Mar 21, 2023 02:26
Miaka 20 iliyopita, Machi 20, 2003, George W. Bush, Rais wa Marekani, aliamuru mashambulizi dhidi ya Iraq bila idhini ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa na kwa hatua ya upande mmoja na kinyume cha sheria kwa ushirikiano wa Waziri Mkuu wa Uingereza Tony Blair. Majeshi ya Marekani na Uingereza yalianzisha vita vikubwa dhidi ya Iraq na kupelekea kuanguka utawala wa Baath ulioongozwa na dikteta Saddam.