Sep 04, 2019 04:30
Marekani imekuwa na nafasi kubwa sana katika vita na mauaji yanayoendelea kufanywa na Saudi Arabia na washirika wake huko Yemen kutokana na misaada ya himaya yake ya kilojistiki, kipelelezi na zana za kivita kwa muungano huo. Suala hilo sambamba na ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu unaofanywa na utawala wa kifalme wa Saudia, vimezidisha malalamiko na upinzani dhidi ya misaada na ushirikiano wa kijeshi wa Marekani na Saudia na washiriki wake katika vita vya Yemen.