-
Vitisho vya Marekani vya kuwawekea vikwazo waitifaki wake iwapo watanunua silaha za Russia
Oct 04, 2019 05:33Mwenendo wa Marekani wa kuchukua hatua za upande mmoja na nchi hiyo kupanua ubeberu wake katika kipindi cha Rais Donald Trump, umeshika kasi zaidi na sasa umechukua sura mpya.
-
Hatua za uhasama za Marekani dhidi ya Venezuela na radiamali ya Russia
Oct 01, 2019 07:46Katika kipindi cha uongozi wa Rais Donald Trump, Marekani imejikita zaidi katika suala la kuipindua serikali ya mrengo wa kushoto nchini Venezuela na kumuondoa madarakani Rais wa nchi hiyo Nicolas Maduro na kisha kuiweka uongozini serikali ambayo ni mshirika wake kwa uongozi wa kinara wa upinzani Juan Guaido.
-
Ukosoaji mkali wa Sergey Lavrov kuhusiana na miamala haribifu ya Marekani dhidi ya mapatano ya JCPO na Ghuba ya Uajemi
Sep 29, 2019 23:06Hatua zilizo kinyume cha sheria za Marekani kujiondoa katika mapatano ya nyuklia ya JCPOA mwezi Mei mwaka jana na kisha kuiwekea Iran vikwazo vikali ambavyo vilikuwa havijawahi kushuhudiwa tena huko nyuma, na baada ya hapo kuzidisha uwepo wake wa kijeshi katika Ghuba ya Uajemi ambao umeshadidisha mizozo katika eneo hilo la kistratijia, ni mambo ambayo yameizidishia wasi wasi serikali ya Russia.
-
Trump akiri: Marekani inaingilia chaguzi zinazofanyika katika nchi nyingine
Sep 28, 2019 22:57Katika kipindi cha Vita Baridi (Cold War) na baada ya vita hivyo Marekani ilikuwa ikitekeleza sera za kuingilia masuala ya ndani ya nchi nyingine. Moja ya mambo muhimu yanayodhihirisha ukweli huo ni mienendo ya Marekani ya kuingilia chaguzi katika nchi mbalimbali kwa lengo la kuwaingiza madarakani viongozi vibaraka na wanaofuata siasa za Marekani.
-
Duru mpya ya hujuma za vikwazo vya Marekani dhidi ya nchi zingine
Sep 28, 2019 04:29Marekani ina rekodi kubwa zaidi ya kutumia aina mbali mbali za vikwazo dhidi ya nchi zingine kwa ajili ya kufikia malengo ya siasa zake za nje. Ushadidishaji vikwazo unaofanywa na Washington katika kipindi cha urais wa Donald Trump umekuwa ukipingwa na kulaaniwa kimataifa. Pamoja na hayo kinachoendelea kushuhudiwa kila uchao ni kutangazwa vikwazo vingine vipya vya Marekani dhidi ya nchi zingine duniani.
-
Gazeti la Washington Post lachapisha ripoti yenye utata dhidi ya Rais Donald Trump
Sep 28, 2019 04:20Gazeti la Washington Post la nchini Marekani limeripoti kwamba, Rais Donald Trump wa nchi hiyo aliwahi kuwaeleza viongozi wawili wa ngazi ya juu wa Russia kuwa, uingiliaji wa Moscow katika uchaguzi wa Marekani, halikuwa jambo la kutia wasi wasi kwa kuwa hata Washington nayo huwa inafanya hivyo katika nchi nyingine za dunia.
-
Raia wanane wa Russia wauawa nchini Libya
Sep 27, 2019 03:22Wanajeshi wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa ya Libya wamesema kuwa, shambulio la anga lililofanywa na wanamgambo wa jenerali muasi Khalifa Haftar huko kusini mwa Tripoli, mji mkuu wa Libya, limeua raia wanane wa Russia.
-
Taasisi ya Russia yafichua maovu ya "Kundi la Kofia Nyeupe nchini Syria"
Sep 22, 2019 23:18Taasisi isiyo ya kiserikali ya Russia kwa jina la the Fund for Research of Problems of Democracy imefichua kuwa, lengo kuu la kundi la kigaidi la "Kofia Nyeupe" huko Syria ni kuchapisha taarifa na habari za uwongo na zisizo sahihi dhidi ya serikali ya nchi hiyo na kuhusu hali ya mambo nchini.
-
Russia: Marekani iache kuibua mizozo Asia Magharibi
Sep 20, 2019 23:29Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia, amekosoa hatua za Marekani za kuibua mizozo eneo la Asia Magharibi (Mashariki ya Kati.)
-
Russia yataka uchunguzi huru kuhusu shambulio la visima vya mafuta vya Saudia
Sep 19, 2019 21:56Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia ametoa mwito wa kufanyika uchunguzi huru usiopendelea upande wowote kuhusu shambulizi dhidi ya taasisi za mafuta za ARAMCO za Saudi Arabia.