Feb 11, 2020 12:54
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Pombe Magufuli amemuagiza Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Selemani Jafo, kuhakikisha anamuandikia barua ya kumfukuza kazi mfanyakazi wa wizara hiyo aliyechana na kuitemea mate Qurani Takatifu mkoani Morogoro.