-
Qatar yakosoa taarifa ya mwisho ya mkutano wa Baraza la Ushirikiano la Ghuba ya Uajemi
Dec 10, 2018 03:05Qatar imekosoa taarifa ya mwisho ya mkutano wa Baraza la Ushirikiano la Ghuba ya Uajemi ikisema kuwa, imeangalia mambo kijuujuu na kuweka kando matatizo ya kweli yanayolikabili baraza hilo.
-
Qatar kujiondoa OPEC Januari 2019
Dec 03, 2018 04:33Qatar imetangaza kuwa itajiondoa katika Shirika la Nchi Zinazouza Mafuta kwa Wingi Duniani (OPEC) mwezi ujao wa Januari 2019.
-
Misri na Saudia zasema mzingiro dhidi ya Qatar utaendelea
Nov 28, 2018 04:11Saudi Arabia na Misri zimesema mzingiro na vikwazo zilivyoiwekea Qatar kwa zaidi ya mwaka mmoja sasa vitaendelea kwa muda usiojulikana, licha ya Doha kuwasilisha lalama zake mbele ya mahakama za kimataifa na taasisi za Umoja wa Mataifa ili kushinikiza kuhitimishwa mzingiro huo.
-
Baada ya kufeli njama zao sasa viongozi wa Saudia waanza kujipendekeza kwa Qatar
Oct 31, 2018 12:04Mfichuaji mmoja mkubwa wa ufisadia wa utawala wa Aal Saud amefichua kwamba viongozi wa ngazi za juu wa Saudi Arabia wamejipeleka kwa siri nchini Qatar lakini viongozi wa Doha wamewadhalilisha viongozi hao wa Saudia.
-
Waqatari wapinga kuhuishwa uhusiano na utawala wa Kizayuni
Oct 28, 2018 04:43Makundi mbalimbali ya wananchi wa Qatar yametangaza kuwa yanapinga kuhuishwa uhusiano wa nchi yao na utawala wa Kizayuni wa Israel sambamba na kushuhudiwa harakati za baadhi ya nchi za Kiarabu za kutaka kuhuisha uhusiano na utawala huo wa Kizayuni.
-
Waziri wa Ulinzi wa Qatar: Imarati na Saudia zinapaswa kuiomba radhi Qatar
Oct 27, 2018 23:04Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Ulinzi wa Qatar ameashiria matamshi yaliyotolewa hivi karibuni na Muhammad bin Salman kwamba Saudi Arabia ina hamu ya kuanzisha tena uhusiano na Qatar na kusisitiza kwamba: Nchi nne zilizoisusia na kuiwekea vikwazo Qatar zinapaswa ziiombe radhi.
-
Serikali ya Qatar nayo yaitaka Saudi Arabia kueleza walipo raia wake waliotekwa nyara na nchi hiyo
Oct 15, 2018 01:16Huku dunia ikiwa bado inaishinikiza Saudia kuweka wazi hatma ya mwandishi wa habari na mkosoaji wake aliyetoweka katika ubalozi wa nchi hiyo nchini Uturuki, serikali ya Qatar kupitia mkuu wa kamisheni ya kitaifa ya haki za binaadamu, ameitaka Riyadh kuieleza Doha kuhusu hatma ya raia wake waliotekwa nyara na utawala wa Aal Saud.
-
Ndege za Qatar Airways kuendelea na safari za Iran licha ya vikwazo vya Marekani
Oct 09, 2018 04:33Shirika la ndege la Qatar Airways limesema safari za ndege za shirika hilo za kwenda na kutoka Iran zitaendelea kama kawaida, licha ya vikwazo vya Marekani dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu.
-
Saudia, Imarati na Marekani kuunda muungano wa kijeshi Pembe ya Afrika
Oct 01, 2018 00:03Gazeti moja la nchini Qatar limefichua kuwa, Umoja wa Falme za Kiarabu kwa kushirikiana na Saudi Arabia zina nia ya kuunda muungano mwingine wa kijeshi wa nchi kadhaa katika eneo la Pembe ya Afrika.
-
Amir wa Qatar: Hitilafu zimelilemaza Baraza la Ushirikiano la Ghuba ya Uajemi
Sep 26, 2018 04:45Akizungumza jana usiku katika Mkutano wa 73 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa huko New York, Amir wa Qatar amekosoa vikwazo vya Saudi Arabia na waitifaki wake dhidi ya nchi yake na kusema hitilafu zilizopo zimelilemaza Baraza la Ushirikiano la Ghuba ya Uajemi.