-
Ukosoaji wa Amnesty International kwa ukatili na ukandamizaji unaofanywa na serikali ya Misri
Sep 19, 2018 22:09Wakati serikali ya Rais Abdel Fattah el-Sisi inaendelea kuwabana na kuwakandamiza wapinzani kwa kutoa hukumu za adhabu kali dhidi yao Shirika la Msamaha Duniani Amnesty International limeeleza kwamba ukandamizaji unaofanywa na serikali ya Cairo dhidi ya uhuru wa kutoa maoni tangu el-Sisi ashike hatamu za madaraka ya nchi ni wa "kiwango cha kutisha na haujawahi kushuhudiwa."
-
Amnesty International: Ukandamiza wa uhuru wa kujieleza Misri umevuka mpaka
Sep 18, 2018 22:40Shirika la kutetea haki za binadamu la Amnesty International limetangaza kuwa, ukandamizaji wa uhuru wa kujieleza nchini Misri katika kipindi hiki cha utawala wa Abdel Fattah al Sisi umefikia kiwango cha tahadhari na haujawahi kuonekana nchini humo.
-
Wafungwa wa kisiasa wanakabiliwa na hali mbaya katika jela za Misri
Sep 13, 2018 09:15Hali ya wafungwa wa kisiasa nchini Misri miaka mitano baada ya mapinduzi ya kijeshi nchini humo inaripotiwa kuwa mbaya sana.
-
EU yalaani kuhukumiwa kifo wananchama wa Ikhwani, Misri
Sep 11, 2018 20:50Umoja wa Ulaya umelaani hukumu ya kifo iliyotolewa na mahakama moja nchini Misri, dhidi ya makumi ya wanachama wa harakati ya Ikhwanul Muslimin.
-
Wanachama 75 wa Ikhwanul Muslimin wahukumiwa kifo nchini Misri
Sep 08, 2018 21:51Mahakama ya rufaa ya Misri imewahukumu adhabu ya kifo wanachama 75 wa kundi la Ikhwanul Muslimin kwa tuhuma za kuhusika katika matukio yanayojulikana kwa jina la "Rābiʿa al-ʿAdawiyya" kama ambavyo pia imewahukumu kifungo cha maisha jela wanachama wengine 46 wa kundi hilo.
-
Rais Sisi aidhinisha sheria inayodhibiti matumizi ya mitandao
Sep 02, 2018 22:15Rais wa Misri Abdel Fattah al-Sisi ameidhinisha sheria mpya ya kudhibiti mitandao ya kijamii katika kile kinachotajwa kuwa ni muendelezo wa sera za kukandamiza upinzani.
-
Wanaharakati Misri wataka kuachiwa huru wapinzani
Aug 28, 2018 04:35Muungano wa wanaharakati wa kisekulari na mrengo wa kushoto nchini Misri umekemea hatua ya vyombo vya usalama nchini humo ya kuwatia nguvuni shakhsia kadhaa wa upinzani na kutoa wito wa kuachiwa huru wafungwa wote wasiokabiliwa na tuhuma za kuhusika na machafuko.
-
Saudia inadhamini nakisi ya bajeti yake kwa kuongeza gharama za Hija
Aug 18, 2018 23:38Saudi Arabia inakidhi nakisi ya bajeti yake ya mwaka kwa kuzidisha gharama za ibada ya Hija, suala ambalo limewakasirisha mahujaji kutoka nchi mbalimbali hususan mahujaji kutoka Misri.
-
Jumuiya za kutetea haki za binadamu: Serikali ya al Sisi inakandamiza wapinzani
Aug 16, 2018 23:19Jumuiya saba za kutetea haki za binadamu nchini Misri zimeikosoa serikali ya nchi hiyo zikisisitiza kuwa mienendo yake dhidi ya wapinzani inakiuka sheria.
-
Kiongozi wa Ikhwanul Muslimina ahukumiwa kifungo cha maisha jela, Misri
Aug 12, 2018 22:22Kiongozi wa harakati ya Ikhwanul Muslimina ya Misri na maafisa wengine kadhaa wa ngazi za juu wa harakati hiyo wamehukumiwa kifungo cha maisha jela kwa tuhuma za kuchochea mauaji na machafuko katika ghasia zilizotokea nchini humo miaka mitano iliyopita.