-
Nchi za eneo la Sahel zatishia kusimamisha ndege za Nigeria iwapo anga ya nchi hizo itakiukwa
Dec 09, 2025 11:28Shirikisho la Nchi za Sahel barani Afrika linalojumuisha Mali, Niger na Burkina Faso (AES) limetangaza kuwa litazizuia ndege zote zinazokiuka anga yashirikisho hilo kufuatia ripoti za ukiukaji wa sheria uliofanywa na Nigeria.
-
Serikali ya Nigeria yafanikisha kuachiwa huru watoto 100 waliotekwa nyara katika jimbo la Niger
Dec 08, 2025 06:26Serikali ya Nigeria imefanikisha kuachiliwa huru watoto 100 wa skuli waliotekwa nyara mwezi uliopita katika Jimbo la Niger. Hayo ni kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa na televisheni ya Channels Television jana Jumapili.
-
Wabeba silaha wateka nyara watu wengine 14 Nigeria, yumo bibi harusi na kitoto kichanga
Dec 01, 2025 05:44Washambuliaji wenye silaha wamewateka nyara wanawake 13 na mtoto mchanga katika hujuma mpya ya uvamizi uliofanywa usiku wa kuamkia jana Jumapili kaskazini mashariki mwa Nigeria, ukiwa ni mwendelezo wa matukio ya hivi karibuni ya utekaji nyara mkubwa unaoshuhudiwa katika taifa hilo la Afrika Magharibi.
-
Rais wa Nigeria: Wanafunzi wa kike 24 waliotekwa nyara wiki jana wakombolewa
Nov 26, 2025 07:13Wanafunzi wa kike 24 waliokuwa wametekwa nyara kutoka katika shule yao ya bweni wiki iliyopita kaskazini magharibi mwa Nigeria wamekombolewa. Hii ni kwa mujibu wa taarifa kutoka ofisi ya Rais.
-
Raia wengi wakimbia makazi yao baada ya magaidi kuteka nyara mabinti 13 katika jamii ya Borno, Nigeria
Nov 24, 2025 14:39Wimbi la hofu limeikumba jamii ya Borno, na raia wengi wameanza kuondoka majumbani mwao leo Jumatatu, siku mbili baada ya ISWAP, tawi la kundi Boko Haram, kuwateka nyara mabinti 13 wenye umri wa miaka 15 hadi 20.
-
Wanafunzi 303, walimu 12 watekwa nyara na watu wenye silaha katika skuli ya jimbo la Niger, Nigeria
Nov 23, 2025 06:33Jumuiya ya Wakristo ya Nigeria (CAN) imetangaza kuwa, jumla ya wanafunzi 303 na walimu 12 wametekwa nyara na watu wenye silaha wasiojulikana likiwa ni tukio la pili kubwa kutokea ndani ya wiki moja, huku hofu za usalama zikiongezeka katika nchi hiyo yenye watu wengi zaidi barani Afrika.
-
Mahakama ya Nigeria yamhukumu kifungo cha maisha jela kiongozi wa Wabiafra wanaopigania kujitenga
Nov 22, 2025 02:41Mahakama ya Nigeria imemhukumu Nnamdi Kanu, kiongozi wa harakati ya kupigania kujitenga ya Watu wa Asili wa Biafra (IPOB), kifungo cha maisha jela baada ya kumpata na hatia ya mashtaka yote saba aliyoshtakiwa yanayohusiana na ugaidi.
-
Nigeria yafunga shule katika jimbo la Kwara kufuatia ongezeko la ukosefu wa usalama
Nov 21, 2025 03:01Mamlaka husika katika Jimbo la Kwara nchini Nigeria zimefunga shule zote katika eneo la Iflodun, Ekiti, Irepodun, Isin na Oke Ero kufuatia vitisho vipya vya usalama katika jimbo hilo.
-
Rais wa Nigeria athibitisha kuuawa afisa wa ngazi ya juu wa jeshi
Nov 19, 2025 12:24Rais wa Nigeria amethibitisha kuwa Brigedia jenerali Musa Uba ameuawa na kundi la kigaidi akiwa matekani. Mauaji hayo yamefanywa siku chache baada ya afisa huyo wa ngazi ya juu wa jeshi la Nigeria kutekwa nyara na wanamgambo wa kundi la ISWAP kufuatia shambulio la kuvizia kaskazini mashariki mwa Jimbo la Borno ambalo pia liliwaua wanajeshi wanne.
-
Mkuu wa jeshi la Nigeria aagiza kutafutwa usiku na mchana mabinti wa shule waliotekwa nyara
Nov 19, 2025 02:23Jenerali wa ngazi ya juu wa jeshi la Nigeria ameviagiza vikosi vya jeshi hilo kuendesha msako wa "usiku na mchana" ili kuwanusuru mabinti 25 wa shule waliotekwa nyara kaskazini-magharibi mwa nchi hiyo.