-
9 waaga dunia katika ajali ya ndege Sudan, vita vyaingia siku ya 100
Jul 24, 2023 07:44Watu wasiopungua tisa wakiwemo wanajeshi wanne wameaga dunia baada ya ndege ya abiria iliyokuwa imewabeba kuanguka nchini Sudan, huku mapigano yaliyozuka katikati ya mwezi wa Aprili kati ya pande zinazoongozwa na majenerali hasimu nchini humo wanaowania madaraka yakiingia siku yake ya 100.
-
Sudan yaendelea kushuhudia mapigano makali katika miji mbalimbali
Jul 22, 2023 00:30Mapigano makali yameendelea kuripotiwa katika miji mbalimbali ya Sudan baina ya jeshi la nchi hiyo na kikosi cha usaidizi wa haraka huku kukiwa hakuna ishara za kumalizika vita hivyo hivi karibuni.
-
Jeshi la Sudan: Tuko tayari kuhitimisha vita na RSF kwa sharti la kusitishwa mashambulizi
Jul 14, 2023 08:35Baraza la Uongozi la Sudan limetangaza kuwa jeshi la nchi hiyo liko tayari kusitisha vita na Vikosi vya Usaidizi wa Haraka RSF, kwa sharti kwamba vikosi hivyo visimamishe mashambulizi na kuanza mazungumzo ya kisiasa ili kuunda serikali ya kiraia.
-
UN: Vita nchini Sudan vimepelekea watu zaidi ya milioni tatu kuwa wakimbizi
Jul 13, 2023 04:28Umoja wa Mataifa umeeleza kuwa vita vya karibu miezi mitatu huko Sudan vimepelekea watu zaidi ya milioni tatu kuwa wakimbizi na kutoa wito kwa pande zinazopigana kuwajibika.
-
Sudan yapinga majeshi ya kigeni kupelekwa nchini humo
Jul 12, 2023 23:28Sudan imepinga kutumwa wanajeshi wa kigeni nchini humo na kutangaza kuwa itawachukulia wanajeshi hao kuwa ni sawa na askari vamizi.
-
Indhari ya Katibu Mkuu wa UN ya kufikia Sudan kwenye ukingo wa vita kamili vya wenyewe kwa wenyewe
Jul 11, 2023 08:00Mapigano nchini Sudan yanaendelea kupamba moto, na juhudi zilizofanywa hadi sasa za kuleta suluhu na kurejesha amani na utulivu katika nchi hiyo sio tu hazijafanikiwa, lakini pande mbili zinazopigana zimeshadidisha pia mashambulizi yao. Kutokana na hali hiyo, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametahadharisha kuwa, Sudan sasa imeshafika kwenye ukingo wa vita kamili vya wenyewe kwa wenyewe.
-
Jeshi la Sudan lakataa kushiriki mkutano wa IGAD nchini Ethiopia
Jul 11, 2023 04:05Jeshi la Sudan limekataa kushiriki mkutano wa ngazi ya juu wa kuzindua mchakato wa amani wa nchi hiyo uliofanyika mjini Addis Ababa, Ethiopia; huku mapigano yakishtadi katika nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika.
-
Katibu Mkuu wa UN alaani shambulio la anga Sudan lililoua watu 22 Omdurman
Jul 10, 2023 03:53Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amelaani shambulizi la anga lililotokea Omdurman nchini Sudan, ambalo limeripotiwa kuua takriban watu 22.
-
Iran na Sudan kufufua uhusiano wao wa kidiplomasia karibuni
Jul 06, 2023 23:38Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amekutana na kufanya mazungumzo na mwenzake wa Sudan kwa mara ya kwanza baada ya miaka saba, ambapo wamekubaliana kufufua uhusiano wa kidiplomasia wa nchio mbili hizi karibuni hivi.
-
Baraza la Usalama latakiwa kushughulia jinai dhidi ya raia katika mapigano ya Sudan
Jun 28, 2023 23:22Asasi na jumuiya 41 zenye mfungamano na wanawake Afrika, zimelitaka Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kufuatilia na kushughulikia jinai dhidi ya raia nchini Sudan zinazofanywa na pande mbili hasimu katika vita vyao.