-
Israel yavunja zaidi ya misikiti na makanisa 50 Palestina
Sep 25, 2017 00:40Walowezi wa Kizayuni wamevunja misikiti na makanisa yasiyopungua 53 katika kipindi cha miaka minane (8) iliyopita katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu na Wazayuni.
-
Wapalestina wawasilisha ushahidi wa jinai za Israel dhidi yao ICC
Sep 20, 2017 22:02Mawakili na wanaharakati wa kutetea haki za binadamu wa Palestina wamewasilisha ushahidi mbele ya Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC inayothibitisha kuwa vyombo vya dola vya utawala wa Kizayuni wa Israel vimehusika katika jinai dhidi yao.
-
Mfalme wa Bahrain ataka nchi za Kiarabu ziache kususia Israel
Sep 18, 2017 09:35Mfalme Hamad bin Isa Aal Khalifa wa Bahrain amezitaka nchi za Kiarabu kuacha kuusussia utawala haramu wa Israeli.
-
Umoja wa Mataifa: Wapalestina 19 wameuawa shahidi tangu kuanza mwaka huu
Sep 16, 2017 23:18Ofisi ya Uratibu wa Masuala ya Kibinadamu ya Umoja wa Mataifa (OCHA) katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu imetangaza kuwa, Wapalestina 19 wameuawa shahidi tangu ulipoanza mwaka huu wa 2017.
-
Brigedi ya Izzudeen Qassam yatangaza himaya yake kwa Waislamu wa Myanmar
Sep 16, 2017 09:17Brigedi ya Izzudeen Qassam tawi la kijeshi la Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS imefanya gwaride kubwa kama ishara ya kufungmana na wananchi Waislamu wa Myanmar wanaokabiliwa na unyama na ukatili wa mabudha wanaosaidiwa na jeshi la nchi hiyo.
-
Upinzani wa Wapalestina dhidi ya mipango ya hadaa ya Rais Trump wa Marekani
Sep 15, 2017 22:05Kuongezeka hatua za upuuzaji wa haki za Wapalestina, zikiwemo za kuundwa nchi yao huru, katika kipindi cha utawala wa Rais Donald Trump wa Marekani, kumeongeza hasira na malalamiko ya wananchi hao wanaodhulumiwa na utawala kandamizi na ghasibu wa Israel katika siku za hivi karibuni.
-
Hamas: Tutafungamana na chaguo la muqawama ili kufanikisha malengo ya wananchi wa Palestina
Sep 14, 2017 03:28Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imesisitiza kuwa itaendelea kufungamana na chaguo la muqawama kama njia pekee ya kufanikisha malengo ya wananchi wa Palestina katika ardhi yenye uhuru na kujitawala.
-
UN yalaani Israel kwa kuzuia maendeleo ya Palestina
Sep 13, 2017 03:14Umoja wa Mataifa umeulaani utawala wa Kizayuni wa Israel kwa kuzuia maendeleo pamoja na kuzorotesha hali ya kibinadamu katika ardhi za Palestina zilizo katika eneo la Quds Mashariki, Ukingo wa Maghribi na Ukanda wa Ghaza katika kipindi cha zaidi ya miaka 50 ya kukalia kwa mabavu maeneo hayo.
-
Jumuiya kubwa zaidi ya wafanyakazi Canada yasusia Israel
Sep 05, 2017 23:11Jumuiya kubwa zaidi ya wafanyakazi katika sekta binafsi nchini Canada imetangaza rasmi kujiunga na 'Harakati ya Ulimwengu ya Ususiaji wa Israel' maarufu kwa jina la BDS.
-
Larijani: Migogoro ya nchi za Kiislamu, sababu ya kusahauliwa Palestina
Sep 04, 2017 22:06Spika wa Majlisi ya Ushauri wa Kiislamu (Bunge la Iran) amesema kuwa, nchi nyingi za Kiislamu hivi sasa zina migogoro ya ugaidi na ya kiusalama, jambo ambalo limepelekea baadhi ya wanasiasa waisahau kadhia ya Palestina.