-
Mgogoro wa Riyadh na Doha wasababisha idadi ya Mahujaji wa Qatar kupungua
Aug 29, 2017 03:05Athari za mgogoro kati ya Doha na Riyadh zimeathiri pakubwa idadi ya Mahujaji wa Qatar walioenda kutekeleza ibada tukufu ya Hijja mwaka huu nchini Saudi Arabia.
-
Wanamfalme wanaomuunga mkono bin Nayef wafungwa jela ya siri na Bin Salman, Saudia
Aug 28, 2017 10:29Duru za habari nchini Saudia zimeripoti kwamba, Mohammad bin Salman bin Abdulaziz Aal Saud, mrithi wa kiti cha ufalme nchini humo anatumia jela za siri kuwafunga wanamfalme wengine wanaomuunga mkono Muhammad bin Nayef, mrithi wa kiti cha ufalme aliyefutwa kazi.
-
Wayemen waandamana kulaani ukatili wa Saudia dhidi yao
Aug 27, 2017 03:13Mamia ya maelfu ya wananchi wa Yemen kwa mara nyingine tena wamefanya maandamano katika mji mkuu Sana'a kulaani ukatili na mashambulizi ya kila uchao ya Saudi Arabia dhidi ya nchi hiyo maskini.
-
Ndege za kivita za Saudia zimeua raia 56 Yemen katika wiki moja
Aug 26, 2017 02:23Hujuma za ndege za kivita za Saudia zimeua raia zaidi ya 56 kote Yemen wakiwemo wanawake na watoto katika kipindi cha wiki moja iliyopita.
-
Waislamu milioni 1.4 wameshawasili Saudia kutekeleza Ibada ya Hija
Aug 25, 2017 03:14Zaidi ya Waislamu milioni 1.4 wameshawasili Saudi Arabia hadi hivi sasa kwa ajili ya kutekeleza ibada ya kila mwaka ya Hija ambayo inaanza wiki ijayo.
-
Raia 35 wauawa katika mashambulio ya kijeshi ya Saudia nchini Yemen
Aug 23, 2017 09:32Kwa akali watu 35 wameuawa nchini Yemen na makumi ya wengine kujeruhiwa kufuatia mashambulio ya anga ya ndege za kijeshi za utawala vamizi wa Saudi Arabia katika mji mkuu Sana'a.
-
Makumi ya watu wauawa Yemen katika shambulio la anga la Saudia dhidi ya maeneo ya raia
Aug 23, 2017 03:35Watu wasiopungua 30 wameripotiwa kuuawa katika mashambulio yaliyofanywa na ndege za kivita za utawala vamizi wa Saudi Arabia katika eneo la makaazi ya raia katika mkoa wa Sana'a mji mkuu wa Yemen.
-
Zarif: Iran inakaribisha kubadilika sera za kieneo za Saudi Arabia
Aug 23, 2017 03:13Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema: Ikiwa Saudi Arabia itaangalia upya siasa na sera zake za eneo la Mashariki ya Kati itapata jibu na radiamali chanya ya Jamhuri ya Kiislamu.
-
Qatar: Tunaishitaki Saudia kwa kutishia kushambulia ndege zetu za abiria
Aug 21, 2017 03:53Serikali ya Qatar imetangaza kuwa imekusudia kuishitaki Saudi Arabia katika Umoja wa Mataifa kutokana na nchi hiyo kutishia kuzishambulia ndege zake za abiria.
-
Qatar yafichua nyaraka za uungaji mkono wa Saudia na Imarati kwa magaidi wa Al-Qaeda nchini Yemen
Aug 20, 2017 21:57Qatar imefichua nyaraka zinazoonyesha kuwa Saudi Arabia na Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) zinawaunga mkono magaidi wa mtandao wa Al-Qaeda na kundi la kitakfiri la Daesh (ISIS) nchini Yemen.