Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza udharura wa kukuza ushirikiano kati ya Tehran na Islamabad katika nyanja mbalimbali.
Rais Ebrahim Raisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amewasili katika mji mkuu wa Pakistan Islamabad katika ziara rasmi ya kikazi yenye lengo la kuimarisha usalama na uhusiano wa kibiashara kati ya nchi mbili.
Watu wasiopungua 168 wamepoteza maisha katika matukio yaliyosababishwa na mvua, baada ya mvua kali na mafuriko kuikumba Pakistan na nchi jirani ya Afghanistan.
Serikali ya Pakistan imechukua uamuzi wa kushtukiza na uliowashangaza na kuwapiga butwaa watu wengi, nao ni wa kuiweka harakati ya Zainabiyyun kwenye orodha yake ya tasisi za kigaidi licha ya kwamba harakati hiyo muda wote imekuwa ikipigania amani na usalama kwa Pakistan.
Watu wenye silaha wameua abiria wasiopungua 11 katika matukio mawili tofauti yaliyojiri kusini magharibi mwa Pakistan.
Rais Ebrahim Raisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema, kustawishwa uhusiano wa Iran na Pakistan hakufurahishi madola ya kibeberu na kwa hivyo yanazusha fitna ili kuleta mpasuko kati ya mataifa hayo mawili na nchi hizo mbili za Kiislamu.
Kamanda wa Kikosi cha Nchi Kavu cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (SEPAH) amesema kuwa, hadi hivi sasa magaidi 15 wameshaangamizwa katika operesheni za kuzima mashambulizi matatu ya kigaidi yaliyofanywa na magaidi hao kusini mashariki mwa Iran.
Musadik Masood Malik, Waziri wa Mafuta wa Pakistan amesema kuwa nchi yake inahitajia mno gesi ya Iran na kwamba msimamo wa Islamabad uko wazi kuwa, kukamilishwa mradi wa kupelekwa gesi ya Iran nchini Pakistan ni jambo la dharura.
Kiongozi wa kundi la kigaidi la "Jaish al-Dhulm" ameuawa katika shambulio la askari usalama wa Iran.
Tume ya Uchaguzi ya Pakistani imetangaza matokeo ya mwisho ya uchaguzi wa bunge nchini humo, na wagombea huru wenye mfungamano na chama cha Tehreek-e-Insaf cha Imran Khan wamenyakua viti 101.