-
Rais wa Somalia: Nchi za kigeni zinavuruga mchakato wa uchaguzi nchini
Feb 07, 2021 04:01Rais Muhammed Abdullahi Farmajo wa Somalia amesema uingiliaji wa madola ajinabi katika mambo ya ndani ya nchi hiyo ndiyo sababu kuu ya kugonga mwamba mazungumzo ya kujaribu kuupatia ufumbuzi mkwamo wa uchaguzi katika nchi hiyo.
-
Jeshi la Somalia lawaangamiza magaidi 8 wa al-Shabab walioshambulia ujumbe wa rais
Feb 06, 2021 01:13Jeshi la Somalia limetangaza kuwaangamiza magaidi 8 wa kundi la al-Shabab ambao waliushambulia kwa mizinga mkutano wa serikali uliokuwa unaongozwa na rais wa nchi hiyo.
-
Marekani inaendelea kuingilia Somalia kijeshi
Feb 02, 2021 22:58Kamandi ya Oparesheni Maalumu za Jeshi la Marekani barani Afrika imetangaza kuwa, Jeshi la Marekani limeanza kutoa mafunzo tena kwa Jeshi la Somalia hata baada ya kutangaza kuondoa askari wake katika nchi hiyo ya Pembe ya Afrika.
-
Umoja wa Mataifa wasisitiza kuhusu utatuzi wa kadhia ya wakimbizi Somalia
Feb 02, 2021 09:19Mratibu mkazi wa Umoja wa Mataifa na wa masuala ya kibinadamu nchini Somalia amesema wakimbizi wa ndani nchini humo ni mtihani mkubwa ambao unahitaji suluhisho la muda mrefu.
-
Mwakilishi wa UN Somalia alaani vikali shambulio la kigaidi la mjini Mogadishu
Feb 02, 2021 04:01Umoja wa Mataifa nchini Somalia umelaani vikali shambulizi la kigaidi lilofanywa Jumapili kwenye hotel ya Afrika katika mji mkuu Mogadishu na kusababisha vifo vya watu kadhaa na wengine wengi kusalia majeruhi.
-
Watu kadhaa wauawa katika shambulio la kigaidi la al-Shabaab Somalia
Jan 31, 2021 23:48Kwa akali watu watatu wameuawa huku wengine wengi wakijeruhiwa baada ya wanamgambo wa kundi la kigaidi la al-Shabaab kushambulia hoteli moja katika mji mkuu wa Somalia, Mogadishu kwa mabomu na risasi.
-
Uganda yakanusha madai kuwa jeshi lake limeua magaidi 189 wa al-Shabaab
Jan 28, 2021 00:49Serikali ya Uganda imekadhibisha taarifa kuwa jeshi la nchi hiyo UPDF limeua wanachama 189 wa genge la al-Shabaab kusini magharibi mwa mji mkuu wa Somalia, Mogadishu.
-
9 wauawa katika mpaka wa Kenya na Somalia, AU yatoa kauli
Jan 26, 2021 07:28Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika amesema amani katika mpaka wa Kenya na Somalia ni jambo muhimu kwa ajili ya uthabiti wa eneo zima la Afrika Mashariki na Pembe ya Afrika.
-
Jeshi la Uganda laua wanachama 189 wa al Shabab nchini Somalia
Jan 23, 2021 04:28Jeshi la Uganda UPDF limetangaza kuwa, wanajeshi wa nchi hiyo wameua wanachama 189 wa genge la al Shabab katika shambulizi la kushtukiza na la kasi kubwa nchini Somalia.
-
Mripuko waua watu 7 katika mji mkuu wa Somalia, Mogadishu
Jan 07, 2021 23:13Watu wasiopungua 7 wameuawa katika mripuko wa bomu uliotokea katika mji mkuu wa Somalia, Mogadishu.