-
HAMAS yaomba mabunge na viongozi wa dunia waisaidie na kuiunga mkono Palestina
Aug 19, 2020 06:27Kiongozi mwandamizi wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS ameyataka mabunge duniani pamoja na viongozi wa kisiasa watoe msaada na uungaji mkono kwa kadhia ya Palestina kwa ajili ya kukabiliana na njama za utawala haramu wa Kizayuni wa Israel.
-
Uhusiano wa UAE na Israel unalenga kutoa pigo kwa Muqawama na malengo matukufu ya Palestina
Aug 17, 2020 08:46Kiongozi mwandamizi wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS amesema, lengo la makubaliano yaliyofikiwa baina ya Imarati na utawala wa Kizayuni ni kutoa pigo la kuudhuru muqawama na malengo matukufu ya Palestina.
-
Harakati ya Kenya-Palestina yalaani mapatano ya UAE na Israel
Aug 16, 2020 02:16Harakati ya Mshikamano wa Kenya na Palestina imelaani vikali mapatano yaliyofikiwa baina ya watawala wa Umoja wa Falme za Kiarabu na utawala ghasibu wa Israel chini ya usimamizi wa makundi ya Kizayuni nchini Marekani.
-
Spika wa Bunge la Iran: Imarati imejidhalilisha kwa kuanzisha uhusiano na utawala wa Kizayuni
Aug 14, 2020 22:29Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) amesema kuwa makubaliano ya Imarati na utawala wa Kizayuni wa Israel ya kuanzisha uhusiano baina ya pande hizo mbili ni ya kijidhalilisha na ni usaliti kwa thamani za Umma wa Kiislamu na malengo ya taifa la Palestina.
-
Palestina yamrejesha nyumbani balozi wake Abu Dhabi baada ya Imarati kuanzisha uhusiano na Israel
Aug 14, 2020 05:04Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Serikali ya Mamlaka ya Ndani ya Palestina ametangaza kuwa balozi wa Palestina mjini Abu Dhabi ameitwa nyumbani kulalamikia hatua ya Imarati ya kuanzisha rasmi uhusiano wa kidiplomasia na utawala haramu wa Israel.
-
Iran: Uhusiano wa kidiplomasia wa Abu Dhabi na Tel Aviv ni ujinga wa kistratijia
Aug 14, 2020 03:37Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imelaani hatua ya kuanzishwa uhusiano wa kidiplomasia baina ya Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE au Imarati) na utawala wa Kizayuni wa Israel na kutaja hatua hiyo kuwa ni ujinga wa kistratijia ambao bila shaka utapelekea kuimarika mhimili wa muqawama na mapambano katika eneo.
-
Hamas: Wapalestina wanapaswa kuulinda Msikiti wa al Aqsa
Aug 11, 2020 02:14Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) imewataka Wapalestina wote kutetea na kuulinda Msikiti mtakatifu wa al Aqsa na kukabiliana na njama za utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya msikiti huo.
-
HAMAS yaonya kuhusu njama ya kuuyahudisha Msikiti wa Ibrahim (as)
Aug 09, 2020 03:43Msemaji wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS ametoa onyo dhidi ya hatua unazopanga kuchukua utawala wa Kizayuni wa Israel za kuuyahudisha Msikiti wa Nabii Ibrahim (as) ulioko katika mji wa Al Khalil huko Palestina inayokaliwa kwa mabavu.
-
Palestina yalaani mpango wa ujenzi wa vitongoji vya walowezi wa Kizayuni kaskazini mwa Quds
Aug 02, 2020 05:27Serikali ya Palestina imelaani hatua ya utawala ghasibu wa Israel ya kupasisha mpango wa ujenzi wa vitongoji vipya vya walowezi wa Kizayuni huko kaskazini mwa mji wa Quds (Jerusalem).
-
Vijana wa Kipalestina wakabiliana na Wazayuni waliotaka kuvamia Msikiti wa al-Aqswa
Jul 30, 2020 03:02Vijana wa Kipalestina wamekabiliana na walowezi wa Kizayuni waliokuwa wakifanya juhudi za kuvamia na kuingia katika Msikiti wa al-Aqswa.