-
Rais Rouhani: Marekani, chanzo cha shari zote Asia Magharibi
Jan 19, 2020 03:27Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema Marekani ndiyo chanzo cha vitendo vyote vya shari, migogoro na matatizo katika eneo hili la Asia Magharibi.
-
Rais Rouhani: Taifa la Iran limekuwa imara zaidi katika kukabiliana na njama na vikwazo vya Marekani
Jan 16, 2020 11:26Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, Marekani inafuata njia ghalati kuhusu taifa la Iran. Ameongeza kuwa, taifa la Iran limezidi kuwa na nguvu na limekuwa imara zaidi mbele ya njama na vikwazo vya Marekani.
-
Rais Rouhani: Wananchi wa Asia Magharibi wahakikishe Marekani inaondoka katika eneo
Jan 15, 2020 12:43Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, kuna udharura kwa wananchi wa Asia Magharibi kufanya kila wawezalo kuhakikisha kwamba, majeshi ya Marekani yanaondoka katika eneo hili.
-
Rouhani: Iran ina irada ya kustawisha ushirikiano wa pande zote na Syria
Jan 14, 2020 13:14Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema Iran na irada ya kuimarisha na kustawisha uhusiano wa pande zote na Syria.
-
Rais Rouhani: Jopo la uchunguzi wa ajali ya ndege ya Ukraine libuniwe
Jan 14, 2020 12:04Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ametoa mwito wa kuundwa jopo maalumu la mahakama la kuchunguza ajali ya ndege ya Ukraine iliyoua watu 176 siku chache zilizopita hapa jijini Tehran, sanjari na kuwafikisha mbele ya sheria wahusika wa ajali hiyo.
-
Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amemtumia ujumbe wa pongezi Sultan mpya wa Oman
Jan 13, 2020 12:31Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ametuma ujumbe akimpongeza Haitham bin Tariq Al Said kuteuliwa kuwa Sultan mpya wa Oman na akasema anataraji kuwa uhusiano wa Tehran na Muscat utaimarika pakubwa katika nyanja zote.
-
Rais Rouhani: Kosa la kibinadamu kutokana na vitisho vya Marekani ndiyo sababu ya kuanguka ndege ya Ukraine
Jan 11, 2020 08:10Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, kosa la kibinadamu lililotokana na vitisho vya Marekani vya kushambulia maeneo nyeti nchini Iran ndiyo sababu ya kuanguka ndege ya abiria ya Ukraine karibu na Tehran.
-
Rais Rouhani wa Iran: Wamarekani wahitimishe hatua zao ghalati
Jan 10, 2020 12:03Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa anataraji kwamba Wamarekani watahitimisha hatua zao ghalati, lakini iwapo watatekeleza hatua nyingine iliyo dhidi ya maslahi ya Iran, basi watapata jibu kali mkabala.
-
Mashauriano ya kidiplomasia ya Iran kwa ajili ya kuarifisha jinai za Marekani
Jan 10, 2020 11:00Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema katika mazungumzo yake ya simu na viongozi wa nchi kadhaa jirani, nchi za Ulaya na Afrika kwamba Iran inaunga mkono amani na usalama lakini haitakaa kimya mbele ya vitimbi vya Marekani.
-
Rais Rouhani: Umoja wa Ulaya unapaswa kuwa na misimamo huru, usiburuzwe na Marekani
Jan 10, 2020 00:36Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, mahesabu ghalati na yenye madhara makubwa ya Marekani yanatokana na kushindwa nchi hiyo kuielewa vizuri Iran na eneo la Asia Magharibi. Amesisitiza kuwa, Umoja wa Ulaya unapaswa kuwa huru na usikubali kuburuzwa na Marekani na kuifanya Iran ikate tamaa kikamilifu na umoja huo.