-
Sharif: Maandamano ya Siku ya Quds ni nembo ya Umoja wa Umma wa Kiislamu
May 26, 2018 15:26Mkuu wa Idara ia Intifadha na Quds Katika Shirika la Tablighi ya Kiislamu la Iran Jenerali Ramadhan Sharif amesema: "Maandamano ya Siku ya Quds nchini Iran na maeneo mengine duniani sasa yamegeuka kuwa jukwaa la Umoja wa Ulimwengu wa Kiislamu na kuunga mkono watu wa Palestina."
-
Waziri wa Uhajiri wa Denmark atoa matamshi ya kuuvunjia heshima mwezi mtukufu wa Ramadhani
May 22, 2018 08:01Waziri wa Uhajiri, Mshikamano na Maskani wa Denmark ametoa matamshi ya chuki na uadui dhidi ya Uislamu kwa kuwataka Waislamu wa nchi hiyo wanapoanza kufunga na katika kipindi chote cha mwezi mtukufu wa Ramadhani wachukue likizo makazini akidai kwamba amali za mwezi huo ni "hatari" kwa watu wote nchini humo.
-
Rais Rouhani: Marekani haiwezi kukabiliana na taifa imara la Iran
May 21, 2018 08:11Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kwamba kamwe Marekani haitoweza kulipigisha magoti taifa imara la Iran.
-
Misri yafungua kivuko cha Rafah kwa ajili ya Ramadhani
May 19, 2018 04:14Misri imefungua tena kivuko cha Rafah, njia pekee inayotumiwa kufikishia misaada ya dharura kwa Wapalestina karibu milioni mbili walio chini ya mzingiro huko Ukanda Gaza tangu mwaka 2007 na kusema kuwa eneo hilo la mpakani litasalia wazi katika mwezi huu mtukufu wa Ramadhani.
-
Mtazamo wa Kiongozi Muadhamu: Ukombozi usioepukika wa Palestina, kushindwa kusikokwepeka kwa Marekani + Picha
May 18, 2018 18:24Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesisitiza kuwa, Baytul Muqaddas ndio mji mkuu wa Palestina na kwa taufiki na uwezo wa Mwenyezi Mungu Palestina itakombolewa tu kutoka katika makucha ya maadui na kwamba Marekani na vitimbakwiri vyake hawawezi kufanya upuuzi wowote mbele ya uhakika na sunna hiyo ya Mwenyezi Mungu.
-
Matukio ya Kiislamu Afrika Mashariki na Harith Subeit + Sauti
May 18, 2018 18:17Kama kamawaida, wiki hii pia iliyosadifiana na kuanza mwezi mtukufu wa Ramadhani imesheheni matukio ya kila namna ya Kiislamu duniani ukiwemo ukanda wa Afrika Mashariki na Kati. Harith Subeit na baadhi ya matukio hayo...
-
Waislamu Uganda watakiwa kutumia vyema nyakati za Ramadhani + Sauti
May 18, 2018 18:14Waislamu nchini Uganda na duniani kiujumla wamehimizwa kujiweka mbali na mambo yanayomkasirisha Mwenyezi Mungu na kutumia vizuri nyakati muhimu za mwezi huu mtukufu wa Ramadhani. Mwandishi wetu Kigozi Ismail ametuandalia ripoti ifuatayo.
-
Kiongozi Muadhamu: Kukombolewa Palestina ni kanuni ya Allah ambayo Marekani haiwezi kukabiliana nayo
May 18, 2018 04:27Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kuwa, moja ya mahitaji muhimu na ya lazima ya umma wa Kiislamu hii leo, ni udharura wa kushikamana na Qur'an Tukufu na kuifanyia kazi.
-
Spika wa Bunge la Iran awatumia salamu za Ramadhani maspika wa mabunge
May 16, 2018 14:08Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu, Bunge la Iran, Ali Larijani amewatumia maspika wa mabunge ya nchi za Kiislamu salamu kwa mnasaba wa kuwadia Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.
-
Waislamu wa Marekani wana hatari ya kunyanyaswa zaidi mwezi wa Ramadhani
May 10, 2018 14:31Baraza la Uhusiano wa Marekani na Uislamu limetaka kuchukuliwa hatua za lazima za kuimarisha usalama kwa ajili ya kuwalinda Waislamu ambao wana hatari ya kukumbwa na mashambulizi na unyanyasaji zaidi katika kipindi cha mwezi mtukufu wa Ramadhani.