-
Kuadhibiwa waungaji mkono wa Palestina katika vyuo vikuu vya Marekani
Nov 12, 2023 23:17Licha ya madai ya kuheshimiwa uhuru wa kujieleza katika nchi za Magharibi ikiwemo Marekani, lakini ukweli wa mambo ni kwamba kuna mistari miekundu katika uwanja huo, likiwemo suala la kutetea kadhia ya Palestina, ambapo waungaji mkono wa taifa hilo linalodhulumiwa hukabiliwa na vikwazo vya aina mbalimbali vikiwemo vya kuadhibiwa na kufungwa jela.
-
Wananchi wa Kano Nigeria waandamana kulaani jinai za Israel Ukanda wa Gaza
Nov 12, 2023 09:40Maelfu ya Waislamu na waungaji mkono wa Palestina katika mji wa Kano, Nigeria wameandamana na kulaani jinai za utawala haramu wa Israel dhidi ya wananchi madhulumu wa Palestina hasa wa Ukanda wa Gaza.
-
Maafisa zaidi ya 1,000 wa serikali ya Marekani wamwandikia barua Biden kumtaka akomeshe jinai za Wazayuni
Nov 12, 2023 03:24Wafanyakazi zaidi ya elfu moja wa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Marekani wamesaini barua ya wazi na kumpelekea rais wa nchi hiyo Joe Biden kumtaka asimamishe jinai na mashambulizi ya utawala wa Kizayuni katika Ukanda wa Gaza na kusitishwa vita haraka katika Ukanda huo.
-
Ansarullah ya Yemen yakosoa vikali ulegevu walioonyesha watawala wa Kiarabu mbele ya Wazayuni
Nov 11, 2023 08:33Harakati ya Ansarullah ya Yemen imesisitiza kuwa itaendelea kuliunga mkono kwa dhati taifa na Muqawama wa Palestina katika Ukanda wa Gaza na imekosoa vikali udhaifu na ulegevu ulioonyeshwa na watawala wa nchi za Kiarabu mbele ya utawala dhalimu wa Kizayuni wa Israel.
-
Sheikh Al-Azhar wa Misri asisitiza juu ya ulazima wa kusitishwa jinai za utawala wa Kizayuni dhidi ya Wapalestina
Nov 11, 2023 02:42Sheikh wa Chuo Kikuu cha Al Azhar cha Misri amesisitiza juu ya ulazima wa kukomeshwa jinai na mashambulizi ya utawala wa Kizayuni dhidi ya Wapalestina.
-
Palestina yaishtaki Israel IAEA kwa kutishia kudondosha bomu la nyuklia Gaza
Nov 09, 2023 23:23Waziri wa Mambo ya Nje wa Palestina amewasilisha faili mbele ya Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA) kulalamikia matamshi ya vitisho ya waziri wa utawala wa Kizayuni kwamba ikilazimu, utawala huo haramu utatumia bomu la nyuklia dhidi ya watu wa Gaza.
-
Misri yapinga mpango wa kuindoa Hamas mamlakani Gaza
Nov 09, 2023 10:02Serikali ya Misri imeripotiwa kukataa pendekezo la Marekani la kutwaa kwa muda mamlaka katika Ukanda wa Gaza, ikisisitiza kuwa Cairo haitakuwa na nafasi yoyote katika kuondolewa madarakani Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) katika eneo hilo lililozingirwa.
-
Wananchi wa Morocco waandamana kuwaunga mkono Wapalestina wa Gaza
Nov 08, 2023 03:40Wananchi wa Morocco kwa mara nyingine tena wamefanya maandamano ya kuwanga mkono wananchi wa Palestina ambao wanakabiliwa na hujuma na mashambulizi ya kikatili ya utawala haramu wa Israel katika Ukanda wa Gaza.
-
Rais wa Iran: Kuendelea kwa mauaji ya Wapalestina kutaathiri ulimwengu
Nov 07, 2023 04:47Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema Tehran inaunga mkono juhudi za pamoja za kimataifa kwa ajili ya usitishaji vita mara moja, kuondoa mzingiro na kutoa misaada kwa watu wanaodhulumiwa wa Ghaza na kusisitiza kuwa: Mauaji ya watu wa Palestina yameyakasirisha mataifa yote huru duniani, na kuendelea kwa mauaji haya kutakuwa na matokeo mabaya hadi nje ya kanda ya Magharibi mwa Asia.
-
Maandamano ya kuwaunga mkono Wapalestina yafanyika Ujerumani, Italia
Nov 05, 2023 10:11Maelfu ya watu wamejitokeza mabarabarani katika mji mkuu wa Ujerumani, Berlin kushiriki maandamano ya kulaani jinai zinazoendelea kufanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya wananchi wa Palestina, huku idadi ya Wapalestina waliouawa shahidi hadi sasa katika mashambulizi dhidi ya Ukanda wa Gaza ikipindukia 10,000.