-
Waislamu Nigeria wawakumbuka Mashahidi wa Siku ya Quds
May 12, 2025 11:14Taasisi ya 'Wakfu wa Shuhada' ya Harakati ya Kiislamu ya Nigeria imewakumbuka na kuwaenzi mashahidi 27 waliouawa na vikosi vya jeshi la nchi hiyo wakati wa maandamano ya amani ya Siku ya Quds ya 2025 huko Abuja, na kusisitiza kujitolea kwao kwa kadhia ya Palestina.
-
Ben-Gvir aagiza kufungwa ofisi ya Mfuko na Wakfu wa al-Quds
Apr 30, 2025 02:31Waziri wa wa Israel mwenye misimamo ya kufurutu ada, Itamar Ben-Gvir, ameamuru kufungwa kwa ofisi ya Mfuko na Wakfu wa al-Quds katika eneo la Quds Mashariki linalokaliwa kwa mabavu na utawala wa Kizayuni; huu ukiwa ni ukiukaji wa wazi wa kanuni za kimataifa, ukiashiria hatua nyingine ya kichokozi inayowalenga Wapalestina katika eneo hilo.
-
Mamilioni ya Wairani washiriki maandamano ya Siku ya Kimataifa ya Quds
Mar 28, 2025 07:45Wananchi Waislamu wa Iran kote nchini wamejitokeza kwa mamilioni kushiriki katika maandamano ya Siku ya Kimataifa ya Quds, kuonyesha mshikamano na Palestina, na kulaani ukatili wa utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya wananchi madhulumu wa Palestina hasa katika Ukanda wa Gaza.
-
Kiongozi Muadhamu: Siku ya Quds ya mwaka huu itakuwa ya aina yake
Mar 28, 2025 03:01Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei amesema maandamano ya Siku ya Kimataifa ya Quds mwaka huu yanayofanyika leo Ijumaa ya Machi 28 kote duniani yana umuhimu mkubwa kuliko miaka iliyopita.
-
Hamas yataka walimwengu wajitokeze kwa wingi kuiunga mkono Palestina Siku ya Quds
Mar 27, 2025 11:09Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina Hamas imetoa mwito wa kuhamasishwa walimwengu kujitokeza kwa wingi katika siku za Ijumaa, Jumamosi na Jumapili ili kuonyesha mshikamano na Gaza na al-Quds wakati huu ambapo Israel, kwa uungaji mkono wa Marekani, inaendelea na vita vyake vya mauaji ya halaiki dhidi ya Wapalestina Gaza, mkabala wa kimya cha dunia.
-
Ayatullah Khatami: Siku ya Quds itakuwa tofauti kabisa mwaka huu
Mar 29, 2024 12:12Khatibu wa Swala ya Ijumaa iliyoswaliwa hapa Tehran hii leo ameashiria jinai za utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza na kusema kuwa, hadithi ya Siku ya Kimataifa ya Quds mwaka huu, itakuwa hadithi tofauti kabisa kutokana na hamasa na wingi wa watu watakaoshiriki matembezi ya siku hiyo.
-
"Siku ya Quds imebakisha hai kadhia ya Palestina"
Mar 27, 2024 02:08Mkuu wa Makao Makuu ya Intifadha na Siku ya Quds ya Iran amesema maandamano ya Siku ya Kimataifa ya Quds yana umuhimu mkubwa katika kubakisha hai kadhia ya ukombozi wa Palestina.
-
OIC: Papua New Guinea imefanya makosa kwa kufungua ubalozi Quds
Sep 08, 2023 07:37Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) imekosoa vikali hatua ya Papua New Guinea kufungua ubalozi katika mji wa Quds unaokaliwa kwa mabavu na utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Spika wa Bunge la Iran: Uchokozi wa utawala wa Israel unathibitisha utambulisho wake wa kifashisti na kibaguzi
Apr 11, 2023 03:03Spika wa Majlisi ya Ushauri wa Kiislamu, Bunge la Iran, amesema vitendo vya kichokozi vilivyofanywa hivi karibuni na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Wapalestina katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu vinadhihirisha tabia ya utawala huo wa kifashisti na ubaguzi wa rangi.
-
Australia yatengua uamuzi wa kuitambua Quds kuwa mji mkuu wa Israel
Oct 18, 2022 07:37Serikali ya Australia imetangaza habari ya kubatilisha uamuzi wake tata wa kulitambua eneo la magharibi mwa Quds linalokaliwa kwa mabavu, eti kuwa ni mji mkuu wa utawala haramu wa Israel.