-
Vikwazo vya Marekani dhidi ya Iran na miito inayoongezeka ya kuondolewa vikwazo hivyo
Mar 19, 2020 10:03Licha ya kuibuka virusi angamizi vya Corona ulimwenguni ikiwemo Iran na kuweko ulazima wa walimwengu wote kukabiliana navyo, lakini Marekani ingali inang’ang’ania kuendeleza utendaji wake wa kivikwazo katika fremu ya sera za vikwazo vya kiwango cha juu kabisa dhidi ya Iran na imekuwa ikitangaza mtawalia vikwazo vipya dhidi ya Tehran.
-
Vikwazo vipya vya Marekani dhidi ya Iran; muendelezo wa sera ya mashinikizo ya kiwango cha juu kabisa
Mar 19, 2020 04:27Serikali ya Trump imeamua kutekeleza sera ya mashinikizo ya kiwango cha juu kabisa dhidi ya Iran; na ili kufanikisha lengo hilo baada ya kujitoa kwenye makubaliano ya nyuklia ya JCPOA mnamo mwezi Mei 2018, ilianza kuiwekea Jamhuri ya Kiislamu vikwazo vikali zaidi kuwahi kushuhudiwa. Lakini licha ya kushindwa kufikia lengo ililokusudia, Washington ingali inang'ang'ania kuongeza vikwazo dhidi ya Tehran.
-
Sanders autaka utawala wa Trump uiondolee Iran vikwazo
Mar 19, 2020 04:21Bernie Sanders, Seneta wa jimbo la Vermont anayewania kuteuliwa kuwa mgombea urais wa Marekani katika uchaguzi wa mwaka huu kwa tiketi ya chama cha Democrat ameeleza kusikitishwa kwake na hatua ya utawala wa Donald Trump ya kushadidishi vikwazo dhidi ya Iran wakati huu ambapo taifa hili linakabiliana na mripuko wa ugonjwa wa Corona.
-
Takwa la Russia la kuondolewa vikwazo visivyo vya kiutu vya Marekani dhidi ya Iran
Mar 17, 2020 23:39Kuendelea vikwazo vya Marekani vyenye wigo mpana na ambavyo havijawahi kushuhudiwa dhidi ya Iran ambavyo vilianza kutekelezwa baada ya Washington kujiondoa katika makubaliano ya nyuklia ya JCPOA Mei 2018, ni hatua ambayo ilikabiliwa na malalamiko na ukosoaji mkubwa katika uga wa kimataifa ambapo hata washirika wa Ulaya wa Washington nao waliikosoa hatua hiyo isiyo ya kibinadamu.
-
Waziri wa Ulinzi wa Marekani na naibu wake wawekwa karantini baada ya maafisa 37 wa Pentagon kupatwa na corona
Mar 17, 2020 12:37Waziri wa Ulinzi wa Marekani Mark Thomas Esper na Naibu wake wamewekwa karantini tangu Jumatatu ya jana baada ya kuthibitika kuwa, maafisa 37 wa wizara hiyo wameambukizwa virisi vya corona.
-
Iraq yaishtaki Marekani Baraza la Usalama baada ya kushambulia vituo vya jeshi la nchi hiyo
Mar 17, 2020 12:13Wizara ya Mambo ya Nje ya Iraq imeishtaki Marekani katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa baada ya jeshi la nchi hiyo kushambulia kambi za jeshi na askari polisi wa Iran.
-
Idara ya Mahakama ya Iran: Vikwazo vya dawa vya Marekani dhidi ya Iran ni kielelezo cha jinai dhidi ya binadamu
Mar 17, 2020 11:34Msemaji wa Idara ya Mahakama nchini Iran amesema kuwa, vikwazo vya kidhalimu vya Marekani kama vikwazo vya dawa na zana za tiba ni kielelezo kikubwa cha utenda jinai wa ubeberu wa kimataifa unaoongozwa na Marekani.
-
Hofu ya Corona; Wamarekani wapiga foleni kununua bunduki
Mar 17, 2020 04:24Foleni ndefu zimeonekana nje ya maduka ya kuuza bunduki na silaha za moto nchini Marekani, wakati huu ambapo wananchi wa nchi hiyo wananunua bidhaa muhimu za msingi kwa pupa kutokana na hofu ya ugonjwa wa Corona.
-
Iraq katika kuihami na kuitetea Al-Hashdu-Sha'abi sambamba na kukabiliana na kupambana na Marekani
Mar 16, 2020 22:10Katika muda wa siku chache zilizopita ndege za kivita za Marekani zilishambulia mara kadhaa kwa makombora ngome za Al-Hashdu-Sha'abi na Muqawama wa Iraq; mashambulio ambayo yamekosolewa vikali na Wairaqi wengi.
-
Uingiliaji wa Marekani katika masuala ya ndani ya Lebanon na kuendelea mwenendo ulio dhidi ya Hizbullah
Mar 15, 2020 05:56Katika kikao cha Ijumaa iliyopita pamoja na Hassan Diab, Waziri Mkuu wa Lebanon, Dorothy Shea, balozi mpya wa Marekani nchini Lebanon sambamba na kuingilia masuala ya ndani ya nchi hiyo ya Kiarabu, alisema kuwa mazingira ya msaada wa Washington kwa ajili ya kuushinda mzozo wa kiuchumi wa taifa hilo, unategemea kutengana serikali ya Beirut na Harakati ya Muqawama ya Hizbullah.