-
Mgogoro wa Corona na kuongezeka idadi ya vifo nchini Marekani
Apr 17, 2020 00:16Chuo Kikuu cha Johns Hopkins nchini Marekani kimetangaza kuwa karibu watu 5000 wamefariki dunia katika kipindi cha masaa 24 yaliyopita kutokkana na virusi vya Corona.
-
Waislamu wawasaidia madaktari na wauguzi nchini Marekani
Apr 17, 2020 00:10Kufuatia uhaba wa vifaa vya wauhudumu wa afya katika hospitali za Marekani, Waislamu wa nchi hiyo wameunda kundi la kujitolea katika kupambana na virusi vya Corona.
-
Tahadhari ya Russia kuhusiana na kuutumia kisiasa mgogoro wa corona
Apr 16, 2020 23:53Katika kipindi hiki cha mgogoro wa mlipuko wa virusi vya corona, Marekani ambayo ni kinara wa nchi za Magharibi imeendeleza siasa zake zisizo za kibinadamu dhidi ya nchi hasimu na wapinzani wake, hususn katika kuzidisha vikwazo vya kiuchumi na kuzizuia kupata misaada ya kimataifa. Suala hili limekosolewa sana na madola mengine makubwa duniani.
-
Kwa mara nyingine UN yaitaka Marekani iondoe vikwazo vyake duniani wakati huu wa corona
Apr 16, 2020 03:12Msemaji wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kwa mara nyingine ametilia mkazo mwito wa umoja huo wa kuitaka Marekani ifute vikwazo vyake kwa mataifa ya dunia wakati huu wa vita dhidi ya COVID-19.
-
Umoja wa Afrika walaani kitendo cha Marekani cha kuikatia misaada WHO
Apr 15, 2020 20:15Moussa Faki Mahamat, Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika (AU) amelaani kitendo cha Marekani cha kulikatia misaada ya kifedha Shirika la Afya Duniani (WHO) la Umoja wa Mataifa tena wakati huu wa vita vya dunia nzima dhidi ya corona.
-
Hatua ya Marekani ya kusitisha mchango wake wa kifedha kwa Shirika la Afya Duniani
Apr 15, 2020 08:22Rais Donald Trump wa Marekani ametelekeza kivitendo tishio lake la kusitisha mchango wa kifedha ya nchi hiyo kwa shirika la Afya Duniani (WHO). Trump amedai kuwa, WHO imefeli katika kutekeleza majukumu yake.
-
Kukabiliana na Corona; Changamoto za kimataifa za kuokoa maisha ya wanadamu
Apr 15, 2020 03:13Kuhatarisha afya ya watu kwa malengo ya kisiaisa si tu kuwa ni kinyume cha sheria bali ni ukatili. Hiyo ni kauli ya madakatari na wataalamu 550 wanachama wa Baraza la Kitiba la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ambao wamemuandikia barua Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa na kubainisha nukta hiyo huku wakilalamikia kuendelea sera za vikwazo vya Marekani dhidi ya taifa la Iran.
-
Trump akosolewa na magavana wa Marekani kwa kudai kuwa ana mamlaka mutlaki
Apr 14, 2020 07:07Magavana wa majimbo ya Marekani wamemjia juu Rais Donald Trump wa nchi hiyo baada ya kiongozi huyo kudai kuwa ana uwezo na mamlaka kamili ya kutoa miongozo na maagizo ya kuchukuliwa ya kukabiliana na janga la Corona.
-
Corona yapelekea kutangazwa 'maafa makubwa' katika majimbo yote ya Marekani
Apr 13, 2020 03:40Kufuatia kushtadi mgogoro wa virusi vya Corona nchini Marekani, kwa mara ya kwanza ya historia ya nchi hiyo kumetangazwa hali ya 'maafa makubwa.'
-
Hatimaye corona yailazimisha Tanzania kupiga marufu safari za ndege, Marekani yaongoza kwa vifo na maambukizi
Apr 12, 2020 23:16Hatimaye serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imepiga marufuku safari zote za ndege za abiria za kimataifa ikiwa ni siku chache tu baada ya Rais John Pombe Magufuli wa nchi hiyo kusisitizia msimamo wake wa kutofunga mipaka ya Tanzania akisema kuwa kufunga mipaka hiyo kutaziletea madhara makubwa nchi jirani kama za Uganda, Rwanda, Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.