-
Wizara ya Ulinzi ya Marekani (Pentagon) inalenga kupanua wigo wa makabiliano na Russia, China
Jan 29, 2020 03:10Katika zama za utawala wa Rais Donlad Trump, Marekani imekithirisha makabiliano na Russia na China ambazo ni washindani wake wakuu katika uga wa kimataifa. Sera hiyo ya utawala wa Trump ilitiliwa mkazo katika Waraka wa Kistratijia wa Usalama wa Taifa la Marekani mwaka 2018.
-
Indhari ya Umoja wa Ulaya kuhusu kutofikiwa makubaliano ya kibiashara na Uingereza katika kipindi cha baada ya Brexit
Jan 28, 2020 21:57Suala la mpango wa Uingereza wa kujitoa katika Umoja wa Ulaya (Brexit) linahesabiwa kuwa daghadagha muhimu zaidi ya wananchi wa Uingereza.
-
Larijani: Lengo la 'Muamala wa Karne' ni kuwadhalilisha Waislamu
Jan 28, 2020 08:28Spika wa Majilisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) amesema madhumuni ya njama za Marekani dhidi ya Wapalestina kwa jina la 'Muamala wa Karne' ni kuwadhalilisha na kuwatweza Waislamu.
-
Saudia yaipongeza Marekani kwa mauaji ya kigaidi ya Jenerali Soleimani
Jan 28, 2020 08:25Waziri wa Mambo ya Nje wa Saudi Arabia ameipongeza Marekani kwa kumuua shahidi Luteni Jenerali Qassem Soleimani, aliyekuwa Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (SEPAH) pamoja na wanzake kadhaa nchini Iraq.
-
Rouhani: Watu wa Asia Magharibi watakabiliana na dhulma za Marekani
Jan 28, 2020 08:21Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema wananchi wa nchi za eneo la Asia Magharibi watakabiliana na dhulma na ubeberu wa Marekani.
-
Waziri wa Ulinzi wa Marekani akataa kutoa maelezo kuhusu ndege iliyotunguliwa Afghanistan
Jan 28, 2020 02:06Waziri wa Ulinzi wa Marekani amekataa kutoa maelezo kuhusiana na ndege ya nchi hiyo iliyotunguliwa nchini Afghanistan.
-
Meja Jenerali Salami: Marekani itajuta kutoa vitisho dhidi ya makamanda wa SEPAH
Jan 27, 2020 23:17Kamanda Mkuu wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema, Marekani inapaswa ichunge hatua inazochukua na akasisitiza kuwa: Wale ambao wametishia kuwaua kigaidi makamanda wa Iran, kama watabaki hai, bila shaka watajuta tu.
-
Raia wa Venezuela watangaza mshikamano wao na Wairani kupinga ubeberu wa Marekani
Jan 26, 2020 12:44Wawakilishi wa Harakati za Kijamii na Kisiasa nchini Venezuela pamoja na kamati za kisiasa kote duniani, wametangaza mshikamano wao na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na kulinda amani mkabala wa vitisho vya Marekani, kupitia maandamano ya amani yaliyofanyika Jumamosi ya Jana.
-
Hizbullah: Marekani ndiyo sababu ya matatizo yote ya Lebanon
Jan 26, 2020 09:26Naibu Katibu Mkuu wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Hizbullah ya Lebanon amesema Marekani ndiyo chimbuko la matatizo yote yanayoikabili Lebanon.
-
Maveterani wa kivita Marekani wamtaka Trump aombe radhi kwa kudharau hasara kubwa iliyosababishwa na kipigo cha Iran
Jan 25, 2020 23:50Kundi moja la maveterani wa vita vya nje ya Marekani wamemtaka rais wa nchi hiyo Donald Trump aombe radhi kwa kudharau madhara waliyopata wanajeshi wa Marekani baada ya kambi yao ya Ain al Assad ya nchini Iraq kushambuliwa kwa makumi ya makombora ya Iran.