wa Kizayuni nusura kusambaratika kabisa kufuatia mapigo makali ya jeshi la Iran
Jun 26, 2025 12:35Ayatullah Khamenei, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran ametoa ujumbe wa tatu kupitia televisheni ya taifa kwa wananchi wa Iran akiwashukuru na kuwapongeza kwa msimao wao wa kutetea na kuunga mkono kwa dhati mfumo wa Mapinduzi ya Kiislamu, hasa baada ya kushambuliwa na utawala haramu wa Israel kwa uungaji mkono na msaada wa moja kwa moja wa Marekani.
-
Kiongozi Muadhamu katika ujumbe wa Hija: Mataifa ya Kiislamu lazima yakabiliane na jinai za Wazayuni
Jun 05, 2025 03:49Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ametoa ujumbe muhimu kwa mnasaba wa msimu wa Hija ya mwaka huu; ambapo ameitaja Hija kuwa ibada ya kuhajiri kutoka katika maisha ya kimaada na kwenda katika maisha ya tauhidi na kumpwekesha Allah.
-
Kiongozi Muadhamu: Matamshi ya Trump ni fedheha kwa taifa la Marekani
May 17, 2025 07:53Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei amekosoa matamshi ya hivi karibuni ya Rais Donald Trump wa Marekani na kuyataja kuwa ni "fedheha" kwa taifa la Marekani.
-
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu: Hakuna maslahi makuu kwa Umma wa Kiislamu kuliko Umoja
May 04, 2025 08:09Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Ali Khamenei, amesema kuwa lengo la Mwenyezi Mungu katika kwa kuweka ibada ya Hajj ni kuwasilisha kielelezo kamili na kinachoelekeza namna ya kuendesha maisha ya binadamu, na akaongeza: muundo na sura ya dhahiri ya ibada hii ni ya kisiasa kabisa, huku maudhui yake yakiwa ya kiroho na ya ibada, ili kuhakikisha manufaa kwa wanadamu wote.
-
Kiongozi Muadhamu: Siku ya Quds ya mwaka huu itakuwa ya aina yake
Mar 27, 2025 23:31Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei amesema maandamano ya Siku ya Kimataifa ya Quds mwaka huu yanayofanyika leo Ijumaa ya Machi 28 kote duniani yana umuhimu mkubwa kuliko miaka iliyopita.
-
Kiongozi wa Mapinduzi: Mwaka 1404 ni "Mwaka wa Uwekezaji kwa ajili ya Uzalishaji"
Mar 20, 2025 07:42Ayatullah Khamenei Kiongozi Muadhamu uwa Mapinduzi ya Kiislamu ametuma ujumbe kwa mnasaba wa kuanza mwaka mpya wa 1404 hijria shamsia na kuutaja mwaka huu mpya kuwa ni "Mwaka wa Uwekezaji kwa ajili ya Uzalishaji."
-
Kiongozi Muadhamu: Iran inakabiliwa na muungano wa madola ya kinafiki
Mar 03, 2025 03:38Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei amesema Jamhuri ya Kiislamu haina tatizo na mataifa mengine; lakini hata hivyo inakabiliwa na muungano mpana wa "madola ya kinafiki" yanayojaribu kuingilia mambo yake ya ndani na kuvuruga uhusiano wake wa nje.
-
Mwakilishi wa Kiongozi wa Mapinduzi awasalia Mashahidi wa Hizbullah, bahari ya umati wa watu yaifunika Beirut
Feb 23, 2025 11:28Sheikh Muhammad Yazbek, Mwakilishi wa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ameongoza Sala ya Maiti ya kusalia miili ya Mashahidi Sayyid Hassan Nasrullah na Sayyid Hashim Safiyyuddin katika mazishi ya kihistoria yaliyofanyika leo katika mji mkuu wa Lebanon, Beirut.
-
Kiongozi Muadhamu: Maandamano dhidi ya Israel yanaashiria kuungwa mkono zaidi Palestina duniani
Feb 22, 2025 08:36Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei amesema maandamano na mikusanyiko dhidi ya Israel barani Ulaya na Marekani inaashiria kuongezeka mshikamano wa kimataifa na taifa la Palestina.
-
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu: Mpango wa kijinga wa Marekani kuhusu Gaza hautafika popote
Feb 18, 2025 11:45Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, akiwapongeza wapiganaji wa Muqawama kwa ushindi wao katika Ukanda wa Gaza, amesisitiza kwamba kazi kubwa ya viongozi na wapiganaji wa Muqawama wa Palestina ipo katika "umoja na mshikamano" na "kusimama imara" dhidi ya adui, kuendesha mchakato mgumu wa mazungumzo, pamoja na uvumilivu na ustahimilivu wa wananchi, ambavyo vimeinua heshima ya Muqawama katika eneo.