-
Ulyanov: Vikwazo dhidi ya Iran vitaondolewa karibuni
Aug 16, 2022 03:04Mwakilishi wa Kudumu wa Russia katika Taasisi za Kimataifa zenye makao yao mjini Vienna, Austria amesema yumkini vikwazo dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran vitaondolewa karibuni hivi.
-
Amir-Abdollahian: Leo tunakabidihi mapendekezo yetu ya mwisho katika JCPOA
Aug 15, 2022 07:57Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema, siku zijazo ni siku muhimu kuhusiana na makubaliano ya nyuklia ya JCPOA na kwamba Tehran inasubiri uamuzi kutoka upande wa Marekani kuhusu maudhui ya tatu.
-
DAESH (ISIS) wametumia asilimia 90 ya silaha za Marekani katika operesheni za kigaidi
Aug 15, 2022 06:07Mtaalamu mmoja wa masuala ya kiusalama amesema, asilimia 90 ya wahanga na waathirika wa ugaidi nchini Iraq hasa katika maeneo yaliyokombolewa wameuliwa kwa silaha za Marekani.
-
Onyo la Russia kuhusu uwezekano wa kuvunja uhusiano wa kidiplomasia na Marekani
Aug 14, 2022 04:14Kutokana na Marekani kuendeleza sera za uhasama dhidi ya Russia na vitisho ilivyotoa vya kuitangaza Russia nchi inayofadhili na kuunga mkono ugaidi, Moscow imeonya kuwa, kuchukuliwa uamuzi huo kutaufikisha uhusiano wa pande mbili kwenye nukta isiyorudishika nyuma na kuna uwezekano hata wa kuvunjika uhusiano wa kidiplomasia baina ya Russia na Marekani.
-
Kissinger: US ipo katika ncha ya kuingia vitani na Russia, China
Aug 14, 2022 02:48Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani amesema Washington imepuuza diplomasia, na kutukuwepo kiongozi thabiti, dunia inajongelewa na vita kutokana na mizozo ya Ukraine na Taiwan.
-
Abdollahian: Lugha ya vitisho dhidi ya Iran haitaambulia chochote
Aug 13, 2022 22:31Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema Marekani inapaswa kufahamu kuwa, kutumia lugha ya vitisho dhidi ya taifa la Iran hakutakuwa na manufaa yoyote kwa Washington.
-
Marekani imeanzisha vita 400, robo barani Afrika na Asia Magharibi
Aug 13, 2022 06:51Utafiti mpya umefichua kuwa, zaidi ya robo ya vita vilivyoanzishwa na Washington katika historia ya Marekani vimefanyika katika nchi za Afrika na eneo la Asia Magharibi (Mashariki ya Kati).
-
Marandi: Matukio kuhusu Bolton na Salman Rushdie yanatia shaka
Aug 13, 2022 06:41Mshauri wa timu ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika mazungumzo ya uondoaji vikwazo huko Vienna ameshangazwa na sadfa ya matukio mawili ya hivi karibuni huko Marekani, na kuashiria kuwa yumkini matukio hayo yanafungamana na mazungumzo ya kujaribu kuhuisha makubaliano ya nyuklia ya JCPOA.
-
Russia yaonya juu ya uwezekano wa kuvunja uhusiano na Marekani
Aug 13, 2022 03:43Afisa mmoja katika wizara ya mambo ya nje ya Russia ameonya kuwa uhusiano wa nchi hiyo na Marekani unaweza ukafika kwenye "nukta isiyoweza kurudishika nyuma" na mbaya zaidi kuliko ya hivi sasa.
-
Iran: Marekani haiwezi kuficha jinai zake kwa kuibua madai bandia
Aug 12, 2022 21:02Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kitendo cha Marekani cha kuibua tuhuma na madai yasiyo na msingi wala mashiko yoyote hakiwezi kuficha wala kuhalalisha jinai za serikali ya Washington.