-
Waafrika 1,700 wadaiwa kushiriki katika vita vya Russia, Ukraine
Feb 26, 2026 04:54Waziri wa Mambo ya Nje wa Ukraine, Andrii Sybiha amedai kwamba, zaidi ya Waafrika 1,700 wanapigana kwa niaba ya Russia katika vita vyake dhidi ya Ukraine, na kuongeza kwamba Moscow inatumia hadaa kuwasajili jeshini raia hao wa Kiafrika.
-
Kenya yaitaka Russia iirejeshee miili na raia wake waliofungwa katika vita vya Ukraine
Feb 21, 2026 11:07Serikali ya Kenya imeitaka Russia iirejeshe nyumbani miili ya raia wake waliouawa na wale waliokamatwa kama wafungwa wa vita, ambao wameripotiwa kuwa walipiigania Russia katika vita na Ukraine.
-
Mtazamo wa Moscow kuhusu maneva ya pamoja ya baharini kati ya Iran, Russia na China
Feb 21, 2026 09:11Moscow imetangaza kuwa mazoezi ya pamoja ya majini kati ya majeshi ya Iran, Russia na China yatafanyika katika Lango -Bahari la Hormuz.
-
Russia yakanusha madai ya kuwaajiri Wakenya katika vita vya Ukraine
Feb 20, 2026 07:12Russia imekanusha madai kwamba inawaajiri Wakenya kupigana vitani nchini Ukraine, kufuatia ripoti za Huduma ya Kijasusi ya Kitaifa ya Kenya kwamba zaidi ya Wakenya 1,000 kwa sasa wanapigana upande wa Russia katika mzozo huo.
-
Kremlin: Jeshi la majini la Russia kuzima 'uharamia' wa Magharibi
Feb 18, 2026 06:24Afisa mwandamizi wa Ikulu ya Russia (Kremlin) ameonya kwamba, yumkini jeshi la wanamaji la nchi hiyo likatumwa kuzuia mataifa ya Magharibi kukamata meli za Urusi kama sehemu ya vikwazo dhidi ya usafirishaji wa mafuta ya Moscow.
-
Kremlin: Russia haina mpango wa kushiriki mkutano wa 'Bodi ya Amani'
Feb 13, 2026 02:03Ikulu ya Russia ya Kremlin imethibitisha kwamba maafisa wa nchi hiyo hawana mpango wa kuhudhuria mkutano wa kwanza wa Bodi ya Amani (ya Gaza) uliopangwa kufanyika Februari 19 huko Washington.
-
Kengele ya hatari ya Russia kuhusu matokeo mabaya ya chokochoko yoyote dhidi ya Iran
Feb 11, 2026 10:29Serikali ya Russia imeonya kuhusu matokeo mabaya ya kuanzisha chokochoko yoyote dhidi ya Iran.
-
Ramaphosa na Putin wajadili suala la kuhitimisha vita kati ya Russia na Ukraine
Feb 11, 2026 06:55Rais wa Vladimir Putin wa Russia amefanya mazungumzo ya simu na mwenzake wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa ambapo pande hizo mbili zimejadili kuhusu suluhu inyoweza kufikiwa nchini Ukraine.
-
Trump apinga wito wa Putin wa kurefusha muda wa Mkataba wa New START
Feb 06, 2026 06:22Rais wa Marekani, Donald Trump amepinga pendekezo la Rais wa Russia, Vladimir Putin la kuongezwa kwa khiari muda wa Mkataba wa New START, unaoweka mipaka ya silaha za nyuklia, ambao muda wake ulimalizika jana Alkhamisi.
-
Rais wa Ukraine aliagiza jeshi liue 'makumi ya maelfu ya Warusi'
Jan 28, 2026 10:19Jeshi la Ukraine linapaswa lijikite katika kusababisha vifo vingi zaidi kwa Russia kadiri iwezekanavyo. Hayo yametamkwa na Rais wa Ukraine Vladimir Zelensky na kusisitiza kwamba, idadi ya vifo 50,000 vya Warusi kwa mwezi ni "kiwango bora" ambacho wanajeshi wa Ukraine wanapaswa wajitahidi kukifikia.