-
Rais Xi: Marekani ndilo tishio kuu kwa ustawi na usalama wa China
Mar 04, 2021 23:01Rais Xi Jinping wa China amesema Marekani ndilo tishio kubwa zaidi kwa maendeleo na usalama wa nchi hiyo ya Asia.
-
Kuanza kampeni kubwa ya vikwazo ya serikali ya Biden dhidi ya Russia
Mar 04, 2021 22:59Uhusiano wa Marekani na Russia katika serikali mpya ya Marekani na wakati huu wa uongozi wa Joe Biden umezidi kuwa mbaya. Serikali ya Biden mbali na kudhihirisha misimamo iliyodhidi ya Russia, hivi sasa imeanzisha kampeni kubwa ya vikwazo dhidi ya Moscow.
-
Newsweek: Marekani yumkini ikawa kituo kikuu cha kueneza fikra za kibaguzi
Mar 04, 2021 00:46Jarida la kila wiki la Newsweek la Marekkani limeandika kuwa, waitifaki wa serikali ya Washington wana wasiwasi kwamba yumkini fikra na mitazamo ya mirengo yenye misimamo mikali ya kulia ikasambaa pia katika nchi hizo kutoka Marekani.
-
Iran: Wamarekani wawajibike kuhusu jinai wanazofanya huko Yemen, waache bwabwaje
Mar 04, 2021 00:44Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje ya Iran amesema kuwa Wamarekani wanapaswa kuwajibika kutokana na jinai na uhalifu wao wa miaka 6 sasa huko Yemen badala ya kutoa tuhuma zisizo na msingi dhidi ya nchi nyingine.
-
Syria yatuma barua mbili kwa Baraza la Usalama katika kipindi cha masaa 72
Mar 04, 2021 00:43Wizara ya Mambo ya Nje ya Syria imetuma barua mbili katika kipindi cha masaa 72 kwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa na Mwenyekiti wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kulalamikia hujuma dhidi ya mji wa Damascus.
-
Marekani yazidi kujiimarisha kijeshi nchini Syria
Mar 01, 2021 03:20Duru mbalimbali za Syria zimetangaza habari ya kuzidi wanajeshi magaidi wa Marekani, kujiimarisha ndani ya ardhi ya Syria. Duru hizo zimesema, msafara mwingine wa wanajeshi magaidi wa Marekani umevuka Iraq na kujizatiti katika viunga vya al Hasakah, huko kaskazini mashariki mwa Syria.
-
Khatibzadeh: Huu si wakati mwafaka wa kuitishwa kikao cha JCPOA
Feb 28, 2021 23:44Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje wa Iran amesema kuwa, kwa kutilia maanani misimamo na hatua za karibuni za nchi tatu za Ulaya na Marekani, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inaona kuwa huu si wakati mwafaka wa kufanyika kikao kisicho rasmi kilichopendekezwa na Mkuu wa Siasa za Nje za Umoja wa Ulaya baina ya nchi hizo na Tehran kuhusu kadhia ya mapatano ya nyuklia ya JCPOA.
-
Iran: Njia nyepesi kwa Marekani kurejea katika JCPOA ni kuheshimu ahadi zake
Feb 28, 2021 09:48Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa amesema kuwa, njia sahali kabisa kwa Marekani kurejea katika makubaliano ya nyuklia ya JCPOA ni kuheshimu na kufungamana na ahadi ilizotoa juu ya mapatano hayo ya kimataifa.
-
Makundi ya muqawama Iraq yaapa kujibu chokochoko mpya za Marekani
Feb 27, 2021 08:33Harakati za muqawama za Iraq zimelaani vikali mashambulizi ya anga ya jeshi la Marekani yaliyolenga kambi za makundi hayo ya kupambana na ugaidi katika mpaka wa Iraq na Syria, na kusisitiza kuwa, chokochoko hizo mpya za Washington hazitapita bila kupewa jibu kali.
-
Biden akosolewa kwa kutomuwekea vikwazo Bin Salman kwa mauaji ya Khashoggi
Feb 27, 2021 08:32Mashirika ya kutetea haki za binadamu yamekosoa vikali hatua ya utawala wa Rais Joe Biden wa Marekani ya kuamua kutomuwekea vikwazo Mohammad Bin Salman, mrithi wa kiti cha ufalme wa Saudi Arabia, licha ya kukiri katika ripoti kuwa ndiye aliyetoa amri ya kuuawa Jamal Khashoggi, mwandishi wa habari aliyekuwa akiukosoa utawala wa Aal-Saud.