-
China: Marekani inahatarisha amani kwenye langobahari la Taiwan, mapigano yanaweza kutokea
May 19, 2021 01:34China imekosoa harakati za kichochezi zinazofanywa na Marekani katika langobahari la Taiwan na kueleza kwamba, kuweko manowari ya Marekani katika eneo hilo kunahatarisha amani na uthabiti katika njia hiyo ya baharini ya maji ya kimataifa.
-
Ripoti ya New York Times kuhusu kuongezeka duniani malalamiko dhidi ya utawala wa Kizayuni
May 19, 2021 00:05Gazeti la New York Times limechapisha ripoti inayoonyesha kuongezeka ulimwenguni malalamiko na maandamano yaliyo dhidi ya utawala wa Kizayuni wa Israel kufuatia jinai na mashambulio yake ya kinyama dhidi ya Wapalestina wasio na hatia.
-
Kikao cha tatu kisicho na tija cha Baraza la Usalama kuhusu Palestina, kuendelea ukwamishaji wa Marekani
May 17, 2021 04:09Kwa mara nyingine tena, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limeshindwa hata kulaani jinai za utawala wa Kizayuni kutokana na ukwamishaji wa dola la kibeberu la Marekani.
-
Asasi za Kiislamu Marekani zasusia dhifa ya Idi White House kulalamikia uungaji mkono wa Washington kwa jinai za Israel
May 16, 2021 23:05Jumuiya na asasi za Kiislamu nchini Marekani zimesusa kuhudhuria dhifa ya kila mwaka ya Idul-Fitri inayoandaliwa na Ikulu ya White House kulalamikia uungaji mkono wa serikali ya nchi hiyo kwa jinai za kinyama za utawala haramu wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Wapalestina wakiwemo wa Ukanda wa Gaza.
-
China yasisitiza kutokuwepo uadilifu katika usambazaji wa chanjo ya corona duniani
May 16, 2021 22:05Katika hali ambayo virusi vya corona vinaendelea kuuawa watu wengi duniani na mataifa mengi kutokuwa na uwezo wa kujidhaminia chonjo za kukabiliana na maradhi hayo hatari, nchi tajiri za Magharibi zikiongozwa na Marekani zinaendelea kutekeleza ugaidi wa dawa na vifaa vya matibabu katika ngazi za kimataifa.
-
Marekani sababu kuu ya jinai za utawala haramu wa Israel dhidi ya Wapaletina
May 12, 2021 21:47Gazeti la Marekani la Washington Post limeashiria mashambulio na jinai za hivi karibuni za utawala haramu wa Israel dhidi ya Wapalestina katika mji mtakatifu wa Quds (Jerusalem) na kusema kuwa sio utawala huo tu ndio unazuia kufikiwa lengo lao tukufu la kuwa na nchi huru bali Marekani pia imekuwa na mchango mkubwa katika masaibu na matatizo ambayo yamewasibu kwa miongo kadhaa sasa.
-
China yapinga unafiki wa Marekani, yasema Washington imeua Waislamu wengi dunia
May 11, 2021 12:42China imepinga unafiki wa Merekani katika madai yake ya kutetea haki za Waislamu waliowachache katika eneo la Magharibi mwa China la Xinjiang, na kusisitiza kuwa, Marekani imeua Waislamu wengi katika vita na operesheni zake za kijeshi kuliko nchi nyingine yoyote duniani.
-
Kikao kisicho na tija cha Baraza la Usalama kuhusu Quds sanjari na ukwamishaji mambo wa Marekani
May 11, 2021 09:47Kikao cha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuhusiana na hali ya mambo huko Quds Palestina kilifanyika Jumatatu ya jana tarehe 10 Mei na kumalizika bila ya natija yoyote.
-
Kufichuliwa mambo mapya kuhusiana na Marekani kumuua kigaidi Luteni Jenerali Soleimani
May 10, 2021 05:00Jumamosi usiku, tovuti ya habari ya Yahoo News iliandika makala na ndani yake ilitoa taarifa mpya kuhusu operesheni ya jinai ya kinyama iliyofanywa na jeshi la kigaidi la Marekani ya kumuua shahidi aliyekuwa kamanda wa kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu SEPAH, Luteni Jenerali Qassem Suleimani.
-
Mwaka wa tatu wa Marekani kujitoa katika mapatano ya JCPOA, juhudi nyingi zisizo na maana
May 09, 2021 21:04Miaka mitatu iliyopita, Mei 8 2018, Donald Trump rais wa zamani wa Marekani aliiondoa rasmi nchi hiyo katika mapatano ya kimataifa ya nyuklia mashuhuri kama JCPOA, kwa madai kwamba yalikuwa mapatano mabaya zaidi kuwahi kufikiwa katika historia ya nchi hiyo.