-
Kremlin: Russia haina mpango wa kushiriki mkutano wa 'Bodi ya Amani'
Feb 13, 2026 02:03Ikulu ya Russia ya Kremlin imethibitisha kwamba maafisa wa nchi hiyo hawana mpango wa kuhudhuria mkutano wa kwanza wa Bodi ya Amani (ya Gaza) uliopangwa kufanyika Februari 19 huko Washington.
-
Kengele ya hatari ya Russia kuhusu matokeo mabaya ya chokochoko yoyote dhidi ya Iran
Feb 11, 2026 10:29Serikali ya Russia imeonya kuhusu matokeo mabaya ya kuanzisha chokochoko yoyote dhidi ya Iran.
-
Ramaphosa na Putin wajadili suala la kuhitimisha vita kati ya Russia na Ukraine
Feb 11, 2026 06:55Rais wa Vladimir Putin wa Russia amefanya mazungumzo ya simu na mwenzake wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa ambapo pande hizo mbili zimejadili kuhusu suluhu inyoweza kufikiwa nchini Ukraine.
-
Trump apinga wito wa Putin wa kurefusha muda wa Mkataba wa New START
Feb 06, 2026 06:22Rais wa Marekani, Donald Trump amepinga pendekezo la Rais wa Russia, Vladimir Putin la kuongezwa kwa khiari muda wa Mkataba wa New START, unaoweka mipaka ya silaha za nyuklia, ambao muda wake ulimalizika jana Alkhamisi.
-
Rais wa Ukraine aliagiza jeshi liue 'makumi ya maelfu ya Warusi'
Jan 28, 2026 10:19Jeshi la Ukraine linapaswa lijikite katika kusababisha vifo vingi zaidi kwa Russia kadiri iwezekanavyo. Hayo yametamkwa na Rais wa Ukraine Vladimir Zelensky na kusisitiza kwamba, idadi ya vifo 50,000 vya Warusi kwa mwezi ni "kiwango bora" ambacho wanajeshi wa Ukraine wanapaswa wajitahidi kukifikia.
-
Medvedev: Yumkini mataifa mengi zaidi yakaunda silaha za nyuklia
Jan 26, 2026 10:11Naibu Mwenyekiti wa Baraza la Usalama la Russia, Dmitry Medvedev amesema kuna uwezekano mataifa zaidi kuzalisha silaha za nyuklia kutokana na kuongezeka ukosefu wa utulivu duniani.
-
Putin: Denmark imekuwa ikiitazama Greenland kama koloni lake
Jan 22, 2026 06:01Rais wa Russia, Vladimir Putin amesema, Denmark imekuwa ikiichukulia Greenland kama koloni lake. Amesema hayo akitoa mtazamo wake kuhusu mpango wa Rais wa Marekani, Donald Trump wa 'kukinunua' kisiwa hicho cha Aktiki kinachojitawala.
-
Russia yasisitizia tena haki ya Iran ya kunufaika na nishati ya nyuklia kwa malengo ya amani
Jan 21, 2026 02:39Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia Sergey Lavrov amesisitizia tena haki ya Iran ya kutumia nishati ya nyuklia kwa malengo ya amani.
-
Russia: Badala ya Ulaya kuzungumzia hali ya Iran ifuatilie kuiokoa Greenland
Jan 15, 2026 10:27Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia, Maria Zakharova amesema, badala ya viongozi wa Umoja wa Ulaya, EU kutoa matamshi ya kuzungumzia hali ya Iran, ingekuwa bora kama wanegejikita kushughulikia kadhia ya Greenland, ambayo sasa hivi Marekani inafanya juu chini kuitia mkononi.
-
Medvedev 'amdhihaki' Trump: Usipoharakisha, Greenland itapiga kura ya kujiunga na Russia
Jan 13, 2026 10:29Naibu Mwenyekiti wa Baraza la Usalama la Russia Dmitry Medvedev amesema, Wagreenland wanaweza kupiga kura ya maoni ya kujiunga na Russia ikiwa Rais wa Marekani Donald Trump hatachukua hatua haraka kukinyakua kisiwa hicho cha ncha ya kaskazini, Aktiki.