-
Haniya: Kuanzisha uhusiano na Israel ni kuupiga jambia umma wa Kiislamu
Dec 24, 2020 04:34Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS amesema kitendo cha baadhi ya nchi za Kiarabu cha kuanzisha uhusiano wa kawaida na utawala wa Kizayuni wa Israel ni sawa na kuwapiga jambia kwa nyuma wananchi wa Palestina na umma wa Kiislamu kwa ujumla.
-
Kutangaza msimamo wa wazi Pakistan wa kupinga kuanzisha uhusiano wa kawaida na utawala wa Kizayuni
Dec 23, 2020 09:31Waziri wa Mambo ya Nje wa Pakistan amepinga aina yoyote ya mashinikizo ya nje dhidi ya nchi hiyo kwa ajili ya kujiunga na safau ya nchi zinazoanzisha uhusiano wa kawaida na utawala wa Kizayuni na kueleza kuwa: Islamabad katu haitaitambua rasmi Israel.
-
Wananchi wa Nigeria waandamana kuiunga mkono Palestina na kupinga kuanzishwa uhusiano na Israel
Dec 21, 2020 23:27Wananchi wa Nigeria wameandamana na kutangaza uungaji mkono wao kwa taifa la Palestina na kupinga harakati za baadhi ya mataifa ya Kiarabu za kuanzisha uhusiano wa kawaida na utawala haramu wa Israel.
-
Mamlaka ya Ndani ya Palestina yalalamikia kimya cha Baraza la Usalama kuhusu uvamizi wa walowezi wa Kiyahudi
Dec 20, 2020 23:22Wizara ya Mambo ya Nje ya Mamlaka ya Ndani ya Palestina imelitaka Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuacha kunyamazia kimya uvamizi wa walowezi wa Kizayuni na badala yake uwajibike kivitendo.
-
Palestina yachaguliwa tena kuwa mwanachama wa kamati ya utendaji ya Mahakama ya ICC
Dec 19, 2020 08:39Palestina kwa mara ya pili mtawalia imechaguliwa katika kikao cha nchi wanachama wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC ) kuwa mwanachama wa kamati ya utendaji ya mahakama hiyo.
-
Vyama vya kisiasa Algeria vyakosoa vikali kuanzishwa uhusiano kati ya Morocco na utawala wa Kizayuni
Dec 14, 2020 23:31Vyama vya kisiasa nchini Algeria vimekosoa vikali hatua ya Morocco ya kuanzisha uhusiano wa kawaida na utawala wa Kizayuni wa Israel na kusisitiza kuwa kitendo hicho ni pigo la kidhalili kwa mataifa ya Algeria, Palestina na Sahara Magharibi.
-
Hania: Hamas ni nembo ya malengo ya Palestina na kuendelezwa muqawama
Dec 14, 2020 04:26Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) amesema kuwa kuundwa harakati ya Hamas kwa hakika ni kule kule kuendelezwa njia ya wananchi wa Palestina yaani kupambana kwa muda mrefu na kudumishwa muqawama tangu kujiri mapinduzi ya Shahid Izzudin Qassam.
-
Vyama vya Kiislamu Morocco vyapinga uhusiano wa nchi hiyo na Israel
Dec 13, 2020 07:22Vyama vya Kiislamu nchini Morocco vimepinga vikali uamuzi wa ufalme wa nchi hiyo wa kuafikia kuanzisha uhusiano na utawala haramu wa Israel kufuatia mapatano yaliyosimamiwa na Marekani.
-
Iran: Marekani inawashawishi wengine watoe muhanga kadhia ya Palestina
Dec 12, 2020 03:51Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imesema Marekani inazishawishi nchi zingine kutoa muhanga kadhia ya Palestina na kuwapa mkono wezi kwa njia mbali mbali.
-
Hizbullah: Tawala za Kiarabu katika eneo hazijawahi kuwa pamoja na Palestina
Dec 08, 2020 08:45Naibu Katibu Mkuu wa Harakati ya Hizbullah ya Lebanon amesema kuwa, tawala za Kiarabu zinazotenda jinai katika Mashariki ya Kati hazijawahi kuwa pamoja na Palestina wala kuunga mkono muqawama.