Rais Vladimir Putin wa Russia amesema, Ukraine yenyewe si adui, lakini vinara wa Magharibi wanaoiunga mkono nchi hiyo ndio maadui halisi wa Russia.
Afisa wa ngazi za juu wa serikali ya Russia amekosoa misaada ya silaha ya Marekani kwa Ukraine, akisema inaziweka Moscow na NATO kwenye ncha ya makabiliano ya moja kwa moja ya kijeshi.
Jeshi la Russia limetangaza mafanikio makubwa ya kuwatimua askari wa Ukraine kutoka Jamhuri ya Watu wa Luhansk, eneo ambalo limetangaza kujitenga na Ukraine.
Naibu Waziri wa Hazina wa Marekani amekiri kuwa, pato la mafuta la Russia limeongezeka licha ya vikwazo ilivyowekewa Moscow na nchi za Magharibi.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia ameonya kuwa, hivi sasa kuna uwezekano walimwengu wakashuhudia kutoka Vita vya Tatu vya Dunia.
Mashirika ya kijasusi ya Marekani yamesema kuwa, hayajapata ushahidi wowote wa kuthibitisha madai ya rais wa nchi hiyo Joe Biden kuwa Russia imefanya mauaji ya kimbari nchini Ukraine.
Janet Yellen Waziri wa Fedha wa Marekani ameeleza kuwa, iwapo Russia itashiriki katika mikutano ya kundi la G-20 Marekani haitahudhuria mikutano hiyo. Amesema: Rais Joe Biden anataka Russia ifukuzwe ndani ya G-20.
Shirika la Fedha Duniani (IMF) limeonya kuwa, vikwazo dhidi ya Russia huenda vikadhoofisha na kuipotezea umashuhuri sarafu ya dola ya Kimarekani.
Msemaji wa Rais wa Russia Dmitry Peskov ameyataja matamshi yaliyotolewa na Rais Joe Biden wa Marekani dhidi ya mwenzake wa Russia, Vladimir Putin kuwa "hayakubaliki" na "hayawezi kusamehewa."
Mkuu wa sera za kigeni katika Harakati ya Mapambano ya Kiislamu Palestina (Hamas) amesema moja kati ya mafunzo yanayopatikana katika vita vya Russia na Ukraine ni kuwa, zama za ubabe wa Marekani duniani zimefika ukingoni.