-
Gharibabadi: Nchi za Magharibi ziache sera za kinafiki na ubaguzi kuhusiana na ugaidi
Apr 18, 2024 10:05Katibu wa Baraza Kuu la Haki za Kibinadamu la Iran amesema kuwa, Marekani na nchi za Magharibi kwa ujumla zinapaswa kuachana na siasa zao za kindumakuwili na ubaguzi kuhusiana na ugaidi.
-
Abdollahian: Marekani inapasa kuwajibishwa kwa shambulio dhidi ya ubalozi mdogo wa Iran
Apr 09, 2024 04:35Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran ameeleza kuwa serikali ya Marekani ina jukumu na inapasa kubeba dhima kwa shambulio la kigaidi katika ubalozi mdogo wa Iran mjini Damascus lililofanywa na utawala wa Israel unaotekeleza mauaji ya kimbari huko Gaza.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran akosoa upuuzaji wa Umoja wa Ulaya kuhusu ugaidi wa Israel
Apr 04, 2024 04:18Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amekosoa misimamo ya undumakuwili ya Umoja wa Ulaya na upuuzaji wake kuhusiana na jinai na vitendo vya kigaidi vya utawala ghasibu wa Israel.
-
Kiongozi Muadhamu: Iran itaufanya utawala wa Israel ujutie uhalifu nchini Syria
Apr 02, 2024 10:01Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ametuma salamu za rambirambi kufuatia kuuawa shahidi Majenerali walioongoka wa Kiislamu katika shambulio la utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya ubalozi mdogo wa Iran nchini Syria na kusisitiza kwamba: "Taifa la Iran litawafanya Wazayuni wajutie jinai hiyo na jinai zingine kama hiyo."
-
Rais Raisi: Wazayuni kamwe hawatofikia malengo yao haramu
Apr 02, 2024 06:41Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amezungumzia jinai na ugaidi uliofanywa jana Jumatatu na utawala wa Kizayuni wa kushambulia ubalozi mdogo wa Iran mjini Damascus Syria na kusema kuwa, Wazayuni wanapaswa kutambua kwamba ugaidi wao wa kinyama kama huo hauwezi kuwafanikishia malengo yao maovu.
-
Iran: Utawala wa Kizayuni ni tishio kwa usalama na amani ya dunia nzima
Apr 02, 2024 06:36Mwakilishi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa na taasisi nyinginezo za kimataifa huko Geneva Uswisi amelaani vikali jinai za utawala wa Kizayuni wa Israel katika ubalozi mdogo wa Iran mjini Damascus Syria na kusema kuwa Israel ni utawala unaohatarisha usalama wa dunia nzima na unapuuza kikamilifu hati ya Umoja wa Mataifa.
-
Balozi wa Iran Syria: Tutajibu mapigo kwa Israel sawa na ilivyoshambulia ubalozi wetu mdogo
Apr 02, 2024 03:23Balozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini Syria amesisitiza kuwa, Jamhuri ya Kiislamu itajibu mapigo sawa na utawala wa Kizayuni wa Israel ulivyoshambulia ubalozi mdogo wa Iran mjini Damascus, Syria.
-
Watu 38 wauawa katika hujuma za anga za Israel Syria, Iran yalaani
Mar 29, 2024 08:28Kwa akali watu 38 wameuawa katika mashambulizi ya anga ya utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya mji wa Aleppo (Halab) huko kaskazini mwa Syria.
-
Waziri wa Ulinzi: Iran iko tayari kuisaidia Syria kuimarisha nguvu zake za kiulinzi na za kuzuia mashambulio
Mar 17, 2024 02:28Waziri wa Ulinzi wa Iran Brigedia Jenerali Mohammad Reza Ashtiani amesema Jamhuri ya Kiislamu iko tayari kutumia uwezo wake wote kuisaidia Syria katika kuimarisha ulinzi na uwezo wake wa kuzuia hujuma za Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Syria: Kuunga mkono jinai za Netanyahu kumefichua dhati ya Wamagharibi
Mar 11, 2024 07:53Waziri wa Mambo ya Nje wa Syria amezikosoa vikali nchi za Magharibi kwa kuendelea kuunga mkono jinai za kivita zinazofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Wapalestina wa Ukanda wa Gaza na kusisitiza kuwa, uungaji mkono huo umefichua dhati halisi ya Wamagharibi.