-
Rais Erdoğan aichoma moyo Saudia, asisitiza kuendelea kuiunga mkono Qatar
Nov 16, 2017 04:39Katika kile kinachonekana kuwa ni kuwachoma moyo viongozi wa Saudi Arabia katika mgogogro unaoendelea kati ya nchi za eneo la Ghuba ya Uajemi, Rais Recep Tayyip Erdoğan wa Uturuki amesisitizia uungaji mkono wake kwa Qatar.
-
Qatar: Tutaimarisha na kulinda uhusiano wetu na Iran
Nov 13, 2017 11:55Waziri wa Mambo ya Nje wa Qatar amesema kuwa, Iran ni nchi jirani na nchi za Kiarabu za Ghuba ya Uajemi na kwamba Doha ina manufaa ya pamoja na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran hivyo haiwezi kukata uhusiano wake na Tehran.
-
Rais wa Uturuki akosoa kauli ya Mrithi wa Kiti cha Ufalme wa Saudi kuhusu Uislamu
Nov 12, 2017 04:08Katika msururu wa kurushiana maneneo viongozi wa Saudi Arabia na Uturuki, Rais Reccep Tayyip Erdogan wa Uturuki amekosoa vikali matamshi ya Mrithi wa Kiti cha Ufalme wa Saudia Mohammad Bin Salman kuhusu kile alichodai kuwa ni "Uislamu wa misimamo ya wastani."
-
Amir wa Qatar: Iran ndio njia pekee ya kupitishia chakula na dawa katika kipindi cha mzingiro
Oct 30, 2017 23:16Mfalme wa Qatar Sheikh Tamim bin Hamad Al Thani amesema Iran ndio njia pekee ya kupitishia chakula kwa ajili ya wananchi wa Qatar waliowekewa mzingiro; na akaongeza kwamba Saudi Arabia na nchi nyengine tatu za Kiarabu zinakula njama ya kuubadilisha utawala katika nchi yake.
-
Bahrain yataka Qatar ipokonywe uanachama wa baraza la PGCC
Oct 30, 2017 04:32Waziri wa Mambo ya Nje wa Bahrain, Khalid bin Ahmed Aal Khalifah ametoa mwito wa kuondolewa Bahrain kwenye Baraza la Ushirikiano wa Ghuba ya Uajemi (PGCC).
-
Amir wa Qatar awaonya wanaofanya njama za kuishambulia kijeshi nchi yake
Oct 29, 2017 12:25Amir wa Qatar, Tamim Bin Hamad al-Thani ameonya kuwa, hatua yoyote ya kijeshi dhidi ya nchi hiyo ndogo ya Ghuba ya Uajemi italitumbukiza eneo zima la Mashariki ya Kati katika machafuko.
-
Marekani iliratibu misaada kwa magaidi Syria, afichua waziri mkuu wa zamani wa Qatar
Oct 28, 2017 23:35Waziri Mkuu wa zamani wa Qatar Hamad bin Jassim amefichua namna Marekani ilivyokuwa ikishirikiana na Saudi Arabia, Uturuki na Qatar yenyewe katika kiwafikishia misaada magaidi kwa lengo la kuiondoa madarakani serikali ya Syria tokea mapigano yaanze nchini humo mwaka 2011.
-
Tillerson: Nchi zinazoizingira Qatar ndio wahusika wa kuendelea mgogoro na nchi hiyo
Oct 20, 2017 01:05Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Rex W. Tillerson amekiri wazi kwamba nchi zinazoshiriki katika kuizingira na kuiwekea vikwazo Qatar, ndio wahusika wa kuendelea mgogoro wa taifa hilo dogo la Kiarabu.
-
Imarati ilitaka kuivamia kijeshi Qatar kwa kutumia mamluki wa US
Oct 15, 2017 04:20Imebainika kuwa, Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) ulikula njama ya kuishambulia kijeshi Qatar, kwa kutumia maelfu ya mamluki waliopata mafunzo ya kijeshi kutoka kampuni moja ya Marekani.
-
Imarati yaitaka Qatar isiandae Kombe la Dunia 2022
Oct 09, 2017 04:25Afisa wa ngazi za juu wa usalama katika Umoja wa Falme za Kiarabu amesema mgogoro uliopo kati ya Doha na nchi kadhaa za Kiarabu zikiongozwa na Saudi Arabia utapatiwa ufumbuzi iwapo Qatar itaachana na azma yake ya kuwa mwenyeji wa Kombe la Dunia mwaka 2022.