-
Katibu Mkuu wa UN ana wasiwasi kuhusu mkwamo wa kisiasa Somalia
Mar 26, 2021 03:22Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema mkwamo wa kisiasa unaondelea nchini Somalia kuhusu uchaguzi mkuu licha ya kufanyika duru kadhaa za majadiliano miongoni mwa wadau wa kisiasa nchini humo katika ngazi zote ni suala linalomtia wasiwasi mkubwa.
-
Raia kadhaa wauawa na kujeruhiwa katika shambulio la kombora mjini Mogadishu, Somalia
Mar 25, 2021 22:26Raia wasiopungua watatu wameuawa na wengine watano wamejeruhiwa baada ya makombora kadhaa kulenga ofisi kuu za vikosi vya Umoja wa Mataifa na vya Umoja wa Afrika vinavyolinda amani nchini Somalia (AMISOM) zilizoko katika mji mkuu wa nchi hiyo Mogadishu.
-
Somalia yazindua kampeni ya kitaifa ya utoaji chanjo ya Corona
Mar 17, 2021 01:10Rais Mohamed Abdullahi Farmaajo wa Somalia hapo jana alipokea chanjo ya Corona ya shirika la AstraZeneca la Uingereza, kuashiria kuanza kwa kampeni ya kitaifa ya utoaji wa chanjo ya Corona katika nchi hiyo ya Pembe ya Afrika.
-
UN yatilia mkazo umuhimu wa kufanyika uchaguzi kama ilivyopangwa nchini Somalia
Mar 13, 2021 23:09Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limepasisha azimio la kuitaka serikali ya Somalia kuitisha uchaguzi mkuu kama ilivyopangwa na bila ya kuuchelewesha.
-
Watu wasiopungua 20 wauawa, 30 wajeruhiwa katika mripuko wa bomu uliotokea Mogadishu, Somalia
Mar 06, 2021 00:03Watu wasiopungua 20 wameuawa na wengine 30 wamejeruhiwa katika shambulio la kigaidi la mripuko wa bomu lililotegwa garini uliotokea nje ya mkahawa mmoja ulioko karibu na bandari katika mji mkuu wa Somalia, Mogadishu.
-
Magaidi 52 wa al-Shabaab wauawa katika shambulio dhidi ya jela nchini Somalia
Mar 05, 2021 08:59Wanamgambo wasiopungua 52 wa kundi la kigaidi la al-Shabaab wameangamizwa katika shambulio la wapiganaji hao dhidi ya jela moja iliyoko katika jimbo la Puntland,kaskazini mashariki mwa nchi hiyo.
-
Wanasiasa wa upinzani Somalia waakhirisha maandamano dhidi ya serikali
Feb 26, 2021 09:20Wanasiasa wa upinzani nchini Somalia wameakhirisha maandamano yao waliyokuwa wamepanga kufanya leo Ijumaa baada ya Waziri Mkuu kuingilia kati.
-
Magaidi 15 wa al-Shabaab wauawa katika operesheni ya jeshi la Somalia
Feb 25, 2021 23:59Wanamgambo 15 wa kundi la kigaidi la al-Shabaab wameangamizwa katika operesheni ya jeshi la Somalia kusini mwa nchi.
-
Serikali ya Somalia yapiga marufuku maandamano ya wapinzani
Feb 24, 2021 04:47Serikali ya Somalia imetangaza kupiga marufuku maandamano ya wapinzani katika mji mkuu Mogadishu kutokana na ongezeko la maambukizi ya ya corona na tishio la usalama.
-
Magaidi 52 wa Ash-Shabaab waangamizwa kusini mwa Somalia
Feb 21, 2021 23:26Mkuu wa vikosi vya ulinzi vya Somalia ametangaza kuwa, wanamgambo 52 wa kundi la kigaidi la Ash-Shabaab wakiwemo vinara wawili wa kundi hilo wameuawa kusini mwa nchi hiyo.