-
UN: Kuzingirwa Ukanda wa Ghaza ni kuwaadhibu kwa umati Wapalestina
Jul 18, 2020 03:29Ripota na mtaalamu wa masuala ya haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa amesema kuwa, kuuzingira Ukanda wa Ghaza kunakofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel ni kuwaadhibu kwa umati wananchi wa Palestina.
-
Wimbi la malalamiko mitandaoni baada ya Google kuiondoa Palestina katika ramani ya dunia
Jul 17, 2020 03:38Shirika la intaneti la Google limejiwa juu na watumiaji wa mitandao mbali mbali ya kijamii baada ya kuiondoa "Palestina" katika ramani zake za dunia, na badala yake kupachika jina la "Israel."
-
Vyama mbalimbali Yemen vyapinga kuhuisha uhusiano na adui Mzayuni
Jul 16, 2020 22:12Washiriki katika kikao kilichofanyika Sana'a mji mkuu wa Yemen wakiwakilisha vyama mbalimbali vya siasa na wawakilishi wa Palestina wamesisitiza udharura wa kusimama imara na bega kwa bega na wananchi wa Palestina na kupinga aina zote za kuanzishwa uhusiano na utawala ghasibu wa Israel.
-
Mawaziri wa EU: Mwanya wa kuzuia uporaji wa ardhi za Wapalestina unazidi kuwa finyu
Jul 14, 2020 03:40Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Umoja wa Ulaya wametoa mwito kwa EU-mshirika mkubwa zaidi wa kibiashara wa Israel-kuchukua hatua za makusudi na haraka kuzuia mpango wa Tel Aviv wa kutwaa ardhi zaidi za Wapalestina katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan.
-
China: Uvamizi na uhasama dhidi ya Palestina haupaswi kuhalalishwa
Jul 07, 2020 03:08Waziri wa Mambo ya Nje wa China ameashiria kuhusu uungaji mkono wa nchi hiyo ya Asia kwa wananchi madhulumu wa Palestina na kusisitiza kuwa, kuhujumiwa haki za msingi za Wapalestina hakupaswi kuhalalishwa.
-
EU kuiadhibu Israel iwapo itatwaa ardhi ya Palestina ya Ukingo wa Magharibi
Jul 06, 2020 22:00Umoja wa Ulaya (EU) umetahadharisha kwamba, iwapo Israel itatekeleza uamuzi wake wa kulitwaa eneo la Ukingo wa Magharibi, mawaziri wa nambo ya Nje wa nchi wanachama katika umoja huo hawatafanya safari huko Israel.
-
Sisitizo la Kiongozi Muadhamu kuhusu Iran kuunga mkono taifa linalodhulumiwa la Palestina
Jul 06, 2020 21:58Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amejibu barua kutoka kwa mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) kuhusu matukio ya hivi karibuni ya Palestina.
-
Nchi za Amerika ya Latini zashinikiza vikwazo dhidi ya Israel
Jul 04, 2020 03:14Marais wa zamani na shakhsia wengine mashuhuri wa kisiasa wa nchi za Amerika ya Latini wamekosoa vikali mpango wa utawala haramu wa Israel wa kupora eneo la Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan na kuliunganisha na ardhi nyingine ya Palestina inayokaliwa kwa mabavu.
-
Maandamano ya kupinga ubaguzi Washington yabadilika na kuwa maandamano dhidi ya Israel
Jul 03, 2020 22:37Maandamano ya kupinga ubaguzi wa rangi yanayofanywa na wanachi wa Marekani katika mji mkuu wa nchi hiyo, Washington jana yalibadilika na kuwa maandamano dhidi ya utawala ghasibu wa Israel.
-
Msemaji wa Hamas: njia pekee ya kuwafukuza Wazayuni ni muqawama
Jul 02, 2020 02:14Msemaji wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) amesema kuwa njia pekee ya kuwarejsha nyuma Wazayuni ni kuendeleza mapambano na kuongeza kuwa: Maandamano yanayofanywa na wananchi wa Palestina katika maeneo mbalimbali yametuma ujumbe kwamba wataendeleza muqawama na mapambano hadi kupatikane ushindi.