-
Spika wa Bunge: Iran iko wazi kwa diplomasia lakini usalama wa taifa na nguvu ya ulinzi haviwezi kujadiliwa
Dec 04, 2025 23:28Spika wa Bunge la Iran, Mohammad-Baqer Qalibaf amesema ingawa Iran iko wazi kwa diplomasia, lakini haitalegeza kamba katika suala la usalama wa taifa na nguvu zake za ulinzi.
-
Baraza Kuu la UN lapasisha azimio linaloitaka Israel iondoke katika maeneo ya Wapalestina
Dec 04, 2025 04:15Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa limepitisha rasimu ya azimio llinaloitaka Israeli iondoke kwenye maeneo ya Palestina iliyoyavamia na kuyakaliwa kwa mabavu tangu 1967, ikiwa ni pamoja na al-Quds Mashariki. Rasimu ya azimipia imeitaka Israel itambue haki ya watu wa Palestina ya kujitawala na kuasisi nchi huru.
-
Kampeni ya 'Komboa Mateka Wapalestina' walioko kwenye magereza ya Israel yazidi kupamba moto
Dec 01, 2025 02:15Maelfu ya waandamanaji jana Jumamosi walimiminika kwenye eneo la katikati mwa mji mkuu wa Uingereza, London katika maandamano ambayo ni sehemu ya kampeni ya "Komboa Mateka Wapalestina", wakitaka kuachiliwa huru Wapalestina zaidi ya 9,100 wanaoshikiliwa katika magereza ya kutisha ya utawala wa kizayuni wa Israel, wakiwemo zaidi ya wanawake na watoto 450.
-
Kwa mnasaba wa Siku ya Mshikamano, Iran yasema: Palestina ni jeraha kubwa zaidi linaloungulisha dhamiri ya wanadamu
Nov 29, 2025 23:49Kwa mnasaba wa maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Mshikamano na Watu wa Palestina, Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imesisitizia tena uungaji mkono usioyumba wa Jamhuri ya Kiislamu kwa wananchi madhulumu wa Palestina, ikiielezea hali yao kama "jeraha kubwa zaidi linaloungulisha dhamiri ya wanadamu."
-
Kwa kupiga marufuku shughuli za kundi la 'Palestine Action', Uingereza ni mtetezi kweli wa uhuru wa kutoa maoni?
Nov 28, 2025 23:12Kundi linalolitetea taifa madhulumu la Palestina nchini Uingereza liitwalo 'Palestine Action' limesema, kupigwa marufuku uendeshaji wa shughuli zake na serikali ya London ni hatua ya kidikteta.
-
Israel yatumia mfumo wa akili mnemba (AI) kufuatilia mitandao ya kijamii ya wanajeshi, ili kuzuia ushahidi wa uhalifu wa kivita
Nov 27, 2025 23:29Jeshi la Israel limezindua mradi mkubwa wa akili mnemba (AI), unaojulikana kama Morpheus, ili kuzuia askari wake kuchapisha ushahidi wa uhalifu wa kivita uliofanyika huko Gaza kwenye mitandao ya kijamii.
-
UNRWA: 90% ya Wapalestina Ghaza wanategemea msaada, wanapitisha siku kwa mlo mmoja
Nov 26, 2025 08:47Shirika la Umoja wa Mataifa la Kutoa Misaada na Ajira kwa Wakimbizi wa Palestina (UNRWA) limesema, hali ya kibinadamu katika Ukanda wa Ghaza ingali ni ya majanga licha ya kusitishwa mapigano, na kuonya kwamba vizuizi vinavyowekwa na utawala wa kizayuni wa Israel kwa uingizaji wa misaada vinaifanya hali ya eneo hilo isiweze kuboreka.
-
Baada ya Israel kuwaua Wapalestina wengine 24 Ghaza, HAMAS yataka wapatanishi, hasa US iingilie kati
Nov 23, 2025 03:35Jeshi la utawala wa kizayuni wa Israel limefanya mashambulizi makali ya anga katika maeneo tofauti ya Ukanda wa Ghaza, na kuwaua shahidi Wapalestina wasiopungua 24, wakiwemo watoto, katika mwendelezo wa ukiukaji wa makubaliano ya kusitisha mapigano yaliyofikiwa tangu wiki sita zilizopita kwenye eneo hilo la Palestina lililoteketezwa kwa vita.
-
Sababu za Ripota wa UN za kuonya kuhusu kuendelea Ulaya kuipa silaha Israel
Nov 21, 2025 22:54Umoja wa Mataifa umeonya kuhusu kuendelea nchi za Ulaya kuisheheneza silaha Israel licha ya kwamba kuna ushahidi wa kutosha na usiopingika wa jinsi utawala wa Kizayuni unavyotumia silaha hizo kufanya jinai na mauaji ya umati dhidi ya watu wasio na hatia.
-
Israel yafanya mashambulio ya kinyama Ghaza, yaua Wapalestina 28 na kujeruhi 77
Nov 20, 2025 02:39Wapalestina wasiopunguua 28 wameuawa shahidi katika wimbi jipya la mashambulizi ya kinyama yanayofanywa na jeshi la utawala wa kizayuni wa Israel kwenye Ukanda wa Ghaza, yakiwa ni moja ya ukiukaji mkubwa zaidi wa makubaliano ya kusitisha mapigano yaliyosimamiwa na Marekani na kuanza kutekelezwa mwezi uliopita wa Oktoba.