-
Walid al Mualim: Marekani inafuatilia malengo ya Israel nchini Syria
Sep 10, 2018 23:48Waziri wa Mambo ya Nje wa Syria amesema kuwa lengo la Marekani ni kudhibiti shughuli zote za Syria kwa maslahi ya Israel.
-
Shamkhani: Iran haitasalimu amri mbele ya dhulma na uonevu
Sep 10, 2018 23:48Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran amesema kuwa, taifa la Iran kamwe halitasalimu amri mbele ya dhulma, uonevu na udhalilishaji na litawadunisha maadui na wanaolitakia mabaya.
-
Seneta wa Marekani afichua mpango wa Uingereza wa kufanya shambulio la kemikali Syria
Sep 10, 2018 10:22Seneta mmoja wa Marekani amefichua mpango ulioratibiwa na Uingereza kwa ajili ya kufanya shambulio bandia la silaha za kemikali huko Syria.
-
Amiri Jeshi Mkuu: Taifa la Iran limeirudisha nyuma na kuishinda Marekani
Sep 09, 2018 11:43Amiri Jeshi Mkuu wa majeshi yote ya Iran amesema kuwa Jamhuri ya Kiislamu na taifa la Iran limethibitisha kwa kusimama kidete mbele ya Marekani kwamba, iwapo taifa lolote halitaogopa hasira na ghadhabu za mabeberu na kuamini na kutegemea uwezo wake, madola makubwa yatarudi nyuma na hatimaye kushindwa.
-
New York Times: Trump alipanga njama ya mapinduzi dhidi ya Rais wa Venezuela
Sep 09, 2018 11:42Gazeti la New York Times la Marekani imefichua kwamba, serikali ya Rais Donald Trump wa nchi hiyo mwaka jana ilifanya kikao cha siri na majenerali walioasi jeshi la Venezuela kujadili mipango ya kufanya mapinduzi na kumuondoa madarakani Rais Nicolás Maduro wa nchi hiyo.
-
Iran: Marekani inayatumia makundi ya kigaidi kufikia malengo yake
Sep 09, 2018 03:19Waziri wa Ulinzi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema Marekani inatumia njia zote kukiwemo kuyatumia makundi ya kigaidi kufikia malengo yake pasina kujali madhara kwa nchi nyingine.
-
Hashdu Sha'abi: Marekani ndio inayochochea ghasia Basra, Iraq
Sep 09, 2018 02:42Kamanda wa ngazi za juu wa kikosi cha kujitolea cha wananchi nchini Iraq cha Hashdu Sha'abi amesema harkati hiyo ya wananchi tayari imewakabidhi maafisa wa serikali ya Baghdad ushahidi unaoonesha kuwa ubalozi mdogo wa Marekani mjini Basra ndio uliohusika katika kuratibu na kuchochea machafuko yanayoendelea kushuhudiwa hivi sasa katika mkoa wa Basra, kusini mwa nchi hiyo ya Kiarabu.
-
Rais Rouhani: Iran haina adui yeyote zaidi ya Marekani, Israel na vibaraka wao
Sep 08, 2018 03:45Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran sambamba na kubainisha kwamba, hii leo Iran haina adui mwengine yeyote isipokuwa Marekani, utawala wa Kizayuni na vibaraka wao, amesisitiza kwamba, taifa la Iran litawashinda maadui kwa mshikamano na umoja.
-
Kikao cha Baraza la Usalama la UN, baraza la propaganda za Trump dhidi ya Iran
Sep 06, 2018 05:47Mwakilishi wa Iran katika Umoja wa Mataifa amesema kuwa, Marekani ambayo ni mvunjaji mkubwa zaidi wa sheria za kimataifa inalitumia vibaya Baraza la usalama kwa ajili ya kupeleka mbele sera na mipango yake ya kujichukulia maamuzi ya upande mmoja.
-
The National Interest: Wademokrati watamlazimisha Trump kujiuzulu
Sep 05, 2018 22:30Jarida la The National Interest la Marekani limeandika kuwa iwapo Wademokrati watadhibiti Kongresi ya nchi hiyo yumkini wakamlazimisha Donald Trump kujiuzulu.