-
Jeshi la Somalia lamkamata kamanda mkuu wa al-Shabaab
Jul 26, 2021 07:57Jeshi la Taifa la Somalia limetangaza habari ya kumtia mbaroni kiongozi wa ngazi ya juu wa kundi la kigaidi na kitakfiri la al-Shabaab kusini mwa nchi hiyo.
-
Ilhan Omar ataka ufafanuzi wa Biden juu ya shambulio la anga Somalia
Jul 24, 2021 20:50Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi la Marekani kwa tiketi ya chama cha Democratic amemuandikia barua Rais Joe Biden wa nchi hiyo, akitaka ufafanuzi na maelezo kuhusu shambulio la kwanza la anga lililofanywa na utawala wake nchini Somalia.
-
Magaidi 50 wa kundi la al-Shabab Somalia waangamizwa na jeshi
Jul 21, 2021 07:36Jeshi la Somalia limetangaza kuwa, magaidi wasiopungua 50 wa kundi la al-Shabab wameangamizwa kufuatia shambulio la anga dhidi ya ngome zao katikati mwa nchi hiyo ya Pembe ya Afrika.
-
Shambulio la kigaidi laua na kujeruhi watu 13 katika mji mkuu wa Somalia, Mogadishu
Jul 10, 2021 07:19Watu 13 wameuawa na kujeruhiwa baada ya gari lililotegwa bomu kuripuka katika mji mkuu wa Somalia, Mogadishu.
-
Watu 10 wauawa baada ya gaidi kujiripua Mogadishu, Somalia
Jul 03, 2021 08:10Kwa akali watu kumi wameuawa baada ya gaidi aliyekuwa amejifunga mabomu kujiripua katika mkahawa mmoja wenye shughuli nyingi kwenye makutano ya barabara ya Jubba, katika mji mkuu wa Somalia, Mogadishu.
-
Somalia yatangaza tarehe ya uchaguzi wa rais
Jun 30, 2021 06:32Baada ya kushuhudiwa miezi kadhaa ya mkwamo wa kisiasa nchini Somalia, hatimaye viongozi wa nchi hiyo ya Pembe ya Afrika wameafikiana kuhusu tarehe ya kufanyika uchaguzi usio wa moja kwa moja wa rais.
-
Biden atafakari kuvirejesha vikosi vya Marekani nchini Somalia
Jun 17, 2021 03:04Rais wa Marekani, Joe Biden anatafakari kuwarejesha wanajeshi wa nchi hiyo huko Somalia, eti kwenda kusaidia juhudi za kupambana na magaidi wa kundi la ukufurishaji la al-Shabaab.
-
Makurutu 15 wa kijeshi wauawa katika shambulio la kigaidi, Somalia
Jun 15, 2021 22:05Kwa akali makurutu 15 wameuawa katika shambulio linaloaminika kuwa la kigaidi katika kambi moja ya mafunzo ya kijeshi huko Mogadishu, mji mkuu wa Somalia.
-
UN yawawekea vikwazo vinara wa kundi la kigaidi la Al Shabab
Jun 15, 2021 03:12Vinara watatu wa kundi la kigaidi la Al-Shabaab wameingizwa katika orodha ya vikwazo vya Umoja wa Mataifa ili kusaidia serikali ya Somalia kupambana na kundi hilo.
-
Baada ya US kuondoa askari wake Somalia, sasa yawatuma Kenya
Jun 13, 2021 22:02Rais wa Marekani, Joe Biden ametangaza kuwa serikali yake itatuma vikosi maalumu vya wanajeshi nchini Kenya, eti kwenda kusaidia juhudi za kupambana na magaidi wa kundi la ukufurishaji la al-Shabaab.