-
The Independent: Kadhia ya Khashoggi imezidi kudhihirisha jinsi utawala wa Saudia ulivyo dhaifu
Oct 07, 2018 12:00Gazeti la The Independent linalochapishwa nchini Uingereza limeandika kuwa kusadifiana mkasa wa kuuliwa mwandishi wa habari mkoasoaji wa utawala wa Aal Saud sambamba na matamshi ya udhalilishaji yaliyotolewa na rais wa Marekani kuhusu Saudi Arabia kumezidi kudhihirisha jinsi utawala huo ulivyo dhaifu.
-
Waturuki waandamana mbele ya ubalozi wa Saudia wakitaka kuachiliwa huru Jamal Khashoggi
Oct 06, 2018 01:22Raia wa Uturuki wamefanya maandamano mbele ya ubalozi wa Saudia wakitaka kuachiliwa huru mwandishi wa habari wa Saudia ambaye ametoweka kwa siku kadhaa sasa.
-
Saudia, Imarati na Marekani kuunda muungano wa kijeshi Pembe ya Afrika
Oct 01, 2018 00:03Gazeti moja la nchini Qatar limefichua kuwa, Umoja wa Falme za Kiarabu kwa kushirikiana na Saudi Arabia zina nia ya kuunda muungano mwingine wa kijeshi wa nchi kadhaa katika eneo la Pembe ya Afrika.
-
Gazeti la Marekani: Hakuna nchi yoyote inayoifikia Saudia kwa kuunga mkono ugaidi
Sep 30, 2018 04:34Gazeti la The Boston Globe linalochapishwa nchini Marekani limekosoa siasa za undumakuwili za serikali ya nchi hiyo kuhusiana na ugaidi na kueleza kwamba hakuna nchi yoyote duniani ambayo imeifikia Saudi Arabia kwa kuunga mkono ugaidi.
-
Answarullah yakosoa vikali uhusiano wa Saudia na Israel; yasema tutaendelea kuwaunga mkono Wapalestina
Sep 27, 2018 03:55Msemaji wa harakati ya Answarullah ya nchini Yemen amekosoa vikali kitendo cha viongozi wa Saudia, Imarati na Bahrain cha kuonana na mkuu wa shirika la kijasusi la Israel huko New York Marekani na kusisitiza kuwa, wananchi wa Yemen hawatowaacha mkono kamwe ndugu zao Wapalestina.
-
Mazungumzo ya Waziri Mkuu wa Pakistan na viongozi wa Saudi Arabia
Sep 21, 2018 03:23Katika safari yake nchini Saudi Arabia Imran Khan, Waziri Mkuu wa Pakistan amekutana na kufanya mazungumzo na Mfalme Salman bin Abdul Aziz pamoja na Muhammad bin Salman mrithi wa kiti cha ufalme wa nchi hiyo.
-
Mshikamano wa Saudia na magaidi wa MKO, fitna nyingine za Aal Saud Mashariki ya Kati
Sep 20, 2018 03:08Kiongozi mmoja mkubwa wa zamani wa genge la kigaidi la MKO lenye historia ya kufanya ugaidi, mauaji na jinai kubwa dhidi ya wananchi na viongozi wa Iran amefichua namna Saudi Arabia inavyolisaidia kifedha genge hilo.
-
Saudia yachukua mkopo wa dola bilioni 11 kugharimia vita dhidi ya Yemen
Sep 18, 2018 09:38Wakati vita vilivyoanzishwa na Saudi Arabia dhidi ya wananchi wa Yemen vikiwa vinaendelea, Mfuko wa Kifalme wa nchi hiyo umetangaza kuwa utawala wa Riyadh umepokea mkopo wa kwanza wa kimataifa wa dola bilioni 11 kwa ajili ya kulipia deni la nchi hiyo.
-
Viongozi wa Eritrea na Ethiopia wasaini makubaliano ya amani, uhusiano wazidi kuimarika
Sep 17, 2018 10:52Viongozi wa Ethiopia na Eritrea wametia saini makubaliano ya amani huku uhusiano wa nchi hizo mbili jirani zilizokuwa na uadui mkubwa ukizidi kuimarika siku baada ya siku.
-
Ndege za kivita za Saudia zaua watu 15 Hudaydah, Yemen
Sep 15, 2018 09:28Watu wasiopungua 15 wamepoteza maisha kufuatia hujuma ya ndege za kivita za Saudia katika barabara ya kistratijia inayounganisha mji mkuu wa Yemen, Sana'a na mji wa bandarini wa Hudaydah magharibi mwa nchi hiyo.