Jul 20, 2017 14:09
Kitendo cha kuenea video inayomuonyesha mwanamfalme mmoja akifanya ukatili dhidi ya raia wa Saudia, kimeibua hasira kali na ukosoaji mkubwa wa Wasaudi katika mitandao mbalimbali ya kijamii hususan Twitter, na hivyo kumfanya Mfalme Salman bin Abdulaziz Al Saud kutoa amri ya kutiwa mbaroni mwanamfalme huyo.