-
Mazungumzo ya Mawaziri wa Mashauri ya Kigeni na wa Ulinzi wa Russia na Misri
May 15, 2018 09:10Mawaziri wa Mashauri ya Kigeni na wa Ulinzi wa Russia na Misri wamefanya mazungumzo ya pamoja katika mji mkuu wa Russia Moscow na kubadilishana mawazo kuhusiana na uhusiano wa pande mbili pamoja na masuala ya kieneo.
-
Zarif: Russia yasema itaheshimu mapatano ya nyuklia hata baada ya Marekani kujiondoa
May 14, 2018 09:05Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Mohammad Javad Zarif amesema Russia imethibitisha kuwa itaendelea kuheshimu mapatano ya nyuklia ya Iran ambayo ni maarufu kama Mpango Kamili wa Pamoja wa Utekelezwaji, JCPOA, hata baada ya Marekani kujiondoa.
-
Majibu makali ya Russia kwa vikwazo vipya vya Marekani
May 12, 2018 02:38Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia imetoa tamko kali la kujibu vikwazo vipya vya Marekani dhidi yake na kusema kuwa, vikwazo hivyo vya serikali ya Donald Trump dhidi ya Moscow vinatokana na hamaki za Washington za kushindwa mashambulizi yake ya tarehe 14 Aprili nchini Syria.
-
Kuanza kipindi cha nne cha urais wa Vladmir Putin, utendaji, mipango na changamoto
May 08, 2018 08:46Rais Vladmir Putin wa Russia ambaye tarehe 18 Machi mwaka huu alishinda uchaguzi wa saba wa rais nchini humo, aliapishwa Jumatatu ya jana kwa ajili ya kipindi cha nne cha urais wa taifa hilo.
-
Indhari ya Russia kuhusu kufutwa makubaliano ya JCPOA na taathira zake mbaya
May 05, 2018 07:39Serikali ya Russia imetoa taarifa ikisisitiza kuwa makubaliano ya nyuklia ya JCPOA ni utaratibu ulio na mlingano weenye manufaa ya pande zote na kutahadharisha kuwa kuvunjwa makubaliano hayo kutakuwa kwa madhara. Kwa mujibu wa taarifa hiyo ya Russia, kuvurugwa mlingano unaolegalega wa kimaslahi ndani ya makubaliano ya JCPOA kutakuwa na taathira kuu kwa usalama wa kimataifa na muundo unaopiga marufuku uenezaji wa silaha za nyuklia.
-
Russia: Iwapo Marekani itajitoa katika JCPOA, itabidi iwekewe vikwazo
May 05, 2018 03:22Afisa mmoja wa Russia amesisitiza kuwa, kama Marekani itajitoa katika mapatano ya nyuklia ya JCPOA, itabidi iwekewe vikwazo vya kimataifa.
-
Msimamo wa kiuhasama wa Waziri mpya wa Mambo ya Nje wa Marekani dhidi ya Russia
Apr 29, 2018 22:09Ijumaa iliyopita Mike Pompeo, Waziri mpya wa Mambo ya Nje wa Marekani akizungumza kando ya mkutano wa mawaziri wa mambo ya nje wa nchi zinazounda Muungano wa Kijeshi wa Nchi za Magharibi (NATO) mjini Brussels Ubelgiji, alitaka 'kuwepo mabadiliko ya wazi katika hatua za Russia na vilevile kuitaka ifuate sheria za kimataifa'.
-
Zarif: Mchakato wa Astana ndio njia pekee ya kupatikana amani endelevu Syria
Apr 28, 2018 23:24Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Mohammad Javad Zarif amesema Mchakato wa Amani wa Astana hivi sasa ni harakati pekee ambayo kwa ushirikiano na Umoja wa Mataifa na wengine inaweza kupelekea kupatikana amani adilifu na endelevu nchini Syria.
-
Iran, Russia, Uturuki zatoa tamko la pamoja kuhusu Syria
Apr 28, 2018 11:46Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Russia na Uturuki wametoa tamko la pamoja mwishoni mwa kikao chao cha mjini Moscow, Russia na kutilia mkazo wajibu wa kulindwa ardhi nzima ya Syria na haki ya kujitawala na kujiamulia lenyewe mambo yake taifa hilo la Kiarabu.
-
Russia yakosoa picha na video bandia zinazodai kujiri shambulizi la kemikali Syria
Apr 27, 2018 23:27Mwakilishi wa Russia katika Shirika la Kuzuia silaha za Kemikali, amekosoa kitendo cha kuenezwa picha na video zisizo na ukweli wowote zinazoonyesha kwamba kulijiri shambulizi la silaha za kemikali mjini Douma, Ghouta Mashariki nchini Syria.